Katika matukio yaliyotokea pale kawe pentecostal
church(KPC) karibu na lugalo jeshini jumapili iliyopita ilikua ni pamoja
na muujiza wa MUNGU kwa mtumishi wa MUNGU Paulo Kusayo ambaye ni mzee
wa kanisa kiongozi na mkewe Ester Kusayo baada ya MUNGU kuwabariki
mtoto wa kike baada ya miaka mingi kupita maana ndoa yao yenye mika 12
walijaaliwa kupata mtoto 1 tu na kwa mika 10 hawakupata mtoto lakini
muujiza wa MUNGU ulipotokea wamefanikiwa kupata mtoto tena. ni jambo la
kumshukuru MUNGU sana na hawakuficha furaha yao maana walisema mbele ya
kanisa kuwa huo ni muujiza mkuu sana kwao kwani hawakudhani kama
wangefanikiwa kupata mtoto tena maana kwa mika 10 walitaka mtoto lakini
haikutokea na kwa kumwamini MUNGU walijua tu kuwa wakati wa BWANA
ukifika watafanikiwa na MUNGU alikua amekwisha sema tayari na mtumishi
Paulo lakini imechukua miaka mingi kutokea. |
Comments