Kijana Betheli akiongea vizuri mara baada ya maombezi |
Siku ya 12 ya mkutano wa Mch. Josephat Gwajima ambaye ni Askofu wa
kanisa la Glory Of Christ Tanzania Church maarufu kama Ufufuo na Uzima,
imekuwa siku ya miujiza mingi, kuna na matendo makuu ambayo Mungu
ameyafanya katika viwanja vya Angle Shellaton jijini Arusha mojawapo
likiwa la kijana aitwaye Betheli aliyekuwa bubu asiyeweza kuzungumza kwa
miaka mingi; kuponywa ububu wake baada ya maombezi kutoka kwa Mch.
Gwajima.
Akiongea kwa furaha na huku akimtukuza Mungu mama yake mzazi aitwaye
Grace alisema, mbali na ububu uliokuwa ukimsumbua mwanaye; pia
alisumbuliwa na magonjwa mbalimbali kiasi kwamba alikuwa hawezi kula
chakula mwenyewe maana alikuwa ni mtu wa kulazwa kitandani tu kwa muda
wa miaka mitatu bila msaada wowote.
Mama mzazi wa Betheli akielezea tabu aliyoipata juu ya mwanaye |
Ili kudhihirisha kuwa anaweza kuongea mwenyewe Mch. Gwajima alimwambia
ataje maneno ambayo kwa hapo awali hakuweza kutamka kabisa; Kijana
Betheli aliongea vizuri akiwa ameponywa kabisa kwa kuyatamka kama
yalivyo. Baadaye Mchungaji akaamuru apewe maji naye aliweza kunywa
mwenyewe jambo ambalo hakuweza kulifanya kwa miaka mingi sana.
Kuelezea ushuhuda huo, mama yake alisema kuwa alisafiri na mwanaye
kutoka Moshi mkoani Kilimanjaro kuja Arusha kwaajili ya kuhudhuria
kwenye mkutano huo. Mama huyo ambye alijawa na furaha sana baada ya
kushuhudia mwanye akiongea mwenyewe alisema kuwa anamshukuru Yesu Kristo
sana kwa uponyaji wa mwanaye.
Alisema, miaka mitatu ya magonjwa yake alisumbuka naye sana kila mahali
bila mafanikio lakini ana mshukuru Yesu kwa kumweka huru mwanaye anasema
hana la kumpa bali ni kumsifu na kumshukuru Yesu Kristo.
Kijana Betheli akinywa maji mwenyewe baada ya kuponywa yaliyokuwa yakimsibu |
MUNGU KWETU SISI NI MUNGU WA KUOKOA NA NJIA ZA KUTOKA MAUTINI ZINA YEYE!!!
Comments