Jeneza lililohifadhi mwili wa marehemu, Askofu Mkuu, Moses Kulola. ©Philemon Rupia/WAPO Media |
Kutokana na maelfu ya watu kujitokeza kwa wingi kumuaga Askofu wa
Maaskofu, Baba/Babu wa kiroho kwa wengi nchini, zoezi la kuaga mwili
wake limesitishwa kwa muda kutokana na idadi ya watu kuelemea eneo la
tukio, kwenye kanisa la EAGT Temeke.
Gospel Kitaa imeshuhudia kila mtu akijitahidi kw akadri ya uwezo wake
kufika eneo ambalo jeneza lipo ili apate kutoa heshima zake za mwisho,
lakini umati wa watu kufanyika kizuizi, ambapo pia hitilafu ya mitambo
iliyopelekea vipaza sauti kuzimika, imechangia kupungua kwa ufanisi wa
mawasiliano eneo hilo.
Huenda zoezi likasitishwa kabisa iwapo mambo hayatokaa sawa, ila kwa
kadri waratibu wanavyoweka mambo sawasawa, nafasi ya kuendelea kuaga
inatumainiwa zaidi na kila aliyeacha
shughuli zake kutokana na umuhimu wa hayati kwenye maisha yao.CHANZO NI GOSPEL KITAA
Comments