Watu wengi hufikiri kwamba
tunda ambalo Adamu na Hawa
waliambiwa wasile katika
bustani ya Edeni lilimaanisha
uhusiano wa kingono.
Lakini
Biblia haifundishi hivyo.
Hebu fikiria hili: Hata kabla Hawa
hajaumbwa, Mungu alimwamuru
Adamu asile matunda ya “mti wa
ujuzi wa mema na
mabaya.” (Mwanzo 2:15-18) Amri
hiyo haikumaanisha uhusiano wa
kingono kwa sababu Adamu
alikuwa peke yake. Zaidi ya hayo,
Mungu aliwapa Adamu na Hawa
amri hii iliyo wazi: “Zaeni, muwe
wengi, mjaze dunia.”
(Mwanzo 1:28).
Je, Mungu mwenye upendo
angewapa wenzi hao wa ndoa
agizo la ‘kujaza dunia’ – jambo
ambalo bila shaka, lingehusisha
uhusiano wa kingono – kisha
awahukumu kifo kwa kutii
maagizo yake? – 1 Yohana 4:8.
Kwa kuongezea, Adamu
hakuwepo Hawa ‘alipoanza
kuchukua na kula kati ya
matunda aliyokatazwa. Baadaye
alimpa mume wake pia
alipokuwa pamoja naye, naye
akaanza kula.’ Mwanzo 3:6.
Mwishowe, Mungu
hakuwahukumu Adamu na Hawa
walipofanya ngono na kuzaa
watoto. (Mwanzo 4:1,2)
Kwa
hiyo ni wazi kwamba tunda
ambalo Adamu na Hawa walikula
halikumaanisha tendo la kufanya
ngono bali lilikuwa tunda halisi
lililokuwa mtini.
Comments