Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Mwl Sospeter Simon S. Ndabagoye
|

Kuna majibu mengi juu ya dhana ya Kitabu hiki, kiitwacho Biblia. Moja wapo ya majibu haya ni pamoja na
-Biblia ni kitabu cha Kikristo, yaani kinawaongoza wakristo. Licha ya
kuwa ni kitabu cha zamani sana, ila ni kitabu cha adhimu na muhimu sana.
Thamani ya Biblia ni zaidi ya pesa, dhahabu au mali yoyote uipendayo.
-Kitabu hiki, kina uvuvio wa Mungu moja kwa moja kwa kuwa, maneno
yaliyoandikwa huko, ni pumzi ya Mungu kamili. Tofauti na vitabu vingine,
biblia ni kitabu kinachoishi na kinahuisha kwa kuwa kina pumzi ya uhai.
Ushahidi wa Kibiblia, unaweza kufasili kuwa Biblia inaelezwa katika namna tatu ambazo ni:-
(a) BIBLIA – Ni “Maandiko matakatifu ya Mungu” uKifungua

Biblia
Ukurasa wa kwanza kabisa, utakutana na maandishi yanayosema” Maandiko
matakatifu ya Mungu yaitwayo BIBLIA yaani Agano la Kale na Agano Jipya”.
Pia Ukisoma (2Timotheo 3:15)... na ya kuwa tangu utoto umeyajua
maandiko matakatifu,amabayo yanaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa
imani iliyo katika Kristo Yesu.
(b) BIBLIA- Ni “Neno la Mungu lenye
uzima, Hudumu hata milele” (Yohana 1:1&3)”

Hapo mwanzo kulikuwepo
Neno,naye Neno alikuwepo kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Vyote
vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote
kilichofanyika. (Ufunuo 6:9)”...nikaona chini ya madhabahu, roho zao
waliochinjwa kwaajili ya NENO la Mungu....”
(c) BIBLIA- Ni “Neno
lenye pumzi ya Mungu, na lipo kwaajili ya mwanadamu”

(2Timotheo
3:16&17) “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho,na
kwa kuwaonya, watu makosa yao, na kwa kuwaongoza na kwa kuwaadibisha
katika haki ili mtu wa Mungu awe kamili....”
Ni dhajiri kuwa,
Biblia, ni kitabu kitakatifu, chenyekusheheni Busara na Hekima ya Mungu.
Ni neno linaloishi, lenye nguvu, uweza,na linafaa kwa mafundisho.
Linamwongoza mwanadamu katika njia ya kweli, huku akimwelekea Mungu.
Ukiiamini Biblia, unapata uwezo na mamlaka juu ya vitu vyote, na
ukiomba lolote kwa kulitumia neno la Mungu, utafanyiwa, kwa maana Neno
la Mungu, ndiye Yesu mwenyewe.(Ufunuo 19:13).
“Mkiniomba neno lolote kwa jina langu nitalifanya(Yohana 17:14).
Swali la Kujiuliza, Kama Biblia ni neno la Mungu, na pia ni pumzi ya Mungu, ilandikwa na nani na iliwezekana vipi?
Biblia iko wazi juu ya hilo kuwa, pamoja na hayo yote, Biblia
iliandikwa na wanadamu, tena tofauti tofauti. Pengine hata utamaduni wao
ulikuwa tofauti, sijui, ila ni dhahiri kuwa, hapakuwa na upendeleo juu
ya ukoo fulani, pengine wa Kifalme au la, juu ya uandishi wa Biblia.
Maandiko matakatifu yanasema” Biblia ni maandiko yaliyo andikwa na
watu tofautiwalioongozwa na Roho Mtakatifu, Yaani Manabii. (Yohana
17:17). Biblia siyo hadithi za kutungwa kama vilivyo vitabu vingine,
siyo katiba ya nchi wala haijaandikwa kiujanja ujanja tuu, (2Petro
1:16-21) “Maana hatukufuata hadithi ziizotungwa kwa
werevu.Tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja
kwake, bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake.......18Na sauti hiyo
sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa naye.......20mkijua neno
hili kwanza kuwa hakuna unabii katika unabii upatao kufasiliwa kama
apendavyo mtu fulani tu. 21Maana unabii haukuletwa popote kwa kwa
mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu,
wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Watu hawa awaliongozwa na Roho wa Mungu
katika kuyaandika maneno haya ya Mungu. Pia Malaika walikuwapo ili
kuwaelekeza namna ya kuandika (Ufunuo 1-3:22, Soma tafadhari).
Lengo la Biblia ni nini?

Ukweli ni kuwa, Mungu aliwekeBiblia kwa lengo kuu moja, ambalo ndilo
mahususi na maalum kabisa, kuwa ni UKOMBOZI wa mwanadamu(Mwanzo 3:15).
Pamoja na kuandikwa na watu tofauti tofauti, wenye elimu na utamaduni
tofauti na mazingira tofauti, ila wote, walielekezwa katika kumkomboa
mwanadamu kwa kumuonya, kumwelekeza na kumwongoza katika njia iliyo ya
kweli ambayo ni Yesu Kristo.
Mungu akubariki na kukuinua, akufunulie zaidi na zaidi umjue sana na kumpenda, Katika Jina la Yesu Kristo nimeomba.
Mwl Sospeter Simon S. Ndabagoye
New Elshaddai Ministries NEM-Tanzania.

Kuna majibu mengi juu ya dhana ya Kitabu hiki, kiitwacho Biblia. Moja wapo ya majibu haya ni pamoja na
-Biblia ni kitabu cha Kikristo, yaani kinawaongoza wakristo. Licha ya kuwa ni kitabu cha zamani sana, ila ni kitabu cha adhimu na muhimu sana. Thamani ya Biblia ni zaidi ya pesa, dhahabu au mali yoyote uipendayo.
-Kitabu hiki, kina uvuvio wa Mungu moja kwa moja kwa kuwa, maneno yaliyoandikwa huko, ni pumzi ya Mungu kamili. Tofauti na vitabu vingine, biblia ni kitabu kinachoishi na kinahuisha kwa kuwa kina pumzi ya uhai.
Ushahidi wa Kibiblia, unaweza kufasili kuwa Biblia inaelezwa katika namna tatu ambazo ni:-
(a) BIBLIA – Ni “Maandiko matakatifu ya Mungu” uKifungua

(b) BIBLIA- Ni “Neno la Mungu lenye uzima, Hudumu hata milele” (Yohana 1:1&3)”
(c) BIBLIA- Ni “Neno lenye pumzi ya Mungu, na lipo kwaajili ya mwanadamu”
Ni dhajiri kuwa, Biblia, ni kitabu kitakatifu, chenyekusheheni Busara na Hekima ya Mungu. Ni neno linaloishi, lenye nguvu, uweza,na linafaa kwa mafundisho. Linamwongoza mwanadamu katika njia ya kweli, huku akimwelekea Mungu.
Ukiiamini Biblia, unapata uwezo na mamlaka juu ya vitu vyote, na ukiomba lolote kwa kulitumia neno la Mungu, utafanyiwa, kwa maana Neno la Mungu, ndiye Yesu mwenyewe.(Ufunuo 19:13).
“Mkiniomba neno lolote kwa jina langu nitalifanya(Yohana 17:14).
Swali la Kujiuliza, Kama Biblia ni neno la Mungu, na pia ni pumzi ya Mungu, ilandikwa na nani na iliwezekana vipi?
Biblia iko wazi juu ya hilo kuwa, pamoja na hayo yote, Biblia iliandikwa na wanadamu, tena tofauti tofauti. Pengine hata utamaduni wao ulikuwa tofauti, sijui, ila ni dhahiri kuwa, hapakuwa na upendeleo juu ya ukoo fulani, pengine wa Kifalme au la, juu ya uandishi wa Biblia.
Maandiko matakatifu yanasema” Biblia ni maandiko yaliyo andikwa na watu tofautiwalioongozwa na Roho Mtakatifu, Yaani Manabii. (Yohana 17:17). Biblia siyo hadithi za kutungwa kama vilivyo vitabu vingine, siyo katiba ya nchi wala haijaandikwa kiujanja ujanja tuu, (2Petro 1:16-21) “Maana hatukufuata hadithi ziizotungwa kwa werevu.Tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake, bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake.......18Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa naye.......20mkijua neno hili kwanza kuwa hakuna unabii katika unabii upatao kufasiliwa kama apendavyo mtu fulani tu. 21Maana unabii haukuletwa popote kwa kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Watu hawa awaliongozwa na Roho wa Mungu katika kuyaandika maneno haya ya Mungu. Pia Malaika walikuwapo ili kuwaelekeza namna ya kuandika (Ufunuo 1-3:22, Soma tafadhari).
Lengo la Biblia ni nini?
Mungu akubariki na kukuinua, akufunulie zaidi na zaidi umjue sana na kumpenda, Katika Jina la Yesu Kristo nimeomba.
Mwl Sospeter Simon S. Ndabagoye
New Elshaddai Ministries NEM-Tanzania.
- Get link
- X
- Other Apps
Comments