Hii ndio Safari ya Mwisho ya Askofu Dr. Mosses Kulola hapa duniani


Mwili wa Marehemu ukiingizwa Kaburini
Leo ndo ilikuwa ndiyo siku ya Mwisho ya safari ya Askofu Dr. Mosses Kulola, safari iliyohitimishwa kwa Mwili wake kupumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu likiwa Kaburini
Mazishi yake yamefanyika katika Kanisa la EAGT Bugando na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Makanisa mbaimbali akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.
Mh. Jakaya Mrisho Kikwete
Viongozi wengine waliokuwepo ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Engeneer Evarist Ndikilo, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa, Katibu Mkuu wa CHADEMA Wilbroad Slaa, Mbunge wa Nyamagana(CHADEMA) Ezekiel Wenje.
Edward Lowasa akiweka shada la maua katika Kaburi la Marehemu
Pia Waimbaji mbalimbali wa Nyimbo za Injili Tanzania walikuwepo kuhakikisha kuwa zoezi zima linaambatana na Nyimbo mbalimbali za kumuenzi Baba/Babu yetu Askofu Dr. Mosses Kulola.
Mh. Jakaya Mrisho Kikwete
Sasa naomba nikukumbushe Wasifu wa Marehemu Askofu Dr. Mosses Kulola uliosomwa Jana katika Uwanja wa CCM Kirumba wakati wa kutoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu.

Comments