UMUHIMU WA KIJANA KUWEPO KANISANI







JEREMIA 1: 4 – 10



Ø Ulishawahi kujiuliza ulizaliwa kwa kusudi gani?

Ø Ujana ni zawadi kutoka kwa Mungu.



Ø Mungu anajua umuhimu wa Kijana na shetani anajua umuhimu wake pia.



Ø Ili kuleta mafanikio na matokeo ya haraka Kijana ana uwezo mkubwa sana.



Ø Ni silaha nyepesi mno na hatari sana.



Ø Mungu anamtuma Yesu katika umri wa ujana na matokeo yake ni makubwa sana.





UMUHIMU WA KIJANA KATIKA JAMII:



a.      Kutatua tatizo ndani ya jamii (1Samw, 17: 31-33, 46-51)

b.     Kurudisha matumaini (Esta, 4: 12-16, 7: 1-10

c.      Kurekebisha hali ya mambo (Mwanzo 41: 34 – 44)

d.     Kurudisha heshima iliyopotea katika jamii.





UMUHIMU WA KIJANA KANISANI (Math, 1: 18 – 21)



a.      Kujishughulisha na mambo ya Kanisani kwake, kuwaza jinsi kutakavyopendeza.



b.     Kujishughulisha na Baba yake wa Kiroho (Mchungaji) 2Tim, 1: 2 – 4.



c.      Kuomba juu ya Kanisa / kufundisha / kuwaleta watu kwa Yesu.



d.     Kuwa mkarimu Kanisani na nyumbani, Mf, Rebeka,Mariamu, Mwanzo 24: 13 -26.



e.      Kujitolea kifedha,Kiakili ,Muda (Mf, Dorkasi, Warumi 12: 1)

v Kanisa lenye nguvu ni lile Vijana wao wanajitambua.



v Kanisa lenye matokeo mazuri linatokana na Familia zinazolijenga Kanisa.

v Kijana akikosa mwelekeo anaharibu mwelekeo mzima wa Kanisa.

v Vijana wachache tu wanaweza kuleta mabadiliko makubwa sana Mf, Vijana watatu (3) Shedraki, Meshaki na Abednego (Danieli 3: 16 – 19 mst 28 -30.



v Kijana aliyebadilika moyoni mmoja tu anaweza kuleta mabadiliko makubwa sana, Mf, Danieli 6: 24 – 28.



v Alionyesha Mungu wake na Mfalme na jamii yote ikamwinamia Mungu wake.



v Biblia inasema mtu asiudharau ujana wako, 1Tim, 4: 12.



v Kijana asipojitambua na kuwajibika atadharauliwa tu kama hakuna kitu umekifanya Kanisani kwako kinachoonekana.



v Una ulichokifanya kwa Baba yako wa Kiroho? (Mchungaji).



v Una ulichokifanya katika jamii ya kwenu?.



v Penda kijana ukiwepo mahali uwepo kwa faida, usiwe hasara bali uwe faida.



v Huwezi kuheshimiwa kama hakuna kitu unachomfaidisha nacho Mungu.



v Kijana Joshua alikabidhiwa jukumu la kuwaingiza watu Kanaani kwani alikuwa Kijana aliyejituma, aliye tayari anayepatikana, (Hesabu, 27: 18, Kutoka, 17: 8 – 10).

MUNGU awabariki sana

By Bishop YONA   P  SOLA LEMA
Kanisa la SAFINA VICTORY PENTECOSTAL
Ungalimited, Arusha
0754049163.
karibu kwa maombezi na ushauri wa kibiblia.
 

Comments