![]() |
Mwl Nickson Mabena akifundisha neno la MUNGU na hapo ni Mruvango, wilayani Siha mpakani mwa mkoa wa Kilimanjaro na Arusha. |
1.Hututenga na Mungu ( Mwanzo 3:23,24 ; Isaya 59:2)
"Lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na DHAMBI zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia". Isaya 59;2
2. Wenye dhambi hukataliwa mbinguni.
(1Kor 6:9-11, ; Gal 5:19-21; Efeso 5:3-7, ufunuo 21:27)
"Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji,........" 1Kor 6:9-11
3. Dhambi huleta hasira ya Mungu
(Kumb 25:16; Mith 6:16-19, 1Falme 16:2)
"Kwa kuwa wote wayatendao yasio haki, ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako". Kumb 25:16
![]() |
dhambi ni mbaya sana |
a) Ardhi inalaaniwa kwa sababu ya dhambi.
"Akamwambia Adamu, kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nlikuagiza,nikasema, usiyale; Ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako......" Mwanzo 3:17-18
b) Kazi ngumu kwa jasho kwa sababu ya dhambi.
"Kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi..." Mwanzo 3:16,17,19
"Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu" Ayubu 14:1
c) Uchungu wakati wa kujifungua kwa sababu ya dhambi.
"Akamwambia mwanamke, hakika nitakuzidishia uchungu wako na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.
Tukipata muda mwingine, kadri Mungu atakavyotujalia, tutaendelea na somo. Ubarikiwe!
By mwl Nickson Mabena
Comments