VIZUIZI VYA KUSHINDWA KUFANYA HUDUMA YA MUNGU IPASAVYO.* sehemu ya tano*



Bwana Yesu asifiwe…
Haleluya…

Kumbuka kwamba tunachoangalia katika fundisho hili ni sababu za msingi zinazowafanya watumishi au mkristo yeyote Yule kushindwa kufanya kazi ya Mungu ipasavyo
.Sababu hizo zinazomzuia au kumfanya mtu aliyeyebeba huduma ya Mungu asiweze kuifanya katika viwango vya juu.
Sababu hizi hujulikana kama VIZUIZI au VIKWAZO.

Karibu tuendelee tulipokuwa tumeishia:
Bwana Yesu aliwaambia hivyo kwa sababu maisha yao yalikuwa ni kula na kunywa muda wote maana wakitumainia uwepo wa Bwana Yesu aliyekuwa akitembea nao muda wote,Hata kujiuliza kwamba, ya nini kufunga na kuomba ikiwa Bwana harusi tuko naye ? ndio maana Yesu anawaambia “ [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.] ”

Yaani kwa maneno mengine ni sawa na kusema
“ iliwapasa muishi katika kufunga na kuomba siku zote ”
Na hiyo ndio maana halisi ya mstari huo (Mathayo 17 :21)

• Hivyo kushindwa kuishi maisha ya kufunga na kuomba ni sababu imfanyayo mtu kushindwa kuitimiza kazi ya Bwana kiukamilifu

• Sababu kufunga na kuomba ni mazoezi ya UTAUWA ambayo mazoezi hayo yanakufanya kutunisha misuli ya kiroho,nayo yanafaa zaidi ya mazoezi ya kimwili maana imeandikwa ;
“ Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.”1 Timotheo 4:8

Kumbuka andiko hili tulilolisoma hapo awali Mathayo 17 :21 “ [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”
Lenye maana ya kufunga na kuomba kama desturi ya maisha ya Mkristo na wala sio kufunga na kuomba kwa kusubili tatizo sugu lije ndio ufunge na kuomba
Au labda kwamba upatapo tatizo ambalo yamkini uliliombea kwa muda mlefu,pasipo majibu kisha ndio ufunge na kuomba,hiyo sio maana halisi ya andiko hilo.

• Lakini ifahamike kuwa sio vibaya wala sio dhambi,wala hajikatazwa kabisa katika Biblia kwamba, endapo utaamua kufunga na kuomba kwa tatitizo uliloliombea pasipo majibu,nayo ni sahihi kabisa,ila:

• Wito wangu kwako ni kuishi maisha ya UTAUWA ya kufunga na kuomba kwanza,maana hata kama tatizo sugu litokeapo basi utakuwa na nguvu ya kulishinda kiurahisi,tofauti na kuishi maisha ya kawaida kisha ndipo uanze kufunga na kuomba wakati wa matatizo tu.

Maana ukifanya hivyo yamkini matatizo hayatatoka kwa sababu kiwango chako cha nguvu juu ya matatizo hayo kitakuwa ni kidogo,na kupelekea kuomba pasipo kupata majibu. Hautakuwa na nguvu ya kutosha ya kuyashinda hayo majaribu pindi yajapo.

Haleluya…
Jina la Bwana libarikiwe…

Kushindwa kuishi maisha ya kufunga na kuomba ni kizuizi kikubwa cha kushindwa kutumika vizuri kwa habari ya mambo ya Mungu.Kiwango chako cha ujazo wa roho mtakatifu kinategemea mazoezi yako ya kiroho.

Mfano mmoja wapo ambao roho mtakatifu anapotaka kujaa ndani ya roho ya mtu ni pale mtu huyo anapokuwa anamfanyia Bwana Ibada ya Kufunga na Kuomba. Tunasoma Luka 4 : 1:

“ Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, ”

Andiko hilo linatupa picha halisi ya namna Roho mtakatifu alipomjaa Bwana Yesu baada ya Bwana Yesu Kufunga na kuomba huko nyikani.
Bwana Yesu aliifahamu Siri hii ya ujazo wa roho Mtakatifu,na ndio maana pale alipojazwa roho mtakatifu mara nyingi alikuwa akifunga na kuomba.
Tazama hata pale kabla ya kuwachagua wanafunzi wake,aliingia katika kufunga na kuomba.

• Ipo siri ya mpenyo katika ibada za kufunga na kuomba.Mfano tunaona Ibada ya kufunga ilivyowakomboa wakina Esta na akina Mordekai baada ya kutaka kuuwawa ,iliwabidi kuingia katika kufunga mbele za Bwana maana ndio ilikuwa njia ya pekee kwao ya kuokoa maisha yao.

Tunasoma Esta 8 :16 :
“16 Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, MKAFUNGE kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.”

Pia tazama habari za mji wa mkubwa wa NINAWI uliokuwa umejaa dhambi,
Biblia inasema watu hawa wa mji huu waliposikia neno la Mungu kupitia Yona wote waliiingia katika toba ya Mfungo na kuomba mbele za Bwana,na kwa njia hiyo ndio ikawa mpenyo wao wasiaangamie kwa hasira ya Bwana,Naye Bwana akawasamehe maovu yao.
Tunasoma :
Yona 3 :5 “ Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.”

• Kumbe tunajifunza neno la msingi hapo ya kuwa, Mungu anaweza kukusamehe endapo utaingia katika toba halisi ya kufunga na kuomba kwa kumaanisha.

Kwa sababu kwa maombi ya namna hii ,yanakuwa yanamgusa sana Bwana Mungu wetu,naye huwa tayari kuachilia msamaha kwetu kwa toba ya kufunga na kuomba.

Yeye aishie katika maisha ya kufunga na kuomba hafilisiki kiimani. Naye muda wote anakuwa ni mshindi zaidi ya mshindi.

ITAENDELEA…
UBARIKIWE.

Comments