![]() |
NA PETER MICHAEL MABULA |
BWANA
YESU asifiwe ndugu, leo tunajifunza somo linaloitwa JEHOVAH RAPHA yaani MUNGU
atuponyae kama ilivyo katika Biblia kitabu cha Kutoka 15:26 katika kiebrania.
MUNGU
wako lazima awe MUNGU aponyae na yeye yuko siku zote kwa ajili ya kuponya,
jambo muhimu ni kwenda tu kanisani kwenye maombezi katika jina la YESU KRISTO.
[kutoka 15:26] Biblia
inasema
‘’Akawambia kwamba utaisikiza kwa biidi sauti ya BWANA MUNGU
wako na kuyafanya yaliyoelekea
mbele zake na kutega masikio usikie maagizo yake na kuzishika amri zake Mimi sitatia juu yako
maradhi yoyote niliyowatia wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi
BWANA NIKUPONYAE ‘’
hapo kwenye neno BWANA NIKUPONYAE ndipo hasa kwenye kiini cha somo letu na BWANA NIKUPONYAE kwa lugha ya kiebrania ni JEHOVAH RAPHA.
ndugu zangu naomba ufahamu kwamba MUNGU hapendi kabisa kuwatesa wanadamu na magonjwa ni mashambulizi ya shetani na ndio maana kwa kusudi hilo BWANA YESU alidhihilishwa ili kuzivunja kazi za shetani (1 Yohana 3:8) na katika Maombolezo 3:33 Biblia inatuambia kuwa MUNGU hapendi kuwatesa wanadamu.
[maombolezo3:33]
‘’Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu wala
kuwahuzunisha ‘’hapo kwenye neno BWANA NIKUPONYAE ndipo hasa kwenye kiini cha somo letu na BWANA NIKUPONYAE kwa lugha ya kiebrania ni JEHOVAH RAPHA.
ndugu zangu naomba ufahamu kwamba MUNGU hapendi kabisa kuwatesa wanadamu na magonjwa ni mashambulizi ya shetani na ndio maana kwa kusudi hilo BWANA YESU alidhihilishwa ili kuzivunja kazi za shetani (1 Yohana 3:8) na katika Maombolezo 3:33 Biblia inatuambia kuwa MUNGU hapendi kuwatesa wanadamu.
-Uponyaji hupatikana pale MUNGU
anapoingilia kati
-Miujiza ni ni
tendo la kimungu
ambalo liko juu ya kanuni za
kibinadamu [yohana3:2]
‘’Huyu alimjia usiku akamwambia
Rabi twajua ya kuwa u mwalimu
umetoka kwa MUNGU kwa
maana hakuna mtu
awezaye kuzifanya ishara hizi
wafanyazo wewe isipokuwa MUNGU yu pamoja
naye
-Maana huyu alikuwa
ametengwa yaani najisi au ni mtu
aliyetengwa Mbali na watu
- ndugu ili upokee uponyaji lazima ujue neno la MUNGU linasemaje juu ugonjwa wako. Na uponyaji sio kupona ugonjwa tu bali hata mambo mengine ambayo unataka yapone hivyo ni muhimu kujua neno la MUNGU linasemaje juu ya ugonjwa, maovu, matendo au hata maisha yako
Mama huyu katika [marko 5:25-34] alisema ‘’nikigusa tu nitapona yaani alichora picha moyoni pia [marko
9:23] -ukiweza yote yanawezekana kwake yeye aminiye] maisha yako
[isaya 53:5
‘’-Bali alijeruhiwa kwa
makosa yetu Adhabu ya amani yetu
ilikuwa juu jake na
kwa kupigwa kwake
sisi tumepona’’
-Ndugu mpendwa napenda kukujulisha kwamba BWANA YESU ana nguvu sana na kwa macho yangu nimeshuhudia dada mmoja akipona UKIMWI, kaka mmoja tena ni mzee wetu wa kanisa akipona kifua kikuu(TB) na wengine wengi sana ambao wamepona magonjwa mbalimbali mengi sana na hata wewe unayeumwa hakikisha tu unaende kanisani ambapo wanamhubiri YESU na utaombewa na kupona kabisa maana hakuna ugonjwa ambao kwa YESU unashindikana. Hata kama huna neno la kujua kuhusu ugonjwa wako lakini ile imani tu ya kumwamini BWANA ya kumwanini YESU ni neno kwani Biblia inasema katika Yohana 6:44 Kwamba ‘’ Hakuna mtu awezaye kuja kwangu , asipovutwa na nguvu ya BABA aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.’’
-YESU ana nguvu [mathayo 8:5,13]
‘’YESU akawaambia nitakuja
niponye
KWANINI YESU ALIKUJA DUNIANI ?
Kuna vifo vya aina
mbili vilikua vimetokea na sababu ya BWANA YESU kuja ili ule uhusiano wetu na MUNGU Baba yetu urudi na pia magonjwa na kila mapando ya shetani yaondolewa, tuwe wazima
1-kifo cha kimwili
yaani mwili kutengana na roho
2-Roho na mwili kutengana
na MUNGU milele
YESU alikua kurudisha haya yaani kwa njia ya kumpa YESU maisha yetu kile kilichoyutenga na MUNGU wetu hakipo tena
-YESU anamtafuta mwenge imani
mfano Yairo na watu waliokuwa wanamsonga YESU katika [Luka 17:11,19] wengine wakaondoka
ila mmoja aliokoka
9 wakaondoka baada kupona ila
mmoja tu ndio akarudi hivyo ndugu hapa tunajifunza kwamba kuokoka
na miujiza ni tofauti. Watu 9
walitendewa miujiza lakini aliyeokoka ni mmoja tu Hivyo baada ya YESU kukuponya
hakikisha unadumu katika kumwabudu MUNGU pamoja na wengine katika kanisa.
MUNGU akubariki sana na kama hujaokoka nakuomba mpe BWANA YESU maisha yako na hiyo itakuwa ni chanzo cha uponyaji wako wa kila kitu kinachokusumbua.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
MUNGU akubariki sana na kama hujaokoka nakuomba mpe BWANA YESU maisha yako na hiyo itakuwa ni chanzo cha uponyaji wako wa kila kitu kinachokusumbua.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
Comments