TAFUTA MWENZI WA MAISHA

 na mwl Paschal Kizwalo
AMANI YA BWANA WETU YESU KRISTO IKAE KWENU WAPENDWA, NI HAJA YANGU KUWA MUNGU AENDELEE KUMUONEKANIA KILA MMOJA WETU KATIKA KILA ENEO LA MAISHA YETU, KUMBUKA WEWE KIJANA MWENZANGU SAFARI YA KUANZISHA FAMILIA SIO KAMA KUTUNGA WIMBO, MUNGU AKUPE UELEWA KATIKA SEHEMU HII FUPI YA SOMO LETU.



Wakati utafika wa kuchagua mwenzi wako wa maisha.
- Chagua vizuri kwa uangalifu
- Siyo muhimu kila wakati kuwa unaangalia mtu anayefaa, bali ni wewe kuwa mtu muhimu na Afaaye, kuigwa mfano wa mtu unayemtafuta.

- Mtu ambaye: -
$ Amekuwa kiroho
$ Ana tabia njema
$ Anajua kutunza na kutumia fedha kwa uangalifu
$ Yuko safi kimahusiano ya kimapenzi (sexually pure)
$ Kimahusiano hampo mbali na utamaduni wako bila kwenda kinyume na kanuni za kibiblia.
$ Anaonyesha heshima kwako na kwa wengine.
$ Kijana ataheshimu wazazi wa mpenzi wake, kama mwenzi wako ni yatima tafuta mzee mkristo safi mwenye heshima ndanii ya jamii awe badala ya mzazi wako ambaye ataweza kutatua matatizo yenu.
$ Hatachukulia mwenzake kama girlfriend bali mwenzi wake wa maisha.
$ Shughuli zote mnafanya pamoja ikiwa ni pamoja na za kifamilia, ndani ya jamii, mambo ya kiroho, vichekesho (share fun)

Muda wote mtakaoshirikiana mtafahamiana vizuri tabia, mienendo. Kila mmoja atamthamini mwenzake.
KUMBUKA NI AHERI UKAKOSEA KUCHAGUA VIATU WAWEZA KUMRUDISHIA MUUZAJI ILA MKE/MME UTAUBEBA MSALABA MPAKA SIKU YA KIFO CHAKO.
KUMBUKA UFALME WA MUNGU NA KUMCHA MUNGU KWANZA MME/MKE BWANA ATAKUPA.
Missionary Field In Tanzania - MFT.

Comments

Unknown said…
NAITWA ADAM NDUNGURU UMRI WANGU MIAKA 25 NAISHI MTWARA NATAFU MCHUMBA WAKUISHI NAE SICHAGUI DINI NA AWE NA VIGEZO VIFUATAVYO 1.AWE MWEUPE KIASI AU RANGI YA CHOCOLATE 2.AWE NA MAPENZI YA KWELI 3.AWE MWEMBAMBA KIASI 4.AWE MREFU KIASI SIO SANA 5.AWE TAYARI KUPIMA UKIMWI
NAMBA YANGU NI 0657607867