WAKATI UFAAO KUANDAA SILAHA YAKO.


   Silaha hutengenezwa wakati wa
amani,wakati wa vita ndipo
hutumika....."WAKRISTO wengi wakati wa
amani hawaombi,ila mambo yakigeuka
kidogo hufunga na kuomba,Wakati wa
kuzama si wakati wa kujifunza kuogelea bali
ulipaswa kujifunza kabla,fanya maazimio ya
kumtafuta MUNGU wako siku za amani na
simama kwenye zamu yako
kikamilifu,Mtafute Mungu wako kwa Bidii...
Mithali 8:17
Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Andaa na uvae silaha
sasa,
Luka 21:34-36.
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima. Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.
"BWANA MUNGU AWABARIKI NA KUWAPA NGUVU ILI KUWEZA KUANDAA SILAHA "
By CONRAD CONWELL

Comments