-Majaribu ni
kushawishi kutenda kinyume na
mapenzi ya MUNGU
-Ni kipimo
kwa mtu yaani
yuko imara na anafaa?
‘’Heri mtu
anastahimilie majaribu kwa
sababu akiisha kukubariwa
ataipokea taji ya uzima BWANA aliowaahidi wampendao
{1 petro 6;7}
‘’Mnafurahi sana
wakati huo ijapokuwa
kwa kitambo kidogo
ikiwa ni laazima
mmehuzunishwa kwa majaribu
ya namna mbalimbali
- KINACHO
JARIBIWA NI NINI?
- Ni imani
ya mtu
-ANAYESABABISHA
JARIBU.
1-Mtu
kujua au kusababisha mwenyewe
2-Watu wengine
kusababisha jaribu hilo
AINA ZA
MAJARIBU
1-MUNGU mwenyewe {zaburi 11:5}
‘’BWANA humjaribu
mweyehaki Bali nafsi yake
humchukia asiye haki
na mwenye udhalimu’’ {mwazo
22:1-2-Ikawa baada ya mambo hayo MUNGU alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
Akasema, Umchukue mwanao, mwana
wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria,
ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo
nitakaokuambia.
} {mithali 17:3}
{…….bali BWANA humjaribu mioyo } na {waebrania 10:32-33 Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu;
pindi mlipotwezwa kwa mashutumu na dhiki, na pindi mliposhirikiana na wale waliotendewa hayo.
}
2- Mtu
mwenyewe binafsi {wagaratia 5:16}
‘’Basi nasema
enendeni kwa roho
wala hamtazitimiza kamwe taama
za mwili ‘’
-Tamaa ya mtu
inaweza kuwa jaribu
-Kuwepo mahali
kwa wakati usio sahihi inaweza kuwa jaribu kwako {2samweli 11:1-12} {waefeso 5:15-16 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
}
-Tabia ya
mtu mwenyewe {mithali 6:25-26-Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.
Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani
} Pia {mithali 15: 1-2}‘’Basi umetengwa
kwa maneno ya
kinywa chako umekamatwa
kwa maneno ya kinywa
chako
Maana kwa
Malaya mtu hutiwa katika
hali ya kuhitaji
kipande cha mkate na
kahaba humwinda mtu
anasema nafsi yake
iliyo ya thamani.
Jawabu la upole hugeuza
hasira Bali neno liumizalo huchochea
ghadhabu,ulimi wa mwenye
hekima hutamka maarifa
vizuri Bali vinywa
vya wapumbavu humwaga
upumbavu
3-
Jaribu la shetani
{massa} {1wathesalonike 3:5}
‘’Kwa hiyo
mimi nami nilipo
siwezi kuvumilia tena nalituma
ili niijue imani
yenu asije Yule
mjaribu akawajaribu na
tabu yenu ikawa haina
faida
{mathayo 4:3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.
} ,{1kor 10 :13Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila
Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini
pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze
kustahimili.
} {yohana 16:33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.
}
KWANINI TUJARIBIWE?
a. tunajaribiwa
ili kuangalia uimara wa imani yetu.
b. kutaka kutunyenyekesha
c. ili kumtambua
MUNGU {danieli 3:28-29} {1perto 1:12}
{luka 23: 47-48}
TUFANYE NINI WAKATI WA JARIBU
1: Inatupasa kufurahi
{nehemia 8:10}
2: Maombi {mathayo 26:4 }
‘’kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni roho radhi
lakini mwili ni dhaifu
3: usiwe mtu
mwenye lawama{2 timotheo 4:16-17 Katika jawabu langu la kwanza
hakuna mtu aliyesimama upande wangu, bali wote waliniacha; naomba
wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
Lakini BWANA alisimama
pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa
utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha
simba.
}.
Hitimisho langu ni hili
{Yakobo 1:13-15-Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na MUNGU; maana MUNGU hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu.
Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
}.
ndugu zangu wapendwa watu wengi sana wamekuwa kwenye majaribu na kudhani kuwa wanajaribiwa na MUNGU kumbe ni tamaa zao wenyewe maana MUNGU hawezi kumjaribu mtu kwa uovu na pia na MUNGU anapomjaribu mtumishi wake kwanza huyo mtumishi anakuwa katika hali nzuri kiroho yaani amejaa Roho wa MUNGU sio wale ambao kwa tamaa zao wenyewe wanadhani wanajaribiwa na MUNGU pia wengine kwa sababu ya kupungukiwa na maombi wanajikuta wanajaribiwa huku wao wakidhani wanajaribiwa na MUNGU kumbe walilala tu usingizi wa kiroho ndio maana wako katika majaribu hayo.
MUNGU akubariki sana ndugu na pia kama hujaokoka nakushauri leo chukua hatua za kumpa BWANA YESU maisha yako ili ufanyike mtoto wa MUNGU na uwe mbali na kuonewa na shetani na mawakala wake majini, wachawi na kila aina ya kazi za shetani.
MUNGU akubariki sana ndugu na pia kama hujaokoka nakushauri leo chukua hatua za kumpa BWANA YESU maisha yako ili ufanyike mtoto wa MUNGU na uwe mbali na kuonewa na shetani na mawakala wake majini, wachawi na kila aina ya kazi za shetani.
YESU KRISTO BAWANA wa utukufu anakupenda sana
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
maisha ya ushindi
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
maisha ya ushindi
Comments