MTOTO WANGU ALIPAA HUKU AMESIMAA

LILY PETER NA MWANAYE TROY
BWANA asifiwe mtumishi! usiku nimeshuhudia kitu kwa macho yangu sikuwa katika ndoto,ilikua usiku wa saa tisa na dk 35 mtoto alikua ameamka analialia nikawa nambembeleza lakini hanyamazi cha ajabu kuna mtu alitokea kitandani ghafla akamgusa mtoto baada ya kumgusa, mtoto akaanza kupaa huku amesimama na kitandani kikabaki kivuli,nilijaribu kuongea nilishindwa,nikawa namwita mume wangu sauti haitoki,nikitaka kutaja jina la YESU nashindwa,nikaamua kusali kimoyomoyo nikaona mikono ya mtu mwingine sikujua ni nani ila alikua anamsaidia mtoto asipae! naamini alikuwa malaika wa BWANA alikuja kumzuia asipae baada ya mimi kusali,pia naamin hawakumchukua kwasababu MUNGU alionyesha muujiza wake.
By Lily Peter

Kutoka maisha ya ushindi.

MUNGU akubariki sana na vikwazo vya shetani vipo lakini MUNGU wetu ni mshindi tu siku zote ninachokuomba endelea na maombi na pia watu hao wana mpango mbaya na mtoto wako ila MUNGU yuko upande wako kukutetea maana umemtegemea yeye hata hivyo ukiweza nenda kanisani kwa maombezi zaidi au hata ukiweza unaweza kuja kanisani kwetu hata leo mchana tukakuombea na MUNGU wa miujiza akatenda muujiza wake na pia hata sisi kuja huko ili kukuombea inawezekana sana. MUNGU akubariki pia ushuhuda wako huu naomba kama ukiniruhusu niuweke kwenye blog na page yetu ili wengi zaidi wajifunze kumtegemea MUNGU kama ulivyofanya wewe na MUNGU akamtuma malaika wake ili kukuokoka wewe na mtoto wako lakini haya ni mpaka wewe mwenyewe uruhusu. ubarikiwe sana

Kutoka kwa Lily Peter
Amina mchungaji,hakika Mungu ni mwema! Unaweza kuuweka hakuna tatizo
 Kutoka maisha ya ushindi.

amen ndugu yangu japokua mimi sio mchungaji ila ni muumini tu. Hata hivyo MUNGU akubariki sana na kila kusudi la shetani dhidi yako na mtoto wako halitafanikiwa kwa jina la YESU KRISTO.
Nakufunika kwa damu ya YESU KRISTO na pia nakuomba kumbuka tu kuokoka ni jambo muhimu sana hivyo unaweza kutafuta kanisa huko huko uliko ambalo ni kanisa la kiroho na ukiwaeleza watakusaidia. pia kama ukipenda naweza kuwaambia wadada kama wewe watatu wakaja wakaomba pamoja na wewe huko kwako. MUNGU akubariki sana na aendelee kukutetea siku zote na Troy akue katika KRISTO amkimbpendeza MUNGU na wanadamu. AMEN

Photo
TROY NA MAMA YAKE

Comments