TAMANI SANA URAIA WA MBINGUNI.*sehemu ya pili*



MTUMISHI GASPER MADUMLA


Nakusalimu katika jina la Bwana nikikuambia,
Bwana Yesu asifiwe…
Haleluya….

Karibu tuendelee pale tulipokuwa tumeishia katika fundisho letu.
Tuliona mfano mmoja wapo wa Stefano mtu aliyejaa Roho mtakatifu,
mtu aliyejaa Neema na uwezo,mtu aliyejaa hekima,

jinsi alivyotamani sana kufanyika raia wa mbinguni maana mtu huyu aliuona utukufu wa Bwana Mungu pamoja na Bwana Yesu ameketi katika mkono wa kuume wa Mungu,angali akiwa bado anaishi kama mwanadamu wengine kabla ya kuuwawa. Tazama hata kifo cha Stephano,
Biblia inasema ;
“ wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja aliyeitwa Sauli.” Matendo 7 :58

Nguo za Stefano ziliwekwa miguuni mwa Sauli,
Hii ina maana kuwa utumishi aliokuwa nao Stefano uliwekwa miguuni mwa Sauli ikiwa ni ishara ya kuendeleza upako aliokuwa nao Stefano,

Maana nguo za Stefano zilikuwa sio kama nguo tu za kawaida,Bali zilikuwa ni Upako/Utumishi aliokabidhiwa Sauli ambaye baadae kidogo tunamuona anatokewa na Bwana Yesu njiani kisha hata jina lake linabadilika na kuwa mtumwa wa Kristo Yesu,aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa aihubiri injili ya Mungu.

• Maisha ya mkristo haswa ni maisha ya umilele baada ya maisha haya kupita.

-Mitume wa Bwana Yesu nao ni mfano mzuri wa watumishi waliokubali kupoteza maisha ya damu na nyama ili kupata uraia wa mbinguni
Karibu mitume wote waliuwawa kwa kuishindania Imani,
maana waliona maisha haya ya kawaida ni maisha yenye kuharibika tu,hivyo walitamani sana kuvikwa vazi la umilele.

Tazama mfano mmoja pale Herode aliponyoosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa Akamwua Yakobo, ndugu yake Yohana, kwa upanga.
Na akiona ya kuwa imewapendeza Wayahudi akaendelea akamshika na Petro.

Sasa tazama
Bibila inasema katika MATENDO 12:5
“ Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.”

Hawa watu wa kanisa walijawa na ujasiri wa namna yake usioelezeka.Kwa sababu sio rahisi kwa kukamatwa kwa mwenzao na kuuwawa kwa upanga,
kisha kukamatwa tena mwingine naye akipangiwa kuuwawa kwa upanga,Tena Kisha wao muda huo huo wakakutana wote na kuaanza kuomba ,

Hii inamaanisha kuwa hata wao waliona ni afadhali kuuwawa kwa ajili ya Kristo Yesu na kwa ajili ya injili,maana kilichomfanya Yakobo ndugu yake Yohana kuuwawa ni injili ya Bwana yesu,na kanisa hawakukoma kuomba mpaka Petro walipomuona kwa macho yao.

* Jambo moja tunalojifunza kupitia mitume wa Bwana Yesu ni kwamba walidhalau maisha haya yasiokuwa na maana kabisa na kutamani sana uraia wa mbinguni.

Mfano wa tatu.
Mtazame Paulo ambaye anasema kufa kwake ni faida.
Anasema
“ Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.” Wafilipi 1: 21

*Tamani sana uraia wa Mbinguni,ambapo kila kitu cha hapa duniani,yaani vile ambavyo havina utukufu kwa Bwana hivyo utaviona kama mavi,na ndivyo Paulo alivyoona
“ Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;”Wafilipi 3:8

• Hivyo basi utagundua kwamba wanafunzi wa Bwana Yesu Kristo,waliteswa na hata wengine waliuwawa wakiishindania IMANI maana walitamani sana kuishi pamoja na Mungu Baba Mbinguni.
Hawa wote waliona thamani ya maisha ya umilele katika utumishi wao waliokuwa wakiufanya.

• Ndio maana wakailinda IMANI waliyoipokea mara moja tu,kwamba wasiipoteze,wakaitetea na kuitunza IMANI waliyokuwa nayo mfano wa KITO CHA THAMANI.

Waliona maisha ya mbele,na wakatiwa nguvu kwa kile walichokiona,
Na ndio maana hata Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake mfano wa ufalme wa mbinguni akiufananisha na hazina iliyositirika.

Tunasoma Mathayo 13 :44
“ Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.”

Sikia ;
Bwana Yesu,Kitu anachowaambia wanafunzi wake katika andiko hili ni kwamba ufalme wa mbinguni ni “uraia wa
mbinguni”ambao unafanana na HAZINA iliyofichika.
Hazina ya mfano huo,haikufichwa na yeyote Yule bali ilifichika,Tuchukulie mfano mdogo wa maisha haya ya sasa hapa duniani.

Dhahabu na almasi ni moja wapo ya vito vya thamani ambavyo vimefichika katika ardhi.Upatikanaji wa Dhahabu ni wa shida sana.
Hivyo Yeye anayetaka hazina ya dhahabu inambidi aache vyote kwa ajili ya kuitafuta kwa moyo mmoja.

Nami nakuambia mtu akiipata dhahabu kamwe hawezi kuiweka hadharani ni lazima aifiche,Ndivyo ilivyo ufalme wa mbinguni haupatikani kwa urahisi yatupasa kuiilinda imani kama kito cha thamani…

ITAENDELEA…
UBARIKIWE.

Comments