Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
Mwanzo 2:24 "Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye
ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja." Ukiangalia (Zaburi
45:10-11 anasema, "Sikia, binti, utazame (maana yake anazungumza na
msichana), utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
Naye mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana
wako, nawe
umsujudie." maneno haya "Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako" yana
maana kuwa kwenu ndo unatoka maswala ya kurudi kwenu au tatizo
kukimbilia kwenu hairuhusiwi ni sawa watu wengi sana wanataka waingie
kwenye ndoa, waoe au waolewe, lakini uhusiano wao na wazazi wao
usibadilike, ambacho ni kitu hakiwezekani. Unapoamua kuolewa, wa kwanza
sio baba yako wala sio mama yako, wa kwanza ni mume wako baada ya Yesu.
Katika mahusiano ya kibinadamu anayekuja pale wa kwanza baada ya Yesu
moyoni mwako ni mume wako.
Uamuzi wa kuoa au kuolewa unamtaka
mtu aingie katika ndoa asilimia mia moja. Ikiwa hautakuwa tayari kuingia
kwenye ndoa kwa asilimia mia moja, tafadhali usiamue kuoa au kuolewa.
Utampotezea tu mwenzako muda maana hakuna ndoa isio na matatizo. Lakini
pia hakuna tatizo ambalo Mungu hawezi kulitatua. Lakini, je, uko tayari
kushirikiana na Mungu katika ndoa kwa kiwango cha asilimia ngapi?.![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNN390pj2eNKy2IuxuMwoNW0AzzT_HlDaUtM5MULKIkauvNhBm9CsJ4OklyIKfQA9deTfrOmxQ8Md_TF5sXoJIIcVgvefu9cQJRtqyuZzN1uzM8gGKHxR0Yf4R6Wnjm9m4w4V5-g53hMKe/s640-rw/ndoa1.jpg)
- Get link
- X
- Other Apps
Comments