Mwili wa Marehemu ukiingizwa Kaburini |
Leo ndo ilikuwa ndiyo siku ya Mwisho ya
safari ya Askofu Dr. Mosses Kulola, safari iliyohitimishwa kwa Mwili
wake kupumzishwa katika nyumba yake ya milele.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu likiwa Kaburini |
Mazishi yake yamefanyika katika Kanisa
la EAGT Bugando na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na
Makanisa mbaimbali akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano Mh. Jakaya Mrisho
Kikwete.
Mh. Jakaya Mrisho Kikwete |
Viongozi wengine waliokuwepo ni pamoja
na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Engeneer Evarist Ndikilo, Waziri Mkuu Mstaafu
Edward Lowasa, Katibu Mkuu wa CHADEMA Wilbroad Slaa, Mbunge wa
Nyamagana(CHADEMA) Ezekiel Wenje.
Edward Lowasa akiweka shada la maua katika Kaburi la Marehemu |
Pia Waimbaji mbalimbali wa Nyimbo za
Injili Tanzania walikuwepo kuhakikisha kuwa zoezi zima linaambatana na
Nyimbo mbalimbali za kumuenzi Baba/Babu yetu Askofu Dr. Mosses Kulola.
Mh. Jakaya Mrisho Kikwete |
Sasa naomba nikukumbushe Wasifu wa
Marehemu Askofu Dr. Mosses Kulola uliosomwa Jana katika Uwanja wa CCM
Kirumba wakati wa kutoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu.
Comments