Historia ya Mwimbaji Sifa John.

Jina langu ni Sifa John. Nilizaliwa katika familia ya kiislamu na ni mtoto wa tano kuzaliwa ila kwa upande wa mama mimi ni mtoto wa pili, na wa kwanza alifariki ambaye alikua anaitwa Mwamvita. Nikiwa muislam nilikua naitwa Tiba Hamadi na baada ya kuokoka siku ambayo nilibatizwa ndipo nikapewa jina la Sifa, na baada ya kuolewa nikawa naitwa Sifa John(John ni Jina la Mume wangu). Baba yangu alitengana na mama yangu baada ya mama kurudi kwenye dini yake awali ya kikristo alikotokea kabla ya kuslim na kuolewa na baba. Baada ya mama kuondoka, baba yangu alioa mke mwengine na ambaye ndiye aliendelea kunilea baada ya kuachwa na mama.

Nilikaa kwa baba yangu mda mrefu bila kumjua mamaangu kwa sababu aliniacha nikiwa mdogo sana mana nilikua na miaka miwili tu, na baada ya kufikisha miaka kumi na nne nilikutana na mkutano wa injili hivyo nikaokoka kupitia mkutano huo. Ugomvi wangu na babaangu mzazi ulianzia hapo. Baba alikasirika sana na akanitenga kabisa na akakataa kuniendeleza kimasomo, na aliniambia hata akifa nisifike na mimi nikifa hatofika kwenye Mazishi. Lakini pamoja na yote baba yangu ananipenda sanaaaaana. na niliwahi kupata ajali ya mguu, mfupa ukakatika mara mbili na kupishana ikawa kwamba nikatwe mguu. Baba yangu alikua analia sanaaa kila akija hospitali.

Madaktari walikua wakimtoa nje mara kwa mara kwajili ya kulia, lakini alipambana kiume na kukwangua acount yake yote ili mimi nisikatwe mguu, mana aliambiwa kwamba ili nipone dawa inatakiwa iagizwe Ufaransa. Baba hakusita juu ya hilo kwani dawa iliagizwa hivyo nikatibiwa mpaka sasa nina miguu yote miwili. Hii yote ni kwaajili ya upendo wa baba yangu, hata mimi nampenda sanaaa baba yangu, lakini ninachomshukuru Mungu baba yangu amerejeza Moyo na sasa tunaishi nae kwa upendo sanaaa.

HISTORIA YAKE KIUIMBAJI
Nilianza huduma ya uimbaji Mwaka 1983 katika kwaya moja ya kanisa la Mchungaji Lukindo Kawe, na wakati huo nilikua nasoma Shule ya Msingi Kawe darasa la 4. Badae niliimba kwaya ya Yerusalem ya kanisa la Pentecoste Kawe-Mbezi kwa Mchungaji Kibingu Marandura ambae kwa sasa ni marehemu.Nipoolewa nilianza kuimba kwaya ya kanisa la EAGT Imani Choir ambayo ilikua chini ya kanisa la Mch. Ernesti Nyanda aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, na hapo nilikua Sololist niliyevuma sana na wimbo wa Kigeugeu. Hiyo ilikuwa ni katika mkoa wa Mwanza.

Badae nilichukuliwa na Kwaya ya Calvary EAGT Nyamanoro kwa Mch Kapera nikiwa Sololist na nilivuma sana kwa wimbo wa Malaika katika Kanisa la Efeso. Hapo sasa nilipata mtu mmoja anaitwa Gahutu akanidhamini nikatoa Album yangu ya kwanza ya Wateule Tutakwenda. Kwa sasa nimetoa album yangu ya pili ujulikanayo kama Usililie Moyoni Yupo Mungu.
Namshukuru sana Mungu ananipigania sana katika huduma hii mana nimekuwa nikisafiri huku na huko kwa ajili ya huduma na ananilinda sana. Pia kupitia huduma ya uimbaji nimefanikiwa kuanzisha huduma ya kusaidia watoto yatima na watoto waishio katika mazingira magumu. Pia ninao vijana ambao walikua wamekata tamaa tunaowapa mafunzo mbali mbali kama kushona, uigizaji, na computer.

Watoto hao nilionao wanapata misaada mbali mbali kama vile elimu mana kuna walimu wanawafundisha hapo kituoni mana walikua hawajawahi kusoma kwajili ya matatizo na shida walizonazo na kukosa msaada.

Comments