Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Pastor Donis and Nnunu Nkone |
Kuolewa na mwanaume ambaye anategemewa kwao na ndiye mtoto kipenzi cha
mama, inahitaji mwanamke mvumilivu na aliyeokoka kweli kweli. Mwanaume
ambaye ni kipenzi kwa mama yake na anayempenda saaana sana mama yake,
lazima aombe sana busara kwa Mungu ili ajue namna ya kuiongoza ndoa
yake, kumlinda na kumsikiliza mkewe. Mwanamke anayeolewa mwanaume wa
hivi, anahitaji kuombewa sana ili aweze kuvumilia mpaka hapo mambo
yatakapokuwa yametulia. Kama wewe msomaji ujumbe huu unakuhusu, Mungu
akutie nguvu na kukuongezea hekima huku akikuponya na machungu. Kama
ndoa ni changa, basi mume wa namna hii ajitahidi kuishi nyumba ambayo ni
mbali na wazazi. Wewe mume usithubutu kumsahau mama yako, na wewe mke
usithubutu kumfanya
mume wako asimjali mama. Mtapata laana mbaya. Ombeni
uvumilivu kwa Mungu na yeye Mungu atawasaidia.
Pata Kitabu chetu ili ujifunze namna ya kuishi na ndugu wa ukweni kwako.
By Pastor Donis and Nnunu Nkone
- Get link
- X
- Other Apps
Comments