Posted by
Peter Mabula
- Get link
 - X
 - Other Apps
 
![]()  | 
Mtumishi Gasper Madumla | 

 
 (Ili kupata mtililiko mzuri wa fundisho hili,tafadhali pitia sehemu 
zilizopita.Na sehemu hizo zinapatikana hapa hapa haina haja ya kuangaika
 kutafuta fundisho hili sehemu nyingine. ) 
 
 Kumbuka kwamba 
tunachoangalia katika fundisho hili ni sababu za msingi zinazowafanya 
watumishi au mkristo yeyote Yule kushindwa kufanya kazi ya Mungu 
ipasavyo.
 Sababu hizo zinazomzuia  au kumfanya  mtu aliyeyebeba 
huduma ya Mungu isiweze kuifanya katika viwango vya juu  hujulikana kama
 VIZUIZI au VIKWAZO.Basi sasa nianze kwa kukusalimu wewe 
mpendwa,nikikuambia,
 
 Bwana Yesu asifiwe…
 Haleluya…
 
 Andiko letu la kusimamia fundisho hili ni Mathayo 17 :20-21 
 “ 20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, 
amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia 
mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno
 lisilowezekana kwenu. 
 21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]” 
 
 Na tuliangalia kiundani juu ya sababu hizo mbili zinazomfanya mtu 
kutokufikia kiwango cha juu cha huduma,na mara nyingi kushindwa kabisa 
kutoa huduma ya ki-Mungu kwa wahitaji,na kwa watu wote wa mataifa.
 Mfano kupitia andiko hilo hapo juu (Mathayo 17 :14-21),
  tulijifunza jinsi gani wanafunzi wa Bwana Yesu walishindwa kufanya 
huduma ya kumtoa pepo mchafu Yule kijana aliyepagawa kwa pepo. 
 
 Sababu hizo ni ;
 • Upungufu wa imani
 • Kushindwa kuishi maisha ya kufunga na kuomba.
 
 (Pitia sehemu zilizopita ujifunze zaidi juu ya sababu hizo mbili.)
 
 -Mtu aliyeokoka nina mfananisha na mtu aliyenunua gari nzuri akiwa 
mtaani kwake. Ambapo mtaani kwake yamkini wanaweza kumcheka kwa 
kejeli,na kusema kuwa;
 
  “ Eeheee!.. hilo gari lenyewe hata 
halimpendezi,tena atakuwa anatudanganya tu, kwa kutuambia eti amenunua 
gari kwa pesa zake! Loh..!
 Sababu hana uwezo wa kumiliki gari,
 Au hata kama kanunua,gari lenyewe ndio hilo,
 hata bure mimi  silichukui..!! 
 Au ni lazima atakuwa amekopeshwa tu,Au kaazima,Au gari litakuwa ni la shemeji yake….n.k ” 
 
 Lakini endapo tatizo likitokea kwa gafla hapo mtaani labda tuseme ndio 
tatizo la kuuguliwa na mtoto wa jirani yake kipindi cha majira ya usiku,
 Ni dhahili kabisa, 
 lazima watamtafuta na kumfuata mtu yule yule waliokuwa wanamsema na 
gari yake ili awapeleke hospitali kwa matibabu ya mto to wao.
 
 Na kwa sababu mtu huyo ana gari,basi yuko ladhi amchukue  mgonjwa na kumpeleka hospitali.
 Ni sawa sawa na mtu aliyeokoka.
 Ukweli ni kwamba kama kusemwa utasemwa sana kwa sababu ya ulokole wako,
 hata mtaani watakubeza kwa maneno ya kejeli,
 Lakini siku ikitokea shida ya mgonjwa hata kama ni majira ya 
usiku,hakika watakuita,nawe kwa sababu umeokoka ,utawasaidia kumuombea 
mgonjwa.
 
 Sikia;
 Ile namna ya  wewe kuwasaidia kumuombea mgonjwa na mgonjwa huyo akapata kupona,
 Ni sawa sawa na Yule aliyechukua gari yake na kumpeleka mgonjwa 
hospitalini kwa uponyaji.Maana hata wewe ulipokuwa unamuombea huyo 
mgonjwa naye akaponywa basi si wewe umponyaye bali ni Yesu aliyemponya,
 Bali wewe umetumika tu kama chombo/kama gari la kumpeleka mgonjwa 
hospitalini,kwa matibabu ya uponyaji,Hospitali hiyo ndio Bwana Yesu 
ambaye ni daktari bingwa wa mabingwa. 
 
 Sasa angalia;
 Endapo
 mtu huyo aliyenunua gari tena pasipo kuifanyia service,kisha akawa 
anaendelea kuitumia kila siku,kila mwezi,na hata kila mwaka,Mwaka hadi 
mwaka.
 Ni ukweli kwamba gari hiyo itakongo’loka na kuharibika kabisa
 kiasi kwamba hata kama kuna mgonjwa akijitokeza kwa gafla ili apelekwe 
hospitalini,
 basi mtu huyo atashindwa kulitumia gari hilo,kwa kumpeleka mgonjwa hospitalini.
 
 Tena anaweza kusababisha kifo kwa mgonjwa kwa sababu gari lipo lakini 
ni bovu,limekosa kufanyiwa services.alikadhalika  mtu aliyokoka asipo 
fanya mazoezi ya kiroho,basi ulokole wake ni bure maana hata ikitokea 
gafla mgonjwa ni ukweli kwamba atashindwa kumuombea kwa jina la Bwana 
Yesu na kupata majibu kwa maombi yaliyoomba.
 
 Oooh!Haleluya…
 Jina la Bwana liinuliwe sana….
 
 *Kushindwa kufanya mazoezi ya kiroho ni kizuizi /sababu kubwa inayopelekea kushindwa kufanya huduma ya Mungu.
 
 Maana hata maandiko yanatuambia kuwa 
 “Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa
 hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule 
utakaokuwapo baadaye.” 1 Timotheo 4 :8
 
 Zipo sababu nyingine ambazo ni kama ukuta wa kushindwa kutekeleza kusudi la Mungu ndani yetu,
 Sababu hizo zinaonekana ni ndogo sana kiasi kwamba twazizalau,Lakini 
mimi leo hii ninakuambia kwamba hakuna jambo dogo mbele za Bwana,maana 
lile ulidhanialo kuwa ni dogo basi kumbe ndio huwa ni kubwa.
 
 Tuangalie kwa ufupi sababu hizo ambazo ni :
 01.Mzaha kwa watumishi wa Mungu
 02.Kulizoelea Neno la Mungu.
 
 01.MZAHA
 Watumishi wengi wanajikuta hawana upako kwa sababu wameruhusu mizaha 
katika utumishi wao,maana watu wa namna hii wamesahau kuwa MIZAHA ni 
dhambi maana Biblia imekataza kabisa mizaha kwa watumishi wa 
Bwana,Tunasoma
 Zab.1:1
 “ Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri
 la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi 
barazani pa wenye mizaha.”
 
 02.KULIZOELEA NENO LA MUNGU.
 
Ulokole wa zamani unatofautiana sana na ulokole wa sasa. Maana watumishi
 wengi wa zamani pindi wamuonapo mtu mwenye dhambi mfano 
mlevi,mzinzi,N.K.Basi  utakuta Watumishi/Mtumishi hulia sana maana hata 
kabla hajamuombea anajisikia kuugua moyoni mwake juu ya dhambi za Yule 
mtu.
 
 Leo hali hii iko tofauti sana na maisha ya ulokole wa sasa
 maana mtu mlokole ambaye ni mtumishi hata amuonapo mtu mwenye dhambi 
kupitiliza,mtumishi huyo utamuona yuko tayari kumuacha aangamie na 
dhambi zake.
 
 Kwa hali hii  inaonesha kuwa neno la Bwana haliko ndani ya watumishi kwa sababu ya kulizoelea Neno la Mungu. 
 Biblia inasema ;
 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko 
upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na 
roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua
 mawazo na makusudi ya moyo. ”Waebrania 4 :12 
 
 Kama tutafahamu hayo ya kuwa neno la Bwana lina nguvu iokowayo,basi kamwe hatuta tamani kuishi kama watu wa mataifa. 
 
 MWISHO
 UBARIKIWE.
- Get link
 - X
 - Other Apps
 

Comments