MZEE HUYU ANAIBA MADUKANI KWA KUTUMIA MAJINI.


     
PICHA YA MFANO
  

Hili ni tukio la kweli ambalo limetokea hapa hapa Tanzania katika moja wapo ya miji mikubwa na limekua likifanyika kwa muda mrefu sana hadi MUNGU alipoamua kuingilia kati ili kuwasaidia wafanya biashara hawa  ambapo mzee huyu alifanikiwa kuiba kwa muda mrefu  na ameiba maduka mengi sana na kuwafilisi wengi sana . 

Mzee huyu ambaye ni mstaafu serikalini ambaye ana miaka 83 sasa amekua na tabia ya kuwaibia wauza duka kwa kutumia fimbo yake ambayo hajawahi kuiacha hata siku moja. Ambapo anachofanya ni kwenda dukani na akifika fimbo yake anaiweka pembeni kidogo ukutani jirani na duka au pembeni tu kidogo na mlango wa kuingia dukani na anachofanya mzee huyu ni kupiga stori na muuzaji wa duka ambapo mzee huyu huongea mengi sana ya kawaida tu maana kuna siku anaongelea siasa wakati mwingine historia na mambo mengine mengi na, hupata watu wengi sana wa kumsikiliza lakini yote hayo huyafanya akisubiria tu fimbo yake ijae pesa ndipo anaaga na kuondoka kwenda kutoa pesa nyumbani kutoka
   ndani ya fimbo na harafu anaenda duka jingine kuiba na kwa mjibu wa mzee huyo  kwa siku anaweza kuiba maduka 4 hadi 6. Na kwa kila tukio la dukani hupiga story mbalimbali akisubiria tu fimbo yake ijae pesa na ishara ya fimbo hiyo kujaa pesa ni kuanguka maana kila ikijaa pesa huanguka na mzee huyo anatambua kuwa muda wa kuondoka umefika maana  chombo chake cha kuiba kichawi kimejaa. Katika fimbo hiyo ameweka majini ambayo ndio hufanya kazi hiyo ya kuiba pesa dukani na kwa sababu fimbo hiyo ina shimo ndani yake majini husokota zile pesa hadi zinajaa na zikijaa tu ilie fimbo inaanguka na mzee huyo anachua fimbo yake na kuondoka kwenda nyumbani kutoa na baadae anaende duka jingine kuendelea na wizi wake.  Kuna ndugu mmoja aliyeokoka alihamia katika mji huo na kufungua duka na ikawa ndio chanzo cha yule mzee kujulikana na kueleza ukweli na baada ya kueleza ukweli yule mzee akahama huo mji na kwenda kijijini.Yule ndugu baada ya kufungua duka mambo yalikua magumu sana pesa haikujulikana inakoenda, siku moja aliamua kuwashirikisha waumini wenzake kanisani na baada ya maombi yule mzee alikuja dukani na akaiweka fimbo yake kama alivyozoea lakini siku hiyo aliumbuka baada ya muuza duka kusikia kelele zikitoka kwenye fimbo ambapo mapepo kwenye fimbo kana kwamba mtu mwenye mapepo anaombewa, na mapepo hayo yalikua yanasema kwamba kuna moto dukani hivyo yanaungua, pale pale yule mzee sijui alikua na connection mapepo yale maana alidondoka na baadae kidogo baada ya kuombewa yeye mwenyewe alianza kusema yote aliyokua anayafanya kwa miaka mingi.
MUNGU akubariki ndugu unayesoma habari hii na kama unasumbuliwa na nguvu za giza katika biashara yako nakuomba uende kanisani ukaombewe na hao akina chuma ulete hawatafanikiwa kwako siku zote. Na pia kama ukiamua kujitenga na shetani kwa kumpa YESU
KRISTO maisha yako hakika utakua umejitenga na uonezi wowote wa shetani.
MUNGU akubariki sana.

Comments