![]() |
Na Mwl. Christopher Mwakasege |
I Wakorintho 14:12. Inasema ‘vivyo
hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za rohoni,
takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa. Mungu hafanyi kitu
bila kusudi, na kusudi la semina hii ni:-
Kuna jambo Mungu anataka kufundisha
katikati yetu ambalo litahusisha sana utendaji wa karama za Roho Mtakatifu.
Kurahisisha ujenzi wa kanisa
lake na kazi zake. Mfano, kuna urahisi wa kujenga kwa kutumia mashine za kujengea
na kubeba matofali kuliko kutumia mkono, ni sawa na kufanya kazi ya Mungu kwa
kutumia karama za Roho Mtakatifu.
I Wakorintho 12:4; anasema pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule. Karama si za mtu ni za Roho Mtakatifu na kazi yake ni kulijenga kanisa.
I Wakorintho 12:4; anasema pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule. Karama si za mtu ni za Roho Mtakatifu na kazi yake ni kulijenga kanisa.
Yesu alisema katika kitabu cha Mathayo
16:18; ”nitalijenga kanisa langu wala milango ya kuzimu haitaliweza”. Karama
zinatokea mahali kama apendavyo Roho. Katika kitabu cha Yohana 14:16, Yesu
alizungumza habari za kutuletea msaidizi mwingine, yaani Roho atakapokuja
atachukua nafasi ya Yesu katika kulijenga kanisa lake.
Roho Mtakatifu sio karama bali anazo karama, pia Roho Mtakatifu sio nguvu bali anazo nguvu. Tunda la Roho linapofunuliwa ndani ya mtu tabia ya Mungu hujitokeza kwake.
Roho Mtakatifu sio karama bali anazo karama, pia Roho Mtakatifu sio nguvu bali anazo nguvu. Tunda la Roho linapofunuliwa ndani ya mtu tabia ya Mungu hujitokeza kwake.
Katika kutafuta vitu vya Mungu, ili
kufahamu karama za Roho Mtakatifu na kazi zake, kuna gharama. Mfano, kwenye
ndege kuna first class, business class na third class. Ukitaka kupata huduma
nzuri zaidi lazima uongeze pesa (gharama) ili upande business class au first
class. Lakini dereva wa ndege (captain) ni yule yule. Vivyo hivyo katika
maswala ya Mungu wako wanaokaa first, business au third class, lakini wote
tunakwenda mbinguni. Hivyo tunahitaji kuingia gharama ili tukae first class
ndani ya Yesu. Gharama hizo ni kama:-
i) kusoma neno la Mungu kwa bidii kwa kadri inavyowezekana ili neno hilo likae ndani yako kwa wingi, maan kujua karama za Roho Mtakatifu bila kuwa an maneno ya Mungu ni vigumu.
ii) Maombi n.k.
i) kusoma neno la Mungu kwa bidii kwa kadri inavyowezekana ili neno hilo likae ndani yako kwa wingi, maan kujua karama za Roho Mtakatifu bila kuwa an maneno ya Mungu ni vigumu.
ii) Maombi n.k.
I Wakorintho 12:1 inasema ‘basi ndugu
zangu kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu’. Tunahitaji kuwa na
hamu ya kuona kwamba karama za Roho Mtakatifu zinafanya kazi na zinafahamika.
Hamu hiyo imepotea katika kanisa la Mungu na hivyo kufanya kazi ya ujenzi wa
kanisa la Mungu kutofanyika kama Mungu anavyokusudia.
I Wakorintho 14:12; ”Vivyo hivyo na
ninyi kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba
mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa”.
UTENDAJI KAZI WA KARAMA.
Mambo muhimu (ya msingi) kufahamu ili karama ziweze kufanya kazi. Mambo hayo ni:-
1.) Kubali kuwa karama za Roho zinaweza kufanya kazi kwako pia.
Mambo muhimu (ya msingi) kufahamu ili karama ziweze kufanya kazi. Mambo hayo ni:-
1.) Kubali kuwa karama za Roho zinaweza kufanya kazi kwako pia.
I Wakorintho 12:4.11; ”Basi pana
tofauti za karama bali Roho ni yeye yule, lakini kazi hizi zote huzitenda Roho
huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye”. Roho
Mtakatifu ndani ya mtu anazo karama zote bali anamgawia kila mtu kama apendavyo
yeye. Rumi 12:3-6; inasema ”kwa maana kwa neema niliyopewa na mwambia kila mtu
aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyo mpasa kunia ……….., basi kwa kuwa tuna
karama zilizo mbalimbali …………..”.
2.) Uwe na hamu (haja) kubwa ya msaada
wa Mungu.
I Wakorintho:1,12; ”ufuateni upendo na
kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu, vivyo hivyo
na ninyi kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba
mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa”.
Angalizo: karama siku zote zina mvuto.
Angalizo: karama siku zote zina mvuto.
3.) Tembea katika wito (nafasi) yako.
Warumi 12:6, ”……… kwa kadri ya neema
tuliyopewa…”, yaani wito (kiwango) ulichopewa. Ndani ya wito kuwa nafasi ambayo
Mungu amekupa. Kuna ngazi, kuna mahali na muda unaotakiwa kuufanyia huo wito.
Galatia 2:6-7 ”……walipokwisha kujua neema niliyopewa…….. walinipa mimi mkono wa
kuume wa shirika”.
Mfano: kuna tofauti ya karama ya unabii na huduma ya unabii, yaani kila mtu aliyeokoka anaweza kutoa unabii bali si kila mtu ana karama ya unabii.
Mfano: kuna tofauti ya karama ya unabii na huduma ya unabii, yaani kila mtu aliyeokoka anaweza kutoa unabii bali si kila mtu ana karama ya unabii.
4.) Karama kutenda kazi vizuri ndani
ya mtu inategemea kiwango cha Imani alichonacho.
Rumi 12:6; ”basi kwa kuwa tuna karama
zilizo mbalimbali …….. ikiwa unabii tutoe unabii kwa kadri ya imani”. Sio zaidi
ya hapo. Rumi 10:17; ”imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la
kristo” yaani kiwango cha imani ulichonacho hakiwezi kuzidi hapo. Imani huja tu
kwa neno la Kristo. Biblia haituruhusu kutembea kwenye karama zaidi ya imani tuliyo
nayo.
Angalizo: kufahamu neno la Kristo kwa wingi ni muhimu. Tembea katika karama za roho kwa kadri ya imani.
Angalizo: kufahamu neno la Kristo kwa wingi ni muhimu. Tembea katika karama za roho kwa kadri ya imani.
Karama zitumike kwa kadri ya Imani
yaani utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu ndani ya mtu utategemea kiwango
cha neno la kristo kilichoko ndani yake. Hii ni kwa sababu Mungu alikusudia
kuwa karama katikati ya kanisa zifanye kazi kwa ufanisi na usalama ili
kulijenga kanisa.
Mfano: Mungu hakuweka unabii ili uongoze kanisa; ila ni kwa ajili ya kuthibitisha neno ambalo Mungu amekwisha kulisema ndani ya mtu.
Kwa sababu karama si zako ni za Roho Mtakatifu, kama huna neno la kutosha ndani yako karama inaweza ikaletwa ndani yako ukaikataa.
Mfano: Mungu hakuweka unabii ili uongoze kanisa; ila ni kwa ajili ya kuthibitisha neno ambalo Mungu amekwisha kulisema ndani ya mtu.
Kwa sababu karama si zako ni za Roho Mtakatifu, kama huna neno la kutosha ndani yako karama inaweza ikaletwa ndani yako ukaikataa.
I Wakorintho 12:8 ”maana mtu mmoja kwa
Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa apendavyo Roho yeye
yule”. I Petro 4:10; ”kila mmoja kwa kadri alivyoipokea karama, itumieni kwa
kuhudumiana….”. Kuna kupewa na kupokea- karama. Unaweza kukataa kwa kutokuja au
hofu n.k.
5.) Jifunze jinsi Roho anavyowasiliana
na roho yako, nafsi yako na mwili wako.
I Wakorintho 3:16; ”hamjui ya kuwa
ninyi mmekuwa hekalu la Mungu na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?” Mtu
ni roho anayo nafsi na anaishi katika mwili. Roho Mtakatifu pia yuko ndani ya
mwili. Hesabu 30:2 ”Mtu atakapo mwekea Bwana nadhiri, ……. Asitangue neno lake;
atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake”. Unaposema maneno
yanafunga nafsi yako.
Mwili unatawaliwa na nafsi, nafsi kazi
yake ni kutafsiri kile ambacho mwili unasema ili roho ielewe na kile ambacho
roho inasema ili mwili uelewe. Kwa hiyo nafsi inasaidiwa pale, unaposoma neno
ili iweze kutafsiri mambo ya rohoni sawasawa na neno. Marko 2:5-8, ”naye Yesu,
alipoiona imani yao, …….. wakifikiri mioyoni mwao ….. Yesu akafahamu rohoni
mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao …..”. Galatia 6:17; ”tangu sasa mtu
asinitaabishe kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.
6.) Ujazo wa Roho
Mtakatifu. Sio wa siku moja ambao unatosheleza.
I Petro 4:9-11 ”mkaribishane ninyi kwa
ninyi, pasipo kunung’unika, kila mmoja kwa kadri alivyoipokea karama,……….. mtu
akihudumu na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu, …….”. yaani kila wakati
kuna nguvu fresh, mtu asihudumu kwa nguvu alizojaliwa bali anazojaliwa kila
wakati na Mungu. Hivyo tunahitaji kurudi kwa Mungu kila wakati kujazwa nguvu za
Roho Mtakatifu.
Kuna kiwango cha nguvu za Roho Mtakatifu ndani ya mtu ambacho hakiwezi (kwa kuwa ni kidogo) kusukuma karama fulani ili ziweze kuhudumu au kufanya kazi; ndio maana tunahitaji kujazwa kila wakati.
Kuna kiwango cha nguvu za Roho Mtakatifu ndani ya mtu ambacho hakiwezi (kwa kuwa ni kidogo) kusukuma karama fulani ili ziweze kuhudumu au kufanya kazi; ndio maana tunahitaji kujazwa kila wakati.
Usikose
Sehemu ya Muendelezo wa Somo hili Siku ya Kesho.
Comments