DONDOO ZA DARASA LA UONGOZI – SEHEMU YA TATU MADHAIFU/ MAPUNGUFU YA SANGWINI (WEAKNESSES OF SANGUINE)

DONDOO ZA DARASA LA UONGOZI – SEHEMU YA TATU
MADHAIFU/ MAPUNGUFU YA SANGWINI (WEAKNESSES OF SANGUINE)

1. Kukosa Nidhamu Ambako Kunadhihirika kwa Njia Nyingi.
Moja wapo ya madhaifu ya Sangwini ni kukusa nidhamu ya kutosha katika mambo mbali mbali. Kama ni masomo Sangwini sio mpenzi wa kusoma sana na kujisimamia mwenyewe. Mwalimu akitoka na yeye anatoka. Kama ni mashureni wanao ongoza kwa kupiga kelele darasani ni Sangwini. Mitaani/ makazini na kwinginepo, wanaoongoza kwa uchokozi na vurugu ni Sangwini. Huwa na nidhamu ya chini katika mambo mbali mbali.

2. Ni watu wa “Milipuko” Hii kwa Kawaida Huisha kwa Haraka kama Ambavyo Huanza.
Sangwini ni watu wa milipuko. Anaweza akalipuka kufanya jambo kwa nguvu sana lakini huwa na nguvu ndogo sana ya kuliendeleza jambo hilo. Mara baada ya muda kidogo tu huishiwa nguvu za kuendeleza hilo jambo alilolianzisha na mara moja huliacha na kushika kitu kingine. Sangwini ni kundi linaloongoza kwa kuchumbia chumbia mara kwa mara na kuacha au kuvunja uchumba bila hata sababu zinazoeleweka. Wanachumbia hawaoi, wanaanzisha hawamalizi. Wanaanzasha baishara kabla hata haijakomaa wamesha acha. Wanaanzisha makanisa kabla hata hayaja komaa wanaacha na kuanzisha mengine au kitu kingine.

3. Kukosa utulivu wa ki-akili. Mawazo ya Sangwini, hayajatulia. (not concetrated).
Mawazo ya Sangwini yametawanyika. Sangwini anatatizo la kuelekeza mawazo yake kwenye jambo moja (concetration) “They are not focused” Hii huwasababisha kuwa na uwezo mdogo wa kushika mambo mazito ambayo yanahitaji “concetration” Mara nyingi ndio kundi linalo ongoza kwa kubamizwa na masomo. Wanafunzi walio wengi wa kundi hili hawafanyi vizuri sana katika masomo yao. 

4. Si wepesi Kustahimili Mambo Magumu au Shuluba.
Sangwini hapendi maisha ya shida, anapenda maisha rahisi na mteremko yasiyo hitaji kumghalimu sana. Hupenda kazi rahisi rahisi, yasiyomfanya atoke jasho sana au aumie sana. 
Sangwini anapenda kuchumia kivulini na kulia kivulini.
Sangwini wengi mashuleni wanachagua masomo yaliyo rahisi na yasiyo “complicated” nimefuatilia nikagundua ni marachache sana tena kwa uchache kumkuta Sangwini anapenda hesabu. Kama atapata nafasi ya kuchagua masomo waliowengi wasingechagua masoma magumu kama hesabu n.k.

5. Wanaahidi ahadi nyingi ambazo hawatakuja kamwe kuzitimiza.
Sangwini ni hodari sana wa kutamka na kuahidi mabo makubwa makubwa na kwa mikwara mingi. Tatizo lake Sangwini linakuja kwenye kutimiza hizo ahadi walizo ahidi. Madaftari mengi makanisani makazini na kwinginepo yamejaa ahadi za Sangwini ambaye yeye mwenyewe tayari Alisha sahau siku nyingi kama anadaiwa na mbaya zaidi hana mpango wa kutekeleza kile alichokiahidi.

6. Ni wazuri kwa kukopa na mara nyingi huwa hawalipi madeni yao.
Kwanza lazima ufahamu kuwa Sangwini wana ujuzi mzuri wa kuongea na kumshawishi mtu kuingia “line” katika jambo fulani. Wanapokuja kukupa wanakuja la lugha laini na tamu sana na wakati mwingine kukuahidi jinsi ambavyo hata wewe utanufaika na na kufurahia matunda ya kumkopesa yeye hicho kiasi cha pesa na kukuahidi kuwa hata kabla ya ile tarehe ya kurejesha atakuwa amesha rejesha kila kitu. Mambo huwa tofauti sana na makubaliano. Walio wengi wakikopa ni wagumu sana wa kulipa madeni. Huko magengeni wanakopa, madukani wanakopa na kwenye maeneo mbali mbali wanakopa na hawalipi na hiyo kusababisha mnigogoro na magombano katika jamii. Sangwini hajali usumbufu wa kudaiwa. Akilini mwake deni sio miongoni mwa vitu vinavyomsumbua kama ambavyo ingekuwa kwa kundi kama Fregmatiki akidaiwa anaweza hata asipate usingizi kwajili ya deni. Sangwini anaweza akawa anadaiwa madeni makubwa tena na kundi la watu wengi hiyo haitamuondolea usingizi atalala tena kama hajaset alam anaweza hata kupitiliza masaa ya kulala.
Unapomkopesha Sangwini kuna mawili ulipwe au usilipwe.

Sangwini kiboko yake ni Sangwini mwenzake. Ukitaka kufurafia mechi ni pale Sangwini kamkopesha Sangwini mwenzake na hataki kulipa. Hapo ndi po huwa nyasi zinawaka moto. Mwishowe huishia kupelekana kwenye vyombo vya sheria na mwishowe kulipana kiduchu kiduchu kwa muda mrefu mpaka mdai anaamua kusamehe na kusahau.

7. Uwezo wao wa Kufikiri Upo Chini.
Uwezo wao wa kufikiri upo chini pia hawana uwezo wa kufikiri kwa undani. Mara nyingi hutegemea kichwa cha mtu mwingine kupata majibu ya maswali yao. Sangwini hapendi kuushughulisha ubongo wake hata kwa vitu vidogo tu. Hesabu ndogo tu ya gengeni hawezi kupiga mwenyewe mpaka atafute caluculator ndio apige mahesabu. Sangwini hawezi hata kujua au kukumbuka tarehe ya leo. Utasikia mara nyingi Sangwini anauliza, “hivi leo juma ngapi? Au leo tarehe ngapi, au hivi huu ni mwaka gani? Juma moja lina siku saba tu lakini Sangwini siku hizo saba zinamshinda kufikiri na kuchambua na kupata jibu kuwa leo ni siku gani mpaka atafute jebu kutoka kwenye kichwa cha mtu mwingine. Tarehe zipo 30 lakini Sangwini hawezi kujua leo ni tarehe ngapi mpaka atumiye ubongo wa mtu mwingine. Huwa najiuliza kama tahehe zingekuwa 366 kwa mwezi mmoja maisha ya Sangwini yangekuwaje?

8. Sio wazuri kuwa viongozi wa juu au kushika nyadhifa za juu kabisa.
Sangwini sio wazuri wa kupewa uongozi wa juu kabisa. Sangwini akiwa ndiye kiongozi wa juu kabisa lazima kanisa au shirika au taasisi itayumba na utatarajia migogoro na marumbano na magomvi ya kila mara katika kanisa, shirika au taasisi. Sangwini anapaswa afanye kazi chini ya mamlaka nyingine asiwe yeye ndiye “top” Sio wazuru wa kuwa viongozi wa juu kabisa kwasababu Sangwini wanatatizo katika swala zima la maamuzi. (Decision making) Maafuzi ya Sangwini mara nyingi huwa sio ya kina mara nyingi huwa yanatokana na “emotion” baada ya muda akitulia vizuri anagundua kuwa hakuwa ameamua vizuri na tayari utekelezaje wa maamuzi hayo unakuwa umeshafika mbali mahali ambapo hawawezi tena kurudi nyuma. Sangwini akishika nafasi ya juu kabisa atakuwa ni kiongozi mwenye maneno mengi na ahadi nyingi lakini utekelezaji wa hali ya chini. Kwahiyo mnapofanya uchaguzi mbalimbali zingatia kama nafasi ya juu kabisa ile ya “final say” isiende kwa Sangwini hata kama ndio wengi wanamtaka huenda ni ushabiki tu akiingia madarakani mtajuta kwanini mlimchagua.

9. Hawapendi Kuchulkuliwa Hatua za Kinidhamu Pale Wanapokuwa Wamekiuka Taratibu. 
Sangwini anatatizo katika swala zima la nidhamu. Hapendi kuchukuliwa hatua za kinidhamu hata kama atakuwa amekosea kabisa. Utakapoanza tu kumuonya basi atakasirika sana kwa hayo maonyo. Wengine watazila kula au watazira kufanya jambo fulani kisa nini ulimsema au kumuonya kwa kosa fulani. Wanataka hata wakikosea wasiambiwe ukweli kama wamekosea. Sangwini akionywa au kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa makosa yake anaweza akalia sana na kulalamika kila mahali kanakwamba ameonewa kwa kiasi cha hali ya juu sana. Wakati mwingine akichukuliwa hatua kwa makosa yake au kuonywa wakati mwingine huamua hata kujiua kutokana na kuchukuliwa hatua za kinidhamu. Huu ni udhaifu mkubwa alio nao Sangwini. Ni mtu mwenye hasira sana tena wakati mwingine hasira zilizopitiliza.

10. Sio Wazuri Kushika Nafasi za juu za Uongozi.
Sangwini anahitaji kuwa chini ya mamlaka nyingine. Sio wazuri kushika nafasi za juu kabisa katika uongozi. Kama Sangwini akiwa ndiye kiongozi wa juu kabisa yaani “top leader” huenda kanisa au kampuni au taasisi isiwe katika hali nzuri. Wanatatizo kubwa katika eneo la “decision making” maamuzi yao huwa sio ya kina wanaamua kabla hawajachambua na kufikiri kwa kina na baadae wanapokuja kukutana na ukweli na uhalisia inakuwa ni “too late” maamuzi yalisha fanyika na hatua za utekelezaji zilishaanza kutendeka. Sangwini akiwa the “top leader” mwenye “final say” basi utatarajia migogoro, magomvi na hali ya kutoelewana katika shirika au taasisi. Nivizuri tunapochagua viongozi kulizingatia hili.

Niandikie kile kilicho kugusa katika somo hili.
Na Mchungaji na Mwl Peter Mitimingi


1. Kukosa Nidhamu Ambako Kunadhihirika kwa Njia Nyingi.
Moja wapo ya madhaifu ya Sangwini ni kukusa nidhamu ya kutosha katika mambo mbali mbali. Kama ni masomo Sangwini sio mpenzi wa kusoma sana na kujisimamia mwenyewe. Mwalimu akitoka na yeye anatoka. Kama ni mashureni wanao ongoza kwa kupiga kelele darasani ni Sangwini. Mitaani/ makazini na kwinginepo, wanaoongoza kwa uchokozi na vurugu ni Sangwini. Huwa na nidhamu ya chini katika mambo mbali mbali.

2. Ni watu wa “Milipuko” Hii kwa Kawaida Huisha kwa Haraka kama Ambavyo Huanza.
Sangwini ni watu wa milipuko. Anaweza akalipuka kufanya jambo kwa nguvu sana lakini huwa na nguvu ndogo sana ya kuliendeleza jambo hilo. Mara baada ya muda kidogo tu huishiwa nguvu za kuendeleza hilo jambo alilolianzisha na mara moja huliacha na kushika kitu kingine. Sangwini ni kundi linaloongoza kwa kuchumbia chumbia mara kwa mara na kuacha au kuvunja uchumba bila hata sababu zinazoeleweka. Wanachumbia hawaoi, wanaanzisha hawamalizi. Wanaanzasha baishara kabla hata haijakomaa wamesha acha. Wanaanzisha makanisa kabla hata hayaja komaa wanaacha na kuanzisha mengine au kitu kingine.

3. Kukosa utulivu wa ki-akili. Mawazo ya Sangwini, hayajatulia. (not concetrated).
Mawazo ya Sangwini yametawanyika. Sangwini anatatizo la kuelekeza mawazo yake kwenye jambo moja (concetration) “They are not focused” Hii huwasababisha kuwa na uwezo mdogo wa kushika mambo mazito ambayo yanahitaji “concetration” Mara nyingi ndio kundi linalo ongoza kwa kubamizwa na masomo. Wanafunzi walio wengi wa kundi hili hawafanyi vizuri sana katika masomo yao.

4. Si wepesi Kustahimili Mambo Magumu au Shuluba.
Sangwini hapendi maisha ya shida, anapenda maisha rahisi na mteremko yasiyo hitaji kumghalimu sana. Hupenda kazi rahisi rahisi, yasiyomfanya atoke jasho sana au aumie sana.
Sangwini anapenda kuchumia kivulini na kulia kivulini.
Sangwini wengi mashuleni wanachagua masomo yaliyo rahisi na yasiyo “complicated” nimefuatilia nikagundua ni marachache sana tena kwa uchache kumkuta Sangwini anapenda hesabu. Kama atapata nafasi ya kuchagua masomo waliowengi wasingechagua masoma magumu kama hesabu n.k.

5. Wanaahidi ahadi nyingi ambazo hawatakuja kamwe kuzitimiza.
Sangwini ni hodari sana wa kutamka na kuahidi mabo makubwa makubwa na kwa mikwara mingi. Tatizo lake Sangwini linakuja kwenye kutimiza hizo ahadi walizo ahidi. Madaftari mengi makanisani makazini na kwinginepo yamejaa ahadi za Sangwini ambaye yeye mwenyewe tayari Alisha sahau siku nyingi kama anadaiwa na mbaya zaidi hana mpango wa kutekeleza kile alichokiahidi.

6. Ni wazuri kwa kukopa na mara nyingi huwa hawalipi madeni yao.
Kwanza lazima ufahamu kuwa Sangwini wana ujuzi mzuri wa kuongea na kumshawishi mtu kuingia “line” katika jambo fulani. Wanapokuja kukupa wanakuja la lugha laini na tamu sana na wakati mwingine kukuahidi jinsi ambavyo hata wewe utanufaika na na kufurahia matunda ya kumkopesa yeye hicho kiasi cha pesa na kukuahidi kuwa hata kabla ya ile tarehe ya kurejesha atakuwa amesha rejesha kila kitu. Mambo huwa tofauti sana na makubaliano. Walio wengi wakikopa ni wagumu sana wa kulipa madeni. Huko magengeni wanakopa, madukani wanakopa na kwenye maeneo mbali mbali wanakopa na hawalipi na hiyo kusababisha mnigogoro na magombano katika jamii. Sangwini hajali usumbufu wa kudaiwa. Akilini mwake deni sio miongoni mwa vitu vinavyomsumbua kama ambavyo ingekuwa kwa kundi kama Fregmatiki akidaiwa anaweza hata asipate usingizi kwajili ya deni. Sangwini anaweza akawa anadaiwa madeni makubwa tena na kundi la watu wengi hiyo haitamuondolea usingizi atalala tena kama hajaset alam anaweza hata kupitiliza masaa ya kulala.
Unapomkopesha Sangwini kuna mawili ulipwe au usilipwe.

Sangwini kiboko yake ni Sangwini mwenzake. Ukitaka kufurafia mechi ni pale Sangwini kamkopesha Sangwini mwenzake na hataki kulipa. Hapo ndi po huwa nyasi zinawaka moto. Mwishowe huishia kupelekana kwenye vyombo vya sheria na mwishowe kulipana kiduchu kiduchu kwa muda mrefu mpaka mdai anaamua kusamehe na kusahau.

7. Uwezo wao wa Kufikiri Upo Chini.
Uwezo wao wa kufikiri upo chini pia hawana uwezo wa kufikiri kwa undani. Mara nyingi hutegemea kichwa cha mtu mwingine kupata majibu ya maswali yao. Sangwini hapendi kuushughulisha ubongo wake hata kwa vitu vidogo tu. Hesabu ndogo tu ya gengeni hawezi kupiga mwenyewe mpaka atafute caluculator ndio apige mahesabu. Sangwini hawezi hata kujua au kukumbuka tarehe ya leo. Utasikia mara nyingi Sangwini anauliza, “hivi leo juma ngapi? Au leo tarehe ngapi, au hivi huu ni mwaka gani? Juma moja lina siku saba tu lakini Sangwini siku hizo saba zinamshinda kufikiri na kuchambua na kupata jibu kuwa leo ni siku gani mpaka atafute jebu kutoka kwenye kichwa cha mtu mwingine. Tarehe zipo 30 lakini Sangwini hawezi kujua leo ni tarehe ngapi mpaka atumiye ubongo wa mtu mwingine. Huwa najiuliza kama tahehe zingekuwa 366 kwa mwezi mmoja maisha ya Sangwini yangekuwaje?

8. Sio wazuri kuwa viongozi wa juu au kushika nyadhifa za juu kabisa.
Sangwini sio wazuri wa kupewa uongozi wa juu kabisa. Sangwini akiwa ndiye kiongozi wa juu kabisa lazima kanisa au shirika au taasisi itayumba na utatarajia migogoro na marumbano na magomvi ya kila mara katika kanisa, shirika au taasisi. Sangwini anapaswa afanye kazi chini ya mamlaka nyingine asiwe yeye ndiye “top” Sio wazuru wa kuwa viongozi wa juu kabisa kwasababu Sangwini wanatatizo katika swala zima la maamuzi. (Decision making) Maafuzi ya Sangwini mara nyingi huwa sio ya kina mara nyingi huwa yanatokana na “emotion” baada ya muda akitulia vizuri anagundua kuwa hakuwa ameamua vizuri na tayari utekelezaje wa maamuzi hayo unakuwa umeshafika mbali mahali ambapo hawawezi tena kurudi nyuma. Sangwini akishika nafasi ya juu kabisa atakuwa ni kiongozi mwenye maneno mengi na ahadi nyingi lakini utekelezaji wa hali ya chini. Kwahiyo mnapofanya uchaguzi mbalimbali zingatia kama nafasi ya juu kabisa ile ya “final say” isiende kwa Sangwini hata kama ndio wengi wanamtaka huenda ni ushabiki tu akiingia madarakani mtajuta kwanini mlimchagua.

9. Hawapendi Kuchulkuliwa Hatua za Kinidhamu Pale Wanapokuwa Wamekiuka Taratibu.
Sangwini anatatizo katika swala zima la nidhamu. Hapendi kuchukuliwa hatua za kinidhamu hata kama atakuwa amekosea kabisa. Utakapoanza tu kumuonya basi atakasirika sana kwa hayo maonyo. Wengine watazila kula au watazira kufanya jambo fulani kisa nini ulimsema au kumuonya kwa kosa fulani. Wanataka hata wakikosea wasiambiwe ukweli kama wamekosea. Sangwini akionywa au kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa makosa yake anaweza akalia sana na kulalamika kila mahali kanakwamba ameonewa kwa kiasi cha hali ya juu sana. Wakati mwingine akichukuliwa hatua kwa makosa yake au kuonywa wakati mwingine huamua hata kujiua kutokana na kuchukuliwa hatua za kinidhamu. Huu ni udhaifu mkubwa alio nao Sangwini. Ni mtu mwenye hasira sana tena wakati mwingine hasira zilizopitiliza.

10. Sio Wazuri Kushika Nafasi za juu za Uongozi.
Sangwini anahitaji kuwa chini ya mamlaka nyingine. Sio wazuri kushika nafasi za juu kabisa katika uongozi. Kama Sangwini akiwa ndiye kiongozi wa juu kabisa yaani “top leader” huenda kanisa au kampuni au taasisi isiwe katika hali nzuri. Wanatatizo kubwa katika eneo la “decision making” maamuzi yao huwa sio ya kina wanaamua kabla hawajachambua na kufikiri kwa kina na baadae wanapokuja kukutana na ukweli na uhalisia inakuwa ni “too late” maamuzi yalisha fanyika na hatua za utekelezaji zilishaanza kutendeka. Sangwini akiwa the “top leader” mwenye “final say” basi utatarajia migogoro, magomvi na hali ya kutoelewana katika shirika au taasisi. Nivizuri tunapochagua viongozi kulizingatia hili.

Niandikie kile kilicho kugusa katika somo hili.

Comments