MWONEKANO WA VIJANA MBELE ZA WAZAZI KWA SASA NDIYO SURA YAO YA BAADAYE.

Na Bishop YONA   P  SOLA LEMA
Kanisa la SAFINA VICTORY PENTECOSTAL
Ungalimited, Arusha
0754049163.



(Luka 2: 52 Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu. )
Yesu anaonyesha mwonekano).

(Zab 11:3Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?)

 -Jinsi kijana wa kiume anavyoishi na Mama yake ndivyo atakavyoishi na mkewe.

   -Jinsi Binti anavyoishi na Baba yake ndivyo atakavyoishi na mume wake.


 -Ni mambo machache tu yatakayobadilika au kuongezeka au kupungua.


- Vijana wetu wana nafasi nzuri ya kujitengenezea tabia za kuwasaidia mbeleni wakati wakiwa na wazazi wao au walezi wao.


Msingi mzuri unaweza kujenga tu pale ukiwa na wazazi wako (Tabia hujengwa).


- Kijana wa kiume kumjali Mama yake/kumpenda (Mith 4:1-3-Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu. Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu.  Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu, Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu) kumtia moyo /kumnunulia kitenge / kuwa karibu.


- Binti kumjali Baba yake / kushauriana naye mambo baadhi/kumweshimu.


Familia nyingi ambazo zina matatizo mengi pamoja na shambulio la shetani, lakini inategemea kijana wa kiume au wa kike anavyokuwa anaishi na wazazi wake.


- Bwana akiamka asubuhi hajui kumsalimia Baba yake kumpokea.

Kijana wa Kiume hajui kumsalimia Mama yake humdharau, hana upendo wowote kwa Mama yake.


- Swala la unyenyekevu linaanzia kwa wazazi pamoja na utii.

Kama una tabia umezificha wakati wa uchumba zitajitokeza wakati umeshaolewa au kuolewa.

Kama unazo tabia hukuzifanya kwa wazazi wako ambazo zilistahili uwape zitakutesa sana katuka ndoa yako, apandacho mtu ndicho atavuna (Gal 6: 7 Msidanganyike, MUNGU hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. )


-Kama utaolewa au kuolewa jitahidi kuishi vizuri na wazazi wako, jifunze kunyenyekea, kutii, kuwapa pole, asante, nisamehe haya ndiyo maisha ya kila siku.


- Kuwaletea wazazi wako zawadi hata kama ni pipi, tunda nk kwa tabia hapa mnaijenga itakusaidia.
MUNGU awabariki sana by Bishop YONA   P  SOLA LEMA
Kanisa la SAFINA VICTORY PENTECOSTAL
Ungalimited, Arusha
0754049163.
karibu kwa maombezi na ushauri wa kibiblia

Comments