![]() |
Padre Ancelmo Mwang'amba baada ya kumwagiwa Tindikali |
Kwa mujibu wa kamanda wa Jeshi la Polisi mjini Magharibi, Mkaadanu
Hassan Mkaadanu, Padri huyo alipigiwa simu, na alipokuwa akitoka nje ili
kuisikiliza vema simu, hapo ndipo tukio likatokea, ambao haijajulikana
kama ni mtu au kundi la watu lililofanya tukio hilo.
Taarifa za hivi sasa zinaeleza kuwa Padri Mwan'gata amelazwa Hospitali
kuu ya Mnazi Mmoja, wodi ya Mapinduzi mpya, ambayo ni wodi maalum kwa
ajili ya viongozi.
Gospel Kitaa imeelezwa kuwa Padri huyo amefanya kazi kwa muda wa zaidi
ya miaka 35 huko Zanzibar, ambapo baada ya taarifa hizi kupatikana,
askofu mkuu wa kanisa katoliki Zanzibar, Agustino Shao ameelezwa
kujifungia kuanzia muda huo na kuendelea kuwepo hadi muda huu ambapo
ripota wa WAPO Radio FM, ameeleza.
Kwa hivi sasa taharuki ni kila mahali, hakuna kinachoeleweka, wakristo
wakieleza kuwa hawana pa kukimbilia kwa kuwa ni zaidi ya miezi minne
kupita tangu padri Evarist Mushi auwawe kwa risasi, na bado mwenendo wa kesi haueleweki, na kwamba sasa hawajui pa kwenda. (tazama picha za maazishi yake)
Kamanda Mkaadamu amekiri kuwa tindikali ni tatizo, na amesema kuwa wanaendelea kufanya jitihada ili kila kitu kiwe wazi.
-Gospel Kitaa-
-Gospel Kitaa-
Padri Joseph Magamba akiwa wodini akipatiwa matibabu |
Comments