Binti huyu hapa juu anaitwa
SARAH, mkazi wa Moshi mjini, alichukuliwa msukuleni na baba mkwe wake na
kumpeleka Singida kulima mashamba ya mahindi na alizeti. Binti huyu alionekana
kuchoka sana mara baada ya kurudishwa toka
msukuleni,jambo lililosababishwa na ugomvi uliotokea kati yake na
babamkwe wake. Sarah aliendelea kushuhudia kuwa mara baada ya kuanza kuita watu
wote waliochukuliwa misukule NJOOO KWA JINA LA YESU, gafla kulitokea ugomvi
huko alikokuwa amefungiwa hadi
kujeruhiwa katika mkono wake wa kulia. Binti huyu alionekana mwenye kuvimba sana mkono wake wa
kulia, alipoulizwa kuhusu gomvi wake na babamkwe wake umesababishwa na nini,
alieleza kuwa ilisikika sauti kubwa ya
kushtua na kutisha ikimuita ‘Sarah njooo kwa jian la yesu”jambo lililimfanya
babamkwe kumpiga na mpini wa jembe mkwe wake na kumfukuzia mbali. Jambo la
kushangaza, binti alizidi kueleza kuwa
mipini ya jembe waliokuwa wanatumia kulimia huko msukuleni ni mikono ya
wanadamu!! Hakika hakuna lililositirika ambalo halitajulikana. Sarah
amefunguliwa na yuko huru kwa jina la yesu.
USHUHUDA WA RATIFA SIRAJI
 |
HAKUNA
jambo gumu la kumshinda MUNGU! Hata hili
ni jepesi machoni pa bwana! RATIFA SIRAJI ni binti aliyekuwa wakala wa
shetani aliyechukuliwa kwa njia ya
kichawi na kuwekwa chini ya mto Wami huku kazi yake ikiwa ni kusababisha
ajali na
kuchukua matumbo ya uzazi ya wanawake kwa njia za kichawi na baada ya
hapo alidai wanawake huenda hospitali na kupimwa na kukutwa na matatizo
ya kizazi na huishia kukatwa. Jambo la kushangaza binti huyu
aliyeonekana mwenye umri mdogo aliezeza kuwa hata alipokuwa anarudishwa
alikuwa anatoka matekani alikuwa
ametumwa kusababisha ajari ya gari la
MASAMA-SERENGETI ili kuchukuwa vizazi vya akina mama watakao kuwa katika
gari
hiyo.
. |
Ratifa akikana kumfahamu rafiki yake ambaye wanafahamiana vizuri |
Jambo la kushangaza mara baada ya
kurudishwa binti alikuwa hamtambui mtu
yeyote hata yule aliyekuwa naishi nae nyumbani kwao. Hakika yake tunaokolewa
kwa neema, hata leo neema ya Mungu ya ukombozi kwa walioibiwa na kutekwa
imemfikia mtoto huyu na kumuokoa. Kwa kushuhudia zaidi alieleza kuwa mara baad
ya kusikia sauti yenye mungurumo ikimuita “NJOOO” bibi aliyefahamika kwa jina
la AMINA ambaye anadaiwa kumchukua na kumuweka mateka aliamua kumtupa katiaka
viwanja vya mashujaa. Binti alipata kuombewa na mchungaji kiongozi JOSEPHAT
GWAJIMA mpaka ufahamu wake na kumbukumbu zikarejea akawatambua ndugu zake. Yesu
ni Yule yule jana leo na hata milele.
 |
Ratifa Siraji akiwa amepona na ameshammpokea Yesu, na kuwekwa huru kutoka katika vifugo vya kumtumikia shetani
|
|
 |
Binti
aliyekuwa amechukuliwa msukule na hapa pichani akiwa amerudi anamshkuru
Bwana Yesu na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima. |
|
 |
HAPPY MANDALI ni
binti mwenye umri wa miaka 16, anaishi mjini Moshi, amepata kurudishwa
toka msukuleni alikochukuliwa na rafiki wa mama yake, ambaye ni mfanya kazi
mwenzake. 
Dada huyu anayeitwa happy alionekana mwenye huzuni kubwa iliyoambatana na kilio
kikubwa! Jambolilimfanya kuendelea kumsihi mchungaji kiongozi Josephat Gwajima
aendelee kumuita mama yake maana binti alidai kuwa amemuacha pia mama yake kule
msukuleni ARUSHA. Binti alizidi kusisitiza kuomba mama yake aitwe kwa kuwa
aliona mateso na taabu alizokuwa akizipata kule msukuleni.Maandiko lazima
yatimie kuwa mwana wa adamu alikuja kutafuta kila kilichopotea hata leo
walokuwa wamepote wanaonekana na kurudishwa kwa jina la YESU
USHUHUDA WA AISHA MOHAMED
 |
ASHA
MOHAMED ana umri wa miaka 19, amekuwa mjumbe
wa shetani kwa kufanyishwa mambo mazito na ya kutisha tangu akiwa na
umri wa
miaka 8. Asha ameweza kueleza mambo aliyoyatenda japo ilikuwa ni ngumu
sana kuongea kutokan na ukweli kwamba alikuwa anasikia uchungu sana kwa
kuwa alijiona kuwa mambo hayo yote hakuna wa kumsamehe makosa yake na
watu
wange mtenga.Lakini Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima alimshauri kuwa
Mungu anasamehe kila dhambi hata iwe na ukubwa kiasi gani, cha msingi
ni ukiri kuwa umekosa ujinyenyekeshe mbele zake na usiyarudie tena.
Hatimaye Asha akaelewa na akaanza kueleza, kuwa wakati anasoma darasa la nane nchini
Kenya, ulikuwa usiku wa manane walimjia kundi la watu wengi wakamzunguka
alikokuwa amelala na kumwambia unahitajika kijijini kwenu. Kulipokucha mchana wa
saa sita, walikuja wasichana 3, wakiwa uchi walimfunika machoni na gafla
alijikuta yuko kijijini kwao katikati ya kundi la wachawi wa kijijini.
Baada ya kuchukuliwa, alianza kufunzwa jinsi ya kuroga, na
mwalimu wake alimtaja kwa jina la Hamis. Asha liendelea kupewa kazi na
majukumu kama kubadilishwa maumbile na
kuwa mwanaume nakuanza kuwaingiia wanawake usiku jambo lililokuwa likisababisha
wanawake kuvunja ndoa zao. Na wakati mwingine alikuwa akiwaingilia wanawake kwa
kugeuzwa maumbile alikuwa nasababisha saratani na kupooza. Jambo la kusikitisha
sana Asha amekuwa mateka kwa muda wa miaka 11 huku chakula chake kikiwa ni
kunywa maji ya chooni!
Aisha
akionesha mkono ambao kulikuwa na kidole cha kichawi ambacho kilikuwa
kimeoteshwa kichawi kwa ajili ya kuwanyonya watu damu na kuwasababishia
kupooza.
Asha
aliendelea
kueleza kuwa alikuwa anatumia kucha yake ndogo ya mwisho kuchoma watu
shingoni na
kunyonya damu mpaka kumsababishia mauti.
Aliendelea kulia sana akidai kuwa amemnyonya damu mdogo wake mwenye umri
wa
miaka miwili, na pia alisema magonjwa kama ya saratani, na kupooza ni
magonjwa ambayo yeye alikuwa anatumwa awasabishiye watu wengi sana.
Aisha
Mohamed akiwa anakiri kuwa amechoshwa sana na kazi za ushirikina,
akasema anataka kummpokea Yesu, akamkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na
Muokozi wa maisha yake, na akaokoka. |
|
|
|
|
Comments