Posted by
Peter Mabula
- Get link
- X
- Other Apps
![]() |
Sospeter Simon S. Ndabagoye |

Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari
kushirikiana na wengine, hasa waliowanyonge....(Warumi 12:16).Msiwe na
majivuno wala kiburi! Nyenyekeeni, pendaneni, fanyeni kazi ya Mungu kwa
umoja, Mungu anaupenda umoja, hata Yesu na Mungu ni umoja. Kuna siri
katika umoja.
Ombeaneni, na saidianeni, kila mtu, amwone
mwenzie kuwa bora zaidi, mwenzio akipungukiwa hekima au maarifa, mwombee
na umrejeshe kundini kwa upole na upendo, Usikubali hata mmoja apotee
machoni pako. Iweni wenye nia ya Kristo ndani yenu.
Jengo la Kanisa lako, au gari la huduma yako, visikutenge na wapendwa
wengine, wala, usijivune kwakuwa, umepata elimu kubwa ya Dini au ya
dunia, Mwinue Yesu aliyekupandisha, huku ukimwombea mwenzio.
Usikubali kwakuwa umepata kazi nzuri, mke mzuri au mme, ukawaona wengine
hawafai, Mshukuru Mungu aliyekufikisha hapo, huku ukimwombea rafiki
yako na wote ambao hawajapata.....
Ukiona ndoa yako imetulia,
hakuna ugomvi, umekula, umekuywa na kulala vizuri, pengne watoto
wanaenda shule bila matatizo, hata kama yapo ni ya kawaida, ombea na
mwenzio afike hali hiyo.
Bebeaneni mizigo.Je, haufahamu kuwa
sote tu viungo katika mwili wa Kristo, na Yesu ndiye Bwana wetu sote?
Je, mguu ukiuma, mkono hauukuni, na pengine njaa ikiuma, mkono hauweki
chakula mdomoni ili meno yakisage, hatimaye koo hukipitisha ili kulijaza
tumbo hilo liache kuuma? Kama mdomo ungeliche tumbo,ingekuwaje njaa
ikiliuma tumbo? Na endapo, miguu ingeacha kukimbia, Simba akikuvamia
ingekuwaje, si kichwa na tumbo vingeraruliwa? Tupendaneni jamani,
tuifanye kazi ya Mungu kwa umoja. Kila mtu anakitu maalumu Mungu kampa,
ambacho mwingine hana, hakuna ambaye Mungu hakumpa kipawa flani.
Ndugu yangu, leo Mungu anasema na wewe juu ya upendo, ushirikiano na
umoja. Jitafakari mwenyewe, jipime ulivyokaa na majirani zako, ulivyokaa
na mwenza wako wa ndoa, Jipie mwenyewe, kisha "Itii sauti hii", chukua
hatua mara moja "tembea na kanisa lako, tembea na mme wako, tembea na
mke wako", kila mara omba juu ya rafiki yako, ombea watoto wako, omba
juu ya watumishi wengine, sheria za kidunia na mifumo ya kututenganisha
wana wa Mungu usivikubali. Tembea na maono ya watu wote kumjua KRISTO,
wakiri dhambi, wabatizwe kisha waokoke, wapate kuurithi ufalme wa Mungu
aliotuandalia wateule wake. Haleluya!
Kheri asomaye na Kuelewa Ujumbe huu, maana akiutendea kazi, atapata Baraka. BY
Sospeter Simon S. Ndabagoye
- Get link
- X
- Other Apps
Comments