Mfahamu kiundani Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Sam Batenzi.

SAM 1
Samwel Batenzi maarufu sana kwa jina la Sam Batenzi, ni Mwimbaji Chipukizi wa Nyimbo za Injili anayekuja kwa kasi ya Ajabu katika tasnia ya Muziki wa Injili Tanzania, kutokana na Uimbaji wake un avyowabariki watu wa Mungu. Kwa mara ya Kwanza, nilikutana na Sam Jijini Mwanza katika kituo cha Kazi yaani HHC ALIVE FM (91.9Mhz), na ndipo hapo nilipopata shauku ya Kumfahamu zaidi.


                           HISTORIA YAKE KIMAISHA Sam alizaliwa miaka 25 iliyopita katika Mkoa wa Mwanza, katika familia ya kikuhani ya Bishop David Batenzi na Mama Batenzi. Sam ni mtoto wa 3 kati ya watoto 4 wa Askofu Batenzi, na kabila lake ni Mnyamwezi kwa Upande wa Baba, na Msukuma kwa Upande wa Mama.
 

                            HISTORIA YAKE KIMUZIKI
Sam alianza kujishughulisha na Maswala ya Kimuziki Mwaka 2000, lakini katika kujifunza vyombo vya Muziki huko Mkoani Mwanza. Na alianza rasmi uimbaji Mwaka 2004 huko Tabora katika shule moja iliyojulikana kama Umoja Secondary School.


Nilipotaka kufahamu ni Kwanini aliamua kuimba Muziki wa Injili na Si aina Nyingine ya Muziki, Sam alisema; “Nimeamua kumtumikia Mungu katika Uimbaji wa Muziki wa Injili kwa sababu Muziki wa Injili ndio muziki ambao umekuwa ukigusa maisha yangu kwa aina moja au nyingine, lakini naweza sema pia nilizaliwa katika familia ya kikristo na kukulia katika Malezi ya Kikristo.Na pia nilipompokea kristo kama mwokozi wa maisha yangu, ndipo nilipogundua nini Mungu amenizawadia, nami nikatumia zawadi hiyo kufanya kazi yake.”
 

Vipi kuhusu vikundi/kwaya ambazo Sam ameimbia?
Hapa Sam anasema; “Nilipokuwa shule niliimbia kikundi kimoja kilijulikana kama LPP (Long Pray Praise) ambacho naweza sema ndo waliendeleza kile Mungu ameweka ndani yangu, lakina pia nimewahi imbia Dar es Salaam Gospel Choir DGC ya Dar, na nimewahi kuwa member kwa muda katika kundi moja la kusifu na kuabudu linajulikana kama New Wine la Dar.
 


Nini ambacho Sam anafanya kwa Sasa?
“Kwasasa nimekuwa nafanya kazi za Uimbaji na vikundi ambavyo vimekuwa vinatengenezwa kwa muda kwa ajili ya kazi fulani tu baadae kinaisha baada ya hiyo kazi.

Kuhusu aina ya Muziki ambao Sam anaupenda sana ni African Music kama Zouk,Rhumba,Qwato,Sebene,Tradition music, lakini pia napenda pia Black Gospel,Jazz,RnB,Soul, na Soft rock.


Ni Mwimbaji gani wa Gospel unaempenda zaidi kwa Hapa Nyumbani?
“Mwimbaji wa Gospel kwa hapa nyumbani naweza sema Jackson Benty, Minza na John Lisu zaidi ya hapo labda vikundi kama Next Level, Sowers, Holy of Holies, Calvary Band, UGM. Ila napenda zaidi makundi.
 

Vipi ulishawahi kurekodi Wimbo wowote?
“Nilipoanza muziki tulirekodi na hilo kundi ambalo nilijiunga nalo la LPP, mbali ya hapo nimekuwa nafanya na watu tu, ila ndo nimeanza taratibu za kuandaa album yangu ya kwanza maana sikupenda sana muziki wa kurekodi studio. Napenda sana muziki wa live, na hata kama ni kurekodi iwe live on stage maana naamini ndo unakuwa na mguso wa aina yake na kuwa karibu na Mungu at a particular time”


Mbali ya Uimbaji, ni Kazi gani Nyingine unayojishughulisha nayo?
“Mbali ya Uimbaji, nafanya kazi ya Video Shooting pamoja na Editing. Maana nda Taaluma yangu hiyo.”
 

Vipi umeshajiunga na Chama cha Waimbaji wa Nyimbo za Injili?
“Kiukweli bado sijajiunga na chama cha waimbaji, maana sikuwa asilimia zote kwa muziki maana nimekuwa na shughuli zingine hasa za kimasomo labda kwa sasa ndo naweza kuanza taratibu za kujiunga.”
 

Ni aina gani ya Muziki unaofanya?
“Mimi nafanya muziki wa asili ya kiafrika ambao nimeupa jina la African Christian Soul (Afrocso), na hii ni kutokana na kugundua sisi Tanzania tumebarikiwa na miziki mbalimbali ya asili ambayo ikifanyiwa kazi, inakuwa mizuri sana badala ya kuanza kucopy nchi za magharibi. Kkwahiyo huo ndo aina ya muziki ambao mimi naimba katika kumtukuza Mungu.”


Ni vyombo gani vya Muziki unavyoweza kupiga?
“Napiga vyombo mbali kama bass guitar, acoustic guitar, kinanda, solo guitar na drums kidogo, ila zaidi chombo changu ni Bass guitar.”
 

Nini Malengo yako ya Baadae?
“Malengo yangu ni kumtukuza Mungu katika anga za kimataifa, na kundi ambalo nililianzisha mwaka jana kwa jina la “The Psalmists” ambalo hadi sasa tumeshafanya matamsaha mawili moja lilifanyika Dar 9 – 1 – 2011 katika kanisa la FPCT Kurasini, na la pili Mwanza 8 – 1- 2012 katika kanisa la FPCT kitangiri pia naanda matamasha mengi zaidi ambayo sasa hivi yatakuwa na muziki wa asili zaidi ili ku’promote such kind of music which is much blesses much”

                     by
Gospel News Media

Comments