Kwenye Biblia, katika Kitabu cha Yona,
tunapata habari za watumishi wa ile Melikebu aliyopanda Yona, jinsi
walivyohangaika baharini, wakatosa mizigo yao wakitafuta ufumbuzi wa
namna ya kupita katika ile dhoruba lakini haikusaidia. Walipomtosa Yona
Baharini DHORUBA ilitulia, wakafanikiwa kuendelea na safari yao.
Yawezekana unafanya kazi pamoja na
mtu, au unashirikiana naye. Lakini mambo yamekuwa hayaendi. Kabla hujawa
naye mambo yalikuwa sawa tu, lakini sasa DHORUBA ni kubwa. Unajaribu
kuacha baadhi ya mambo/Majukumu ili muweze kujikita katika machache
lakini bado haisadii. Kaa chini.
Omba Mungu akufunulie. Wale jamaa wa
kwenye melikebu walipiga kura, ikamwangukia Yona. Yawezekana uliye naye
hapo AMEKIMBIA KAZI YA MUNGU/WITO ama kwa kujua au kutokujua. Pengine
alitakiwa achunge Kanisa au alitakiwa awe mahali fulani akiihubiri
Injili. Utashangaa, mkigundua kusudi la Mungu lililo nyuma ya matatizo
mnayopitia, amani itapatikana na SHUGHULI yako Itasimama Imara Tena!
Comments