WAPATA MTOTO BAADA YA MIAKA 10 BILA KUPATA MTOTO KATIKA NDOA YAO

Katika matukio yaliyotokea pale kawe pentecostal church(KPC) karibu na lugalo jeshini jumapili iliyopita ilikua ni pamoja na muujiza wa MUNGU kwa mtumishi wa MUNGU Paulo Kusayo ambaye ni mzee wa kanisa kiongozi  na mkewe Ester Kusayo baada ya MUNGU kuwabariki mtoto wa kike baada ya miaka mingi kupita maana ndoa yao yenye mika 12 walijaaliwa kupata mtoto 1 tu na kwa mika 10 hawakupata mtoto lakini muujiza wa MUNGU ulipotokea wamefanikiwa kupata mtoto tena. ni jambo la kumshukuru MUNGU sana na hawakuficha furaha yao maana walisema mbele ya kanisa kuwa huo ni muujiza mkuu sana kwao kwani hawakudhani kama wangefanikiwa kupata mtoto tena maana kwa mika 10 walitaka mtoto lakini haikutokea na kwa kumwamini MUNGU walijua tu kuwa wakati wa BWANA ukifika watafanikiwa na MUNGU alikua amekwisha sema tayari na mtumishi Paulo lakini imechukua miaka mingi kutokea.
MCHUNGAJI KIONGOZI WA KAWE PENTECOSTAL  CHURCH(KPC) ELLY BRIGHTON BOTO AKIWAOMBEA AKIWA AMEMBEBA MTOTO NA KUWAOMBEA WAZAZI PAMOJA NA MTOTO WAO

MCHUNGAJI AKIELEZEA JAMBO WAKATI WA IBADA





MR& MRS PAULO KUSAYO WAKIWA KANISANI WAKIMSHUKURU MUNGU KWA BARAKA YA MTOTO BAADA YA MIAKA 10


WAUMINI WAKIWAPONGEZA PAULO NA MKEWE


ILIKUA NI FURAHA YA AJABU


ILIKUA NI UTUKUFU WA MUNGU NA FURAHA KUU




PAULO AKIMSHUKURU MUNGU NA PEMBENI NI MKE WAKE

Comments