“UMESEMA KWAMBA YESU WAKO ANAPONYA, THIBITISHA SASA!”



Mtumishi wa Mungu Benny Hinn
Hayo yalikuwa maneno ya mlemavu mmoja aliyepanda jukwaani pamoja na familia yake na wakati mimi nilipokuwa ninaendelea kuhubiri.
Ujumbe wangu niliokuwa nikiuhubiri ulikuwa juu ya nguvu za Mungu ya kuokoa ,kuponya na kujaza Roho Mtakatifu. Wakati nakaribia nusu ya ujumbe niliokuwa nauhubiri ,ghafla nilimwona kijana wa kihindi na familia yake
,taratibu wakitembea kwenye njia iliyo katikati ya viti wakija jukwaani. Mume alikuwa anachechemea Sana. Niliwaza “Bwana, hii ni ajabu wanakuja kutoa maisha yao kwako”
Hawakusita walikuja mpaka kwenye madhabahu.Hakuna aliyewazuia wakati wanapanda ngazi hadi waliposimama mbele yangu.Nilipigwa butwaa nikaacha kuhubiri na kusema, Niwasaidie nini?

Mtu yule alinitazama kwa macho makavu na kusema “Umekuwa ukituambia kuwa Yesu yu hai, leo mimi nina miaka Ishirini na nane na ni kilema,mke wangu naye ana kansa. Tazama ngozi ya binti yangu inatoka damu kwa sababu ya ugonjwa na ukurutu mkali,hakuna mtu aliyeweza kumsaidia.Unasema kuwa Yesu wako anaponya thibitisha sasa!

Kusanyiko lote lilifunikwa na ukimya wa ajabu, watu wote walinikazia macho pale jukwaani.Niliwatazama watumishi, nao walikuwa wameduwaa maana hawakutegemea jambo kama lile kutokea.

Niliwaita kwangu wale watu na kusema, Ndugu zangu tupige magoti na kumwita Bwana,Kisha nikaomba,”Bwana Yesu mtu huyu ananiambia nithibitishe kile ninachohubiri ,lakini Bwana mimi sihubiri injili yangu,nahubiri injili yako wewe,wewe ndio uthibitisho.”Japo kuwa niliomba kwa ujasiri sikujua nini cha kufanya baada ya hapo.Ilionekana kama muda nao umesimama,mkutano mzima hakuna sauti liyosikika.Nikiwa nimepiga goti tu pale huku macho yangu nikiwa nimeyafunga na nikiendelea kuomba.

Ghafla kukawa na kelele kubwa ambayo ilinishtua nikaamua kufungua macho,Nilipo angaza macho nilimwona yule mtu,mke wake na binti wote wamedondoka pale sakafuni na uwepo wa Mungu wa tofauti ulikuwa umelifunika lile eneo.Baada ya mda mfupi hatimaye walianza kuinuka,baba alipomtazama binti yake alianza kupiga kelele na kulia huku machozi yakimtoka.Mikono ya binti yake ilikuwa haitoi damu tena.Nilishangaa kuona si damu tu iliyokoma bali hata ngozi yake ilionekana kuwa kama mpya.Muda ule ule baba yake alianza kukimbia kuzunguka jukwaa,akisema,nimepona nimepona.Mguu wake wenye ulemavu ulipona dakika hile hile.Mke wake alipoanza kujichunguza naye akagundua kuwa Mungu amemgusa pia.
Uwepo wa Roho Mtakatifu ulibadilisha mkutano ule kiasi kwamba maelfu ya watu waliamua kusalimisha maisha yao kwa Yesu siku ile.Roho Mtakatifu anapokuwa kazini ,hatuitaji kuonyesha au kuthibitisha chochote,Yeye hututumia sisi katika huduma lakini ni uweza wake na ujumbe wake ndio unaoleta uzima.

 



Habari hii imenukuliwa na Masawe Gilbert  (hapa )toka kwa Mtumishi Benny Hinn  Katika kitabu chake”Welcome Holy Spirit”(Karibu Roho Mtakatifu)
Ukurasa wa 172-173

Comments