| Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula, Maisha ya ushindi Ministry | 
Ndugu BWANA YESU asifiwe.
Nakukaribisha katika somo hili ambalo ni chanzo cha machafuko makanisani na kwenye jumuia za au vikundi katika kanisa, pia jambo hili linaweza kuwa ni chanzo cha mtu kutokubarikiwa. Biblia inasema
Nakukaribisha katika somo hili ambalo ni chanzo cha machafuko makanisani na kwenye jumuia za au vikundi katika kanisa, pia jambo hili linaweza kuwa ni chanzo cha mtu kutokubarikiwa. Biblia inasema
{Yakobo 4:1-6 Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
 Mwatamani, wala hamna kitu, 
mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, 
wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu. Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba 
kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa 
rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.
Au mwadhani ya kwamba maandiko yasema bure? Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?
 Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.
} 
MUNGU huwapinga 
wajikuzao  na  huwapa 
neema  wanyenyekevu 
-Neno 
wajikuzao =kiburi 
Ikiwa 
mtu  yuko  na 
kiburi 
1- kiburi 
ni  kikwazo  cha 
makusudi  ya  MUNGU {Ayubu 
35:12Hulia huko, lakini hapana ajibuye, Kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
}   
2- Kiburi 
ni  kikwazo cha  uamsho {zaburi 12:3  Bwana ataikata midomo yote ya kujipendekeza, Nao ulimi unenao maneno ya kiburi;
} 
3- Kiburi 
ni  kikwazo  cha 
umoja {mithali
8:13Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
}
4- Kiburi 
ni  kikwazo  kwa 
kuwafikia  wanajamii ambao wanaihitaji kweli ya MUNGU {mithali 13 :10Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
}
5- Kiburi 
huzuia  neema  ya 
MUNGU  ndani  ya 
kanisa 
   na pia BIBLIA inasema 
{mithali 15:25 Bwana ataing'oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane. } PIA {mithali 16:5-8Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha Bwana watu hujiepusha na maovu. Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye. Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu. }
{mithali 15:25 Bwana ataing'oa nyumba ya mwenye kiburi; Bali atauthibitisha mpaka wa mjane. } PIA {mithali 16:5-8Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha Bwana watu hujiepusha na maovu. Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye. Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu. }
                          DALILI   ZA  KIBURI
1-   Kiburi 
ni  kukufanya maalumu  na 
wakipeeke 
Mfano 
dhehebu,rangi,elimu,ujuzi 
2- Kiburi hutuelekeza  kwenye 
roho  ya  kuhukumu
Mfano 
dhehebu,rangi,elimu,ujuzu
3- Kiburi 
hutufanya   kuangalia  yale 
tusiyo  yaona  na 
badala  ya yale tunayoyaona
Mfano 
sijafanyiwa jambo  fulani ambalo
nilitakiwa kufanyiwa
4- Kiburi 
huleta wivu 
-Unapo barikiwa unasema  ningepata 
na  kile
-kwanii 
abarikiwe mwingine  na  si mimi
5-  Kiburi  kinatufanya tuwaze  watu 
wengine  wananifikiliaje  na  si  MUNGU  
6-  Kiburi  hutufanya  tusiguse utukufu wa  MUNGU –sifa ,heshima,unataka upewe wewe  na si MUNGU 
7-Kiburi humfanya  mtu kuwa  na 
roho  ya kiburi  
Kiburi  kinatabia  ya kujihami na kujitetea .    
MUNGU akubariki sana na siku zote neno la MUNGU linatutaka tutengeneze kwa ile sehemu tuliyoanguka, kazi ni kwako ndugu tukumbuke kuwa MUNGU huwapinga wenye kiburi.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula
Maisha ya ushindi Ministry
MUNGU akubariki sana na siku zote neno la MUNGU linatutaka tutengeneze kwa ile sehemu tuliyoanguka, kazi ni kwako ndugu tukumbuke kuwa MUNGU huwapinga wenye kiburi.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula
Maisha ya ushindi Ministry

Comments