Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
by Vicent Mwengo |
BWANA YESU APEWE SIFA,
Habari yako ndugu popote hapo ulipo, najisikia kukuandikia jambo hili
leo hussani wewe mdada/binti, sikufundishi ila ninachukua wasaa huu
kukukumbusha tu jambo dogo sana linalohusiana na ngono.
Ngono
ni neno moja zito ambalo linamaanisha ufanyaji wa tendo la ndoa katika
utaratibu usio sahihi katika jamii. Nianze hivi kwenye jamii yoyote
jambo lolote huwa lina utaratibu, kama jamii Fulani imezoelea jambo
Fulani na kulikubali basi jambo hilo hufanywa kuwa sehemu ya utamaduni
wa jamii hiyo. Kwa mfano; kama jamii Fulani wameukubali utumiaji wa
bangi na wote kwa pamoja wameuukubali, basi jamii hiyo itakapoambiwa
kutumia bangi ni mnafanya makosa hawawezi kukubali kwani limekubalika
kwenye jamii yote na mtazamo wao uko sahihi.
Tendo la ndoa
katika jamii yoyote lina utaratibu wake, wazee wetu walienenda katika
misingi ya jamii yao ilivyokuwa, wengi mmesimuliwa habari za wazee na
wazee wenu hivyo watu mnazijua vilivyo, sitaki kuzizungumzia sana.
Unapozungumzia ngono, mimi ninalizungumzia jambo hili kwa mtazamo wa
“kibiblia”. Kwa dhana ya utaratibu, hata kwenye Biblia kuna utaratibu
wake, lakini utaratibu wa kwenye Biblia hauna tofauti sana na wa jamii
za wazee wetu, kwani wazee wetu walifanya japo Biblia kwao ilikuwa bado
haijakolea. Lakini pia hata walipoijua walienenda sawasawa kwa kuacha
kuwa na wake wengi. Kuyaleta yote haya ni kutaka tu kukuongezea uwanja
wa kulitathmini jambo hili.
Kwa mtazamo wa kibiblia ngono iko
katika sehemu mbili ambazo ni uasherati (kufanya tendo la kabla ya ndoa)
na uzinzi (kufanya tendo la ndoa nje ya ndoa). Naogopa kuzungumzia
habari za ndoa kwani uhalisia wangu haufundishi habari za ndoa (sijaoa).
Nitajikita kwenye ngono kwa maana ya Uasherati kama nilivyotolea
maelezo hapo juu.
NB: Je wewe mwanadada unatambua kwamba unauwezo wa kuzuia mfumuko wa ngono kwenye jamii???
Ni swali moja rahisi lenye majibu yenye utata, lakini lina suluhu ndani
ya jamii nzima. Nilipowuliza wanadada mahala Fulani swali hili; mmoja
alikuja juu kwelikweli, na kusema “waambie kwanza wanaume waache
kutufuata”. Mwingine akasema Mwengo, ninyi wanaume ndio chanzo cha
tatizo la ngono kwenye jamii kwa sababu mnapenda kweli! Mwingine kwa
sauti ya upole, Vicent siku zote kwenye mapenzi mwanaume ni kama jiko la
mchina na sisi ni kama jiko la mkaa hivyo ninyi wanaume ndio chanzo cha
tatizo. Wengine walikuwa wasikilizaji tu wa mazungumzo, kwani tulikuwa
tumemaliza kazi yetu na tumechoka nikaamua kuzua mjadala wa
kutupumzisha. Achana na hayo lakini leo ninakuandikia wewe mdada ili
ujue na kama ulijisahau basi uzingatie upya. Ndugu wale waliotoa majibu
yao, yamkini hata wewe unapokuwa unalitathmini jambo hili na wewe pia
unamajibu kama yao, yanaweza yasiwe kama yao lakini yanafanana na hayo.
Lakini sasa hebu pata mtazamo uliosahihi juu ya habari hizo.
Kwenye fikra yoyote ile huwa kuna vitu viwili, pata hiyo; “fikra inaweza
ikawa sahihi lakini ikawa na mtazamo usio sahihi vivyo hivyo inaweza
ikawepo fikra sahihi na mtazamo wake ukawa sahihi vilevile”. Lakini
nilichogundua majibu mengi walionayo wanadada ni sahihi lakini mtazamo
wake sio sahihi. Kwa kukufikirisha habari za mtazamo naomba uniambie;
kitendo cha mwaume kukufuata na kukutongoza ndio sababu ya wewe kufanya ngono?
Shaka yangu (suspicious reasons); moja kati ya majibu haya ni sababu ya
wewe mdada kujihusisha na ngono, ukiachia mbali na kubakwa kwa nguvu.
1.Kutaka, kupenda au kukubaliana wewe mwenyewe
2.Kushawishika kwa sababu wenzio wanafanya
3.Kushawishika na mahitaji (fedha nk.)
4.Tama; ila hii ni sawa na ya kwanza.
Hizo ni sababu shaka zangu, zinaweza zikawepo na zingine ukitaka
utatuandikia. Katika sababu nilizozitaja, nyingi zinahusisha ushawishi,
kama kweli unampenda Mungu kwa kuyafuata maagizo yake yaliyoandikwa
kwenye Biblia, hebu niambie kwa dhati yako; Je kwa sababu ya
kushawishiwa basi ndio sababu ya wewe kufanya ngono ???
NB: Mmhh! ni hatari sana usipokuwa na mtazamo sahihi juu ya mahusiano yako ya kimapenzi mdada.
KWANINI WADADA NDIO MZUIE NGONO KWENYE JAMII.
Ninawazungumzia wadada kwa lugha ya kistaarabu sana nikiwaita mabinti,
kwani ndio chumvi ya mapenzi. Unajua kabisa kuwa Mungu alimleta mwanamke
ili kukamilisha ubinadamu wa mwanaume, lakini wote ni kitu kimoja. Bila
mwanamke mwanaume hajakamilika. Nikufikirishe maswali haya tena;
Kwa mabinti, Je ulishawahi kufuatwa na mwanaume ukakataa, alifanya ngono na wewe?
Kwa wanaume wanaosoma ujumbe huu; ulipomfuata mwanamke akakukatalia, je ulifanya nae ngono?
Swali langu la pili linafanana na la kwanza lakini yote kwa pamoja jibu
lake ni haikufanyika ngono. Lakini kwa binti mpumbavu jibu lake ni
hili, kumkatalia huyu na kumkubalia mwingine na kwenda kufanya nae
ngono. Mwanaume alipokataliwa aliondoka zake na kwenda kujaribu kwa
wengine, waliokuwa wapumbavu walimkubalia na kuungana nae kuifanya
ngono. Mwanaume anafanya ngono kwa sababu anapata ridhaa yako. Kuwa
makini na elewa sawasawa hakuna sababu kwa Mungu, eti mimi nilifanya
ngono kwa sababu nilishawishiwa. uliona wapi kwenye Biblia ikasema
usifanye ngono! ila tu ukishawishiwa! (kukaa karibu na mahakama sio
sababu ya kujua sheria) kwa mwanaume yeyote hisia kali zipo kwa mwanaume
aliye kamilika. Lakini je si ingekuwa heri kama angekosa binti wa
kufanya nae ngono, Mabinti nao wakataka mahusiano kwa hekima za kimungu?
Sasa mabinti wote ninaamini mmenielewa ninaposema mna uwezo wa kuzuia
mfumko wa ngono kwenye jamii! Pia ninapozungumzia habari hizi moyo wako
unaweza kujibizana na maandishi haya kwamba sasa mbona mimi ninaye mmoja
tu nab ado hatujafanya tendo la ndoa, la-hasha! mimi sizungumzii idadi
ya wapenzi; uwe naye, uwe nao au usiwe naye mimi sijali. Habari hizi
mimi nazungumzia kuhusu ngono tu.
NB: Wako wapumbavu wengine wanaowaza mioyoni mwao, hakuna wewe… mbona ninafanya na maisha yanaendelea!!!
Ninapotumia neno upumbavu simtukani mtu, kasome kwenye Biblia limetumika kwa maana ileile ninayoimaanisha mimi.
Hapa naomba nianze kwa kukupa mfano wa kimanunuzi tu usihofu utaelewa
tu; Huwa ikiitishwa tenda yoyote mwisho wa siku huchaguliwa mshindi.
Hukabidhiwa tenda na kazi kuanza (hii ni kwa ufupi). Fikiria kama wewe
ndio mtoa tenda (serikali), inafika wakati wa kukabidhi tenda unakuta
kazi imefanyika kwa kutokukamilika, ukiuliza kwa nini unaambiwa fedha
imekwisha! na wewe ulitoa fedha kamili. Au wewe unatoa fedha kamili
kumpatia mwanao atumie kwa muda Fulani, bila kuwepo kwa mabadiliko ya
bei lakini kabla ya muda huo kufika anakwambia imeisha kwa sababu zisizo
na msingi. Je itakuwaje? Namaanisha nini kuuleta mfano huu; Mungu
alikupatia mwili na moyo wenye hisia za kimapenzi, Mungu kama mtoaji,
wewe kama mpokeaji, je unauendeshaje mwili wako. Inaposemwa usifanye
uasherati alimaanisha ukifanya utapata dhambi! na sio utapata magonjwa
(maana wengine wanadanganyana kutumia kondom nk.). Ingekuwa heri kama
kila binti angeijua kweli ya mapenzi. Lakini angalia sasa mapenzi,
yamefanywa fani yaani ndio ujanja na ukisasa leo. Angalia sasa watoto
wadogo walivyoichosha miili yao kwa ngono, inasikitisha sana.
Unapojisemea moyoni mwako mbona maisha yanaendelea...unajua dhana hiyo
imesababisha mtafaruku kwenye jamii kiasi gani.
1.Nusu ndoa;
mwanaume akishakuzalisha ukifika wasaa wa kuoa anagundua mwili wako
umechoka anaahirisha na kukuacha.(inawaumiza sana kisaikolojia)
2.Kutokuolewa, hii ni kwa baadhi kutokuolewa kabisa kwa sababu ya miili yao kuchoka sana na ngono.
3.Kukosa watoto (ugumba); hii ni kwa sababu ya kutoa mimba nyingi ili uonekane hujazaa.
4.Mfumuko wa watoto wa mitaani; hii ni kwa sababu ya kukosa malezi ya baba na mama, mtoto anahitaji malezi ya baba na mama!
Niliyoyasema yanatosha kukukumbusha habari za ngono, nimalizie kwa
kusema hivi, kama hujaanza ngono na umeyasoma maandishi haya basi ongeza
ujasiri wako kuikataa kabisa ngono, kama umejihusisha nayo na umeyasoma
maandishi haya sasa nakushauri kwa moyo wa huruma kwamba acha kabisa,
mgeukie Mungu akupatie hekima ya kuyakabili mapenzi kwa jinsi ya maagizo
yake. Umefanya ngono ndio! Hilo sio kosa kosa ni kukaidi kuacha. lakini
pia tambua kosa lako linasameheka hivyo mtafute mchungaji wako mweleze
habari zako ili akusaidie kwa kuomba sara ya toba.
Utukufu wa
maandishi haya apewe aliyeniwezesha. Haleluya!!! kwa kadri roho
alivyoniongoza kuyaandika maandishi haya juu ya wadada kuzuia mfumko wa
ngono kwenye jamii, ninaamini umejifunza kitu, Mungu akusaidie
kukifanyia kazi na mwenendo wa mahusiano yako yampendeze Mungu na si
kuwapendeza marafiki au ndugu zako. Lakini mwenye nafasi kubwa ya kuacha
ni wewe mwenyewe ndio maana Biblia inasema “acha” haisemi Mungu
akuachishe, hii ni kwamba jukumu la kuacha umepewa wewe na mimi. Basi na
mioyo yenu iimbe; “Ni Yesu huyo ni Yesu huyo!!” maana ndiye
anayeniwezesha. Sifa na utukufu apewe yeye.
ASANTENI WOTE;
NDUGU YAKO KATIKA KRISTO;
MWENGO V.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments