Kwa wadada:SABABU ZINAZO SABABISHA WASICHANA WENGI KUTOPATA WANAUME WA KUWAOA


  • Watu wengi wanajiuliza kwanini wasichana wengi kuolewa imekua tabu? Research imefanyika kwa wasichana na vijana wa kiume na kupata majibu sahihi.Imegundulika kuwa matatizo wanasababisha wasichana wenyewe, na ndio chanzo cha wao kukosa waume wa kuwaoa. Soma hapa chini sababu za wanawake wengi kukosa wanaume wa kuwaoa kama ifuatavyo.....
     
     1. MARINGO – Nipale wakati binti anapokua nakujishtukia kuwa yeye ni mrembo wa ukweli, basi hapoa ataanza kujisikia kuwa yeye ni yeye kudharau wengine na kujiona babkubwa na kuwa too much selective, inapotoke kijana kampenda atakapomfata huwa anamuangalia nakumuona hana hadhi ya kuwa na yeye, itaendelea hivyoooooo mwisho atakuja kukutana na kijana mtanashati wa ukweli hapo ndio atajiaminia huyo ndio mwenye hadhi yake kumbe gubegube, mpaka aje kugundua kashaumizwa anaanza sasa kuumizwa kila mara hapo ataamua sasa kujishusha na kusarandia vijana wa kawaida, kila atakae date nae anakuta ni mchumba wa mtu au mume wa mtu au bf wa mtu, hapo ndio tayari keshakua majeruhi wa mapenzi basi itabidi aishie kuchuna mabuzi fumba na kufumbua yuko above 30 anaanza kulia nina mkosi ohh nuksi nk.
     
    2. UMALAYA – Ule wakati binti anaanza kuchanua badala ya kujitunza nakujiheshimu yeye ndio anatumia nafasi hiyo kuuchezea mwili wake kila mwanaume anayemtongoza anamkubali mwisho anajikuta ana maboyfriend zaidi ya mmoja, hapo anaanza kuangalia sasa maslahi na sio upendo wa dhati anajikuta kaingia kwenye wrong choice basi ataendelea kusakanyia mwengine na mwengine na mwengine ili akutane na right choice hapo kuna mabuzi kibao kuna waume za watu na vijana matapeli wote anabambana nao mwisho anashtukia yuko above 30 ana anza kulia ohh na mkosi sijui nuksi nk.

    3. MAJINI MAHABA – Baadhi ya wasichana wana majini mahaba kwahiyo kuolewa kwao imeshakua ni tabu anaweza apate mchumba afe au mwanaume abadilike tabia nakumchukia au mwanaume aanze kuwa Malaya na kushindwa kumvumilia hatimaye wanaachana mauzauza yanakuwa kibao kwenye mapenzi yake mwisho anajishtukia yuko above 30 anajiona ana mkosi na nuksi.(Lakini kwa maombezi kupitia jina la YESU KRISTO utafunguliwa kutoka kwenye roho hii ya shetani. kimbilia kanisani na utapona)

    4. MARAFIKI WABAYA – Msichana anaweza kuwa haolewi kumbe marafiki alionao sio wema kwake, ukipata mchumba tayari umeshaenda kumweleza shosti wako au mashosti zako, bila wewe kujua wanampeperusha, watakuzunguka ,watatembea nae, watamtega, watakuongelea vibaya, watakuloga, watamloga, watakuharibia mpaka utaachwa kila mara usipokua mjanja ukashtuka ndio hivyo uanajikuta uko abave 30 unaanza kulia ohh nina mkosi sijui nuksi nk. Mpaka hapo nina amini kwa wewe msichana ambaye huolewi kuna fungu lako moja kati ya hayo hapo juu, sasa chakufanya jitambue na ujipange upya kama ushapita above 30 usihofu sana hata miaka 60 wanaolewa bado. MUNGU awasaidie mabinti na kumbuka mme/ mke mwema anatoka kwa MUNGU. Hivyo maombi kwa ajili ya mke/mme lazima yafanyike mapema ili MUNGU amlete kwako yule ambaye madhaifu yako atayaona kama moja ya mambo mema zaidi kwako. MUNGU akupe macho ya rohoni ili uutambue ukuu wake. MUNGU awabariki na amani ya KRISTO YESU iamue mioyoni mwenu.

Comments