NGUVU YA KINYWA,
Mtu wa Mungu Nabii: Samson
Utangulizi: kila kinywa kina
nguvu sana nguvu ya kujenga au kuharibu kinywa kina nguvu ya kuuwa au
kufufua kinywa kina nguvu ya maamuzi kukusanya au kutawanya kupendezesha
au kuchafua kinywa kina nguvu ya kulaani na kubariki kinywa kina nguvu
ya kukupeleka Mbele au kukurudisha nyuma, kinywa kina nguvu ya kuokoa na
kina nguvu ya kupoteza, inatengemea jinsi utakavyo kitumia kinywa
chako, sasa katika somo Mungu atatufundisha namna ya kutumia hii nguvu
iliyoko katika kinywa, nguvu nini?
NGUVU:
Nguvu ni uwezo wakusababisha jambo unalolitaka litokee likatokea
kwa muda ule unaohitaji litokee, sasa nguvu isiyo na uwezo
wakusababisha jambo likatokea mimi siongelei ya namna hiyo bali mimi
naongelea ile nguvu yenye uwezo wa kusababisha jambo likatokea, haswa
nguvu iliyo katika kinywa, kwa mfano tuangalie maandiko matakatifu hapa,
Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.
Mhubiri 9 : 16
Mhubiri 9 : 16
Kwanini
hekima iwe na ubora kuliko nguvu alafu hapo hapo hekima hiyo inapokuwa
kwa masikini inadharauliwa na maneno yake hayasikilizwi hii inamaanisha
kumbe ili masikini asikilizwe kunahitajika nguvu ya kusababisha yeye asikilizwe,asababishe jambo litokee lionekene,
hekima inapokuwa kwako usipoitumia inahama kabisa inaenda kwa mwingine anayeihitaji wewe unabaki na kunywa kilicho na mizaha, hapo ndipo unamkuta mtu wakati wote amebakiza mizahaa tu,
Heri
mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama
katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
Naye
atakuwa Kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao
matunda yake Kwa majira yake, Wala jani Lake Halinyauki; Na kila
alitendalo litafanikiwa. Zaburi 1:1-3
Kumbe unaweza kuwa Na kinywa lakini ukawa hauna nguvu nao ukiongea
usisikilizwi, kinywa chako kitakuwa na Nguvu pale Mungu atapokuwezesha
vinginevyo nisawa na kuwa na mali ambazo hazitumiki,
Luka 21:15
kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.
Nanyi mtasalitiwa Na wazazi wenu, Na ndugu zenu, Na jamaa zenu, Na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu.
Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.
Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu.
Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.
Nanyi mtasalitiwa Na wazazi wenu, Na ndugu zenu, Na jamaa zenu, Na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu.
Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.
Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu.
Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.
Kusudi
kuu la Mungu kukupatia Kinywa ni kwaajili ya wewe kutabiri juu ya
maisha yako kwanza angalia maandiko Matakatifu usisubiri utabir aza
kutamka yale unayosukumwa ndani ya Moyo wako tabiri sasa usingoje
kutabiriwa, onyesha kuwa umekubali mbele za bwana
Ezekieli 37:11” Mkono
wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana,
akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa;
akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.
Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe.
akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.
Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe.
Ukiendelea
kufuatilia kwa karibu kwa habari ya Ezekieli utagundua sababu ya Mungu
kumleta katika bonde lile lililojaa mifupa. Kwanza, Imani ya Ezekieli
ilikuwa imani yenye matumaini. Ingawa hali halisi ya mifupa ilikuwa
imekwisha kauka, yeye alibaki na tumaini kuwa mifupa ile yaweza
kuishi.kwakuwa aliamini Mungu hashindwi na jambo,
Sasa hatua kubwa sana ya Mtu ni ile kudhihirisha kuwa mtu anamjua Mungu na kumtumaini kwa kila jambo na popote hata katikati
ya vita, au hali za kukatisha tamaa, au hana analolitegemea katika
maisha yake lakini bado anataja mambo yajayo, anataja matendo makuu ya
Mungu.na kuamini Mungu atatenda,
Mungu hataki ukate tamaa, wala umkufuru yeye katikati ya magumu au matatizo ukifuatilia
kwa umakini mkubwa katika maandiko matakatifu watu wakubwa katika
biblia hata walioitwa na Mungu, walipitia magumu lakini katikati ya
magumu hayo walitamka maneno ya ushindi.
Pia,
kutamka maneno ya matumaini katikati ya magumu kunakufanya utoke mapema
kwenye hali mtu aliyoko ila ukionyesha kushindwa unaruhusu uvamizi
Inawezekana
unapitia katika hali ngumu kwa sasa, lakini utakalolinena ukiwa katika
dhiki hiyo itakufanya utoke ukiwa shujaa au aliyeshindwa. Maamuzi
unayo wewe mwenyewe Na ndio maana hata Ezekieli alipowekwa mbele ya
mifupa mikavu na kuulizwa 'je mifupa hiyo nyaweza kuishi?' Naye alijibu
kuwa 'wewe Bwana wajua’ akionyesha kuwa hakuna jambo la kumshinda Bwana.
Na ndio maana hata alipopewa nafasi ya kutamka neno alitamka uzima. Ni
muhimu kujua maneno ya kutamka pindi unapopitia katika hali ngumu au
matatizo, unaweza ukaharibu au ukajenga
Ni
muhimu kujua unachokiongea leo ndicho utakachokiishi kesho wewe na
kizazi chako na jamii iliyokuzunguka wengine hujikuta wanaongea maneno
mabaya juu yao wenyewe, huku wakisahau kuwa ni shetani ambaye anawafanya
waongee maneno hayo ili apate nafasi ya kuharibu maisha yao baadaye.
Isaya
57:10 "ulikuwa umechoka kwaajili ya urefu wa njia yako, lakini hukusema
hapana matumaini, ulipata kuuhishwa nguvu zako, kwasababu hiyo
hukuugua"
kumbe watu hawa, hali yao halisi iliwafanya wakate tamaa ya kufika
wanapokwenda lakini pamoja na urefu wa njia bado walichukua hatua
walikiri kuwa matumaini yapo. Na kwasababu ya ukiri huo walipewa nguvu
mpya. Usikiri udhaifu, Mungu anayetenda miujiza yupo na ukimkimbilia
yeye, ataiondoa aibu yako na kukuvika heshima.
Hatua zake za nguvu zitasongwa, Na shauri lake mwenyewe litamwangusha chini.
Ayubu 18:7
Ayubu 18:7
Kumbe katika hatua kuna hatuwa zanguvu
na hatuwa lege lege sawa sawa na Neno la Mungu hatuwa za mtu zinasongwa
na shahuri lake mwenyewe, shahuri unalo wewe mwenyewe juu ya wewe
kuchukuwa hatua au kubaki kama ulivyo,
Kwa mfano:
Ukifuatilia habari ya Yusufu ambaye maisha yake yalianza kwa kuuzwa na
ndugu zake kwa wamisri. Na alipouzwa waliigawa kanzu yake maana yake
aliuzwa bila mavazi yaani uchi,
Lakini
akiwa Misri na matumaini yakaanza kuja likatokea jambo jingine la
kukatisha tamaa. Mke wa potifa akamsingizia kuwa anataka kumbaka, hivyo
akatupwa gerezani maisha nikukumbushe na hapa tukio linalofanana na la
mwanzo likamtokea baada ya Yusufu kusingiziwa na kukimbia Vazi lake
lilibaki mikononi mwa mke Potifa Hivyo anaondoka bila nguo tena nguo
alipatia Gerezani tena za wafungwa,
Katiaka
hali hiyo ni dhahiri kuwa Yusufu alikata tamaa kabisa. Lakini alipotoka
gerezani Yusufu akawa waziri mkuu, jiulize, Mungu aliyemfanya kuwa
waziri mkuu alikuwa wapi kipindi anauzwa? Au jiulize alikuwa wapi
kipindi anawekwa gerezani?
Ni muhimu kujua kuwa kupitia hali ngumu,au katika tatizo flani ukahisi
Mungu amekuacha, si kweli; Mungu bado yupo pamoja na wewe na matumaini
bado yapo. Yesu Kristo ni tumaini la kutosha kwenye maisha yako. Leo
sikia sauti yake hii ikisema Usiogope hali unayopitia . Pata muda
kuingia kwenye maombi na Mungu atakupa tumaini jipya leo. Inawezekana
unapitia shida za ndoa, matatizo kazini,katika biashara, vita shuleni,
roho ya kukataliwa mpaka umejihisi hakuna kesho ile uliyoiwaza.
Leo tambua kuwa hata Ayubu katikati ya dhiki kuu hakuwahi kumkufuru Mungu aliyemtumikia bali aliweka tumaini lake kwake na kwa saa sahihi matumaini makuu yalionekana.leo kwetu ni somo,
Kuna
mtu anasubiri somo kutoka kwako juu ya hali yako unayopitia sasa
usiposhinda utasababisha na wengine watapopitia hali kama yako washindwe
kama wewe unavyotaka kushindwa usikubali kushindwa Mwamini Mungu
Mtumaini kama walivyokusha kushinda wanavyotufundisha,
Hata
kama ndoto yako inaonekana inataka kuzimika,Huduma kisimati,
inawezekana ulikuwa na ndoto za kusoma katika maisha yako lakini sasa
unaona muda umeenda nakwambia bado lipo tumaini.ulikuwa na ndoto ya kuoa
au kuolewa ukahisi muda umeenda bado ushindi upo tena Inawezekana
madktari walikwambia kuwa mwisho wa kuzaa ni miaka 45 na wewe sasa
unajiona unaelekea huo umri ukiwa hauna mtoto lakini nakwambia neno
ambalo Yesu amenituma kwako nikuambie sema neno juu ya maisha yako
chukuwa hatua ya kufanya hivyo na subiri Mungu atende ukishatamka acha
kumsaidia Mungu kwakuharakisha, Mwache Mungu atende kwa majira yake,
usije juta,!!
Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Na miguu yangu haikuteleza.
Zaburi 18 : 36
Zaburi 18 : 36
Ndani
ya nafsi ya kila mwanadamu kuna hatua ndiyo maana kunawatu kimawazo
wako mbali sana hatakama hana kipato kibwa lakini anahatuwa kubwa sana
ndani ya moyo wake, jambo lolote linalotokea halitikei hivi hivi bila nguvu ya hatua kufanyika nayo inaanzia ndani ya moyo wa mwanadamu,
Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, Uovu usije ukanimiliki.
Zaburi 119 : 133
Zaburi 119 : 133
Mungu anaelekeza je hatua
zao ni ndani ya moyo wako sasa kama Mungu hayumo ndani yako ninani
atakayezielekeza hatua zako, ezekieli mkono wa Mungu ulikuwa juu yake
akaweza Kutabiri juu ya mifupa mkavu, je swali langu wewe unatabiri
wakati gani mkono wa Mungu ukiwa juu yako au ukiwa peke yako,
Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.
Mithali 16 : 9
Mithali 16 : 9
Omba maombi maalumu juu ya Hatua zako zote kwa kila jambo unalolifanya,
Mungu akubariki kwakufuatilia somo hili naamini Mungu ninayemtumaini ahatoyaacha maisha yako yabaki kama yalivyokuwa mwanzo,
Kwa msaada wa
ushahuri na maombi na maombezi wasiliana na yule Mtu wa Mungu Nabii
samson, kwa namba 0756 809 209 0653 22 42 19 ni Bure huduma hii,
DVD VCD Za Masomo ya Mtu waMungu Samson zinapatikana,wakati wote, umbali Usiwe kikwazo,Nabii Samson, piga simu 0756 809 209

Comments