MAANDALIO YA MOYO NI YA MWANADAMU,BALI JAWABU LA ULIMI HUTOKA KWA BWANA. (Mithali 16 :1 ) * Sehemu ya pili *
Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Mtumishi Gasper Madumla |
Haleluya…
Bwana Yesu asifiwe…
Karibu katika sehemu ya pili ya fundisho hili la msingi,Dhumuni kuu la
fundisho hili ni kukupa ufahamu kuwa wewe mpendwa yakupasa uandae moyo
wako pindi uendapo kwa Bwana Mungu.Sasa ni jinsi gani waweza kuandaa
moyo wako ? Karibu tujifunze pamoja :
Nilikuambia kuwa Katika
kipindi cha maombi,mtu hupokea majibu yake pale aombapo,Ikiimaanisha
kuwa ukikaa kimya,usitegemee kupokea kitu chochote ,kwa sababu hujaomba,
Bali ukiomba utapata,na hii sio kana kwamba mtu huyo aombaye na
kujibiwa kwamba anajua kuomba sanaa,au anajua kuomba impasavyo ,Bali ni
kwa msaada wa Roho mtakatifu,kwanza akiwa AMEFANYA MAANDALIZI YA MOYO
WAKE.
Katika suala la '' Maandalizi ya Moyo '' Katika eneo
hilo ,ndipo lipo tatizo letu tulio wengi,na laiti kama tutaijua siri
iliyofichika hapa,Basi tutakuwa kila tuombapo twapokea kwa kadri ya
Roho mtakatifu apendavyo Yeye.
Mwanadamu amepewa jukumu la
kuandaa moyo wake ili apokee kile anachoomba.Moyo usioandaliwa hauwezi
kupokea yale ambayo mtu aombayo,Ndio maana andiko linatuambia ''
Maaandalizi ya moyo ni ya mwanadamu '' Hii ikimaanisha kuwa Mungu
hausiki kwa maandalizi ya moyo wako,Yeye anahusika kukupa jawapu la
ulimi wako kwa kadri apendavyo Yeye.
Hakuna awezaye kumpokea
Roho mtakatifu ikiwa hajafungua moyo wake kumpokea,Kitendo cha kufungua
moyo ni suala la maandalizi,na maandalizi haya ni jukumu la mtu binafsi.
Ndio maana hata Bwana Yesu asema “ Tazama, nasimama mlangoni, nabisha;
mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami
nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.” Ufunuo 3 :20.
Jambo la kwanza ni KUSIKIA SAUTI YA BWANA MUNGU maana kusikia kwaleta IMANI (Warumi 10 :17),
Pili ,ili umpokee Bwana Yesu,ni sharti UFUNGUE MOYO WAKO.
Naye Mungu wetu tazama alivyokuwa ni MUNGU wa Demokrasia maana
hakulazimishi ufungue mlango wako ,bali ukipenda waweza kufungua,naye
ataingia.
Namna ya kufungua mlango ni jambo la maandalizi ya
moyo, baada ya kusikia sauti ya BWANA MUNGU,labda tuangalie maandalizi
ya moyo huwaje ? kulingana na andiko letu la Mithali 16 :1.
MAANDALIZI YA MOYO/ The preparations of the heart.
Kumbuka,nilikuambia Moyo unaozungumziwa katika Biblia ni ROHO,na sio
moyo kama kiungo katika mwili wa binadamu,maana moyo wa mwanadamu ulio
kama
kiungo,hauwezi kuuandaa KUPOKEA MAMBO YA KI-UUNGU.
Wenyewe unakazi yake maalumu ya Kusukuma damu tu katika mwili ,Hivyo hausiki kabisa kwa kufanya maandalizi ya kiimani.
Najua hapa pia kuna tatizo sana ,maana watu hufikiri moyo unaotajwa
katika andiko hili ni moyo wa damu na nyama wenye kusukuma damu
mwilini,la hasha! Moyo ni ROHO kibiblia
Haleluya…
Bwana Yesu asifiwe…
Hivyo basi nisemapo '' Maandalizi ya moyo '' ni sawa na kusema '' Maandalizi ya ROHO ''
Maandalizi ya awali ya MOYO/ROHO ni kuilisha chakula.
Maana ROHO ndio itiayo uzima nafsi na mwili.
ROHO ikiwa haina chakula itakuwa dhaifu kiasi kwamba yavamiwa na chochote na pia baadaye hufa.
Sikia :
Kinachomuongoza mtu kutenda jambo lolote atendalo ni NAFSI au ROHO
kutegemea ni nani kati ya nafsi au roho aliyepo juu ya mwenzake.
Yaani ikiwa NAFSI atakuwa juu ya roho,basi ni dhahili mtu ataongozwa kwa
NAFSI,na mtu huyo ndio anayeitwa mtu wa MWILINI,ambaye hutawaliwa na
matendo ya mwilini.
Tunasoma Wagalatia 5 : 19-21 :
“ BASI MATENDO YA MWILI NI DHAHIRI,NDIYO HAYA , uasherati, uchafu, ufisadi,
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo
nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao
mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”
Lakini ikiwa
ROHO iatakuwa juu ya nafsi ndani ya mtu,Basi mtu huyo ataongozwa na
ROHO naye ndie mtu wa rohoni,mtu wa rohoni atatawaliwa na TUNDA LA ROHO
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema,
fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Wagalatia 5 : 22-23
Mpaka mtu aongozwe kwa roho,ipo kazi ya
ziada,sio rahisi,wala si mchezo mchezo tu,bali ni kuacha yote kwa ajili
ya ufalme wa Mungu.
Mungu anapokuwa namba moja katika maisha yako,unakuwa sio mtu wa kawaida.
Roho ili iwe kiongozi katika mwili ni lazima iwe na nguvu,Nguvu hupatikana katika chakula,Chakula cha roho ni NENO LA MUNGU.
ITAENDELEA...
UBARIKIWE.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments