ASKOFU MKUU MOSES KULOLA AFARIKI DUNIA

Askofu  Dr.Moses Kulola enzi za uhai wake
Taarifa imetolewa na Mchangaji  Daniel Kulola kupitia mtandao wa kijamii wa facebook kuwa mzee wetu Askofu Mkuu wa EAGT askofu MOSES KULOLA amefariki dunia.  hii hapa ripoti hiyo

''WATU WA MUNGU SALAAM, NINA SALAAM ZA MAJONZI. BABA YANGU MZEE KULOLA AMEFARIKI... MUDA SIYO MREFU''.
MWANAYE Dr. DANIEL KULOLA


 Askofu mkuu na mwanzilishi wa kanisa la EAGT nchini Tanzania Dr.Moses kulola amefariki Dunia jijini Dar es Salaam ambapo alikua akiendelea na matibabu katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam.
Askofu .Dr Moses Kulola katika mwaka huu alikua akisumbuliwa na matatizo ya kiafya hali iliyopelekea kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi ambapo hivi karibuni alirudishwa nchini Tanzania kuendelea na matibabu yake mpaka Bwana alipomtwaa  akiwa na umri wa miaka 85.

Itakumbukwa kwamba Askofu Dr.Moses kulola ambaye amekua baba wa kiroho wa watumishi wengi wakubwa kwa wadoo wa kiroho ndani na nje ya Tanzania katika kipindi chote cha uhai wake amekua mfano mzuri wa kuigwa kwa kuweza kuhubiri injili katika vijiji na miji yote na kuwaleta mamilion ya watu kwa Yesu,

ASKOFU MKUU MOSES KULOLA ENZI ZA UHAI WAKE  NA HAPA ILIKUA NI VIWANJA VYA JANGWANI MWAKA JANA
Askofu Moses Kulola na Mchungaji Daniel Kulola

Comments