NA BARAKA HIZI ZOTE ZITAKUJIRIA NA KUKUPATA USIKIAPO SAUTI YA BWANA,MUNGU WAKO.(Kumb. 28 : 2 ) * Sehemu ya pili *
Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps

Haleluya…
Bwana Yesu asifiwe…
Karibu mpendwa katika sehemu ya pili ya somo hili zuri. Dhumuni la somo
hili ni kukujenga kiimani kwa kufahamu kuwa BARAKA HAZIOMBWI,maana
maandiko matakatifu yako wazi kabisa yakituambia “ na baraka hizi zote
zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. ” Kumb.28 :
2
Labda tujiulize kuwa Baraka ni nini ?
• Baraka ni kutii sauti ya BWANA MUNGU na kuyafanya maagizo yote akuagizayo.
Tunasoma
Kumbukumbu la torati 30 : 8
“ Nawe utarudi, uitii sauti ya Bwana, na kuyafanya maagizo yake yote
nikuagizayo leo. ” 8 (And you will again give ear to the voice of the
Lord, and do all his orders which I have given you today. )
Kwa lugha nyingine ni kwamba, ili uwe na BARAKA maishani mwako ,Basi yakupasa kwanza UTII sauti ya Bwana Mungu wako kwa bidii.
Kama ukiendelea kusoma katika andiko hilo ( la kumb. 30 : 8) utaona
baada ya kutii sauti ya Bwana Mungu ,ndipo BARAKA zinakujilia pasipo
kuomba.
Tunasoma Kumb. 30 :9
“ Na Bwana, Mungu wako,
atakufanya uwe na wingi wa uheri katika kazi yote ya mkono wako, katika
uzao wa tumbo lako, na katika uzao wa ng'ombe wako, na katika uzao wa
nchi yako; kwa kuwa Bwana atafurahi tena juu yako kwa wema, kama
alivyofurahi juu ya baba zako; ”
Okey,
Baraka kwa lugha ya
kiingereza ni Blessing na neno BLESSING asili yake ni neno la kiyahudi
( Hebrew word ) ambalo ni “BARAK ” lenye maana ya kuachilia nguvu
iliyokuwepo ndani kwa Yule anayebariki ( To give permission for ability
to be released ) Ndio maana ukisoma katika kitabu cha Mwanzo 1: 28.
Biblia takatifu inasema :
“MUNGU AKAWABARIKIA, Mungu
akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale
samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai
kiendacho juu ya nchi. ”
( AND GOD BLESSED THEM, and God said
unto them, Be fruitful, and multiply, and replenish the earth, and
subdue it: and have dominion over the fish of the sea, and over the fowl
of the air, and over every living thing that moveth upon the earth.
{moveth: Heb. creepeth}From KJV ) Gen 1 : 28
BWANA MUNGU
anapoachilia Baraka kwa watu wake,maana yake anaachilia utawala/mamlaka
ambapo mamlaka katika eneo hili huwakilisha nguvu itokayo ndani yake ya
kumiliki/Kutawala.
Hivyo ni lazima maelezo ya Baraka yafuate,mahali ambapo Bwana Mungu hubariki Mfano :
Tumeona hapo katika kitabu cha Mwanzo 1 : 28. MUNGU AKAWABARIKIA, Mungu akawaambia,…
Baada ya kuwabarikia Adam na Hawa tunaona akitoa maelezo juu ya BARAKA hiyo.
Hivyo ndani ya Baraka imo nguvu ya pekee inayotoka kwa Yule
anayebariki. Ukimbariki mtu inamaana kuwa ,kuna nguvu itokayo kwako
inayoambatana na kile unachokibariki.
Sikia ;
BARAKA hupatikana katika kuliishi neno la Mungu.
Hivyo basi unapowaona watu wa mataifa wakimiliki vitu vya thamani kubwa haimaanishi kuwa wamebarikiwa la hasha!
Maana upatiakanaji wa vitu hivyo havikutokana na neno la Mungu,hiyo
sio BARAKA bali ni Neema na Rehema za Mungu alizoachilia kwao kwamba
akiwasubili siku moja watubu kisha ndipo wapokee BARAKA ya kweli iliyomo
ndani ya Yesu Kristo.Tazama maandiko yatuambiavyo hapa :
“
Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka
zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;” Waefeso 1
: 3
Baraka hutoka kwa BWANA MUNGU nazo huanzia rohoni katika
ulimwengu wa roho, ndani ya Kristo. Hii inamaanisha kuwa mtu wa mataifa
hana Baraka,maana Baraka zimo ndani ya Yesu Kristo na ndio maana ni
muhimu sana kumpokea Bwana Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako ili
urithi Baraka za za kweli.
Labda tuangalie wale waliobarikiwa :
01.IBRAHIMU
Tukimtizama Ibrahimu anatupa mfano mzuri wa mtu aliyebarikiwa.Kamwe
hutaona Ibrahimu akiomba BARAKA kwa Bwana Mungu bali yeye aliishi maisha
ya Imani tu ,akilishika neno la Mungu na yote ambayo Bwana Mungu
amuagizayo na Baraka za Mungu zikamfuata pale alipo.
ITAENDELEA…
UBARIKIWE.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments