KONGAMANO KUBWA LA INJILI KWA SIKU SABA JIJINI MWANZA



Kongamano kubwa la injili  litafanyika jijini Mwanza kuanzia jumapili hii tarehe 9 june hadi tarehe 17 june mwaka huu 2013, Ni siku saba za maajabu na kutakuwa na watumishi wa MUNGU kadhaa  watakaohudumu wakiwepo  Bishop Nderitu, Pastor Ken Kamau na mwenyeji wao Mchungaji Dr Daniel Moses Kulola. Tamasha hilo litafanyika katika ukumbi  wa kanisa la EAGT Lumala mpya ambalo lipo nyuma ya soko jipya la sababa wilaya ya Ilemela jini Mwanza, Muda wa kuanza kila siku ni saa 7:30 mchana  kwa siku zote 7 kuanzia tarehe 9-17 june 2013. Masomo yatakayofundishwa ni NENO LA MUNGU, AFYA na SAIKOLOJIA pamoja na Maombezi ya wagojwa wote na wenye mahitaji mbalimbali, na katika tamasha hilo kwaya 20 kutoka Tanzania na waimbaji maarufu kutoka Kenya, UNAKARIBISHWA SANA NDUGU ULIYE MWANZA NA MIKOA YA JIRANI.
MCHUNGAJI DANIEL KULOLA

Comments