![]() |
Waumini wakitafakari hali iliyotokea kanisani hapo. |
Tukio hilo lililotokea majira ya saa saba usiku linamtaja Elia Lunyamila (35) ambaye ni mlinzi pia ni mwenyekiti wa vijana wa kanisa kuuawa akiwa amejumuika kwenye ibada na waumini wengine Alex Msakuzi na Tumsifu Pungu ambao hali zao zinatajwa kuwa taabani wakipatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kukatwakatwa na mapanga sehemu mbalimbali za mwili.
Askofu wa kanisa hilo Eliabu Sentoz amelaani tukio hilo akilitaja kuwa
ni la kinyama kwani limefanyika sehemu ya ibada akiwataka wananchi
kuungana pamoja kulisaidia jeshi la polisi katika kutoa taarifa
kuwabaini wahusika wa shambulio hilo na akiiomba serikali kuongeza nguvu
kukabiriana na wahalifu hao.
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ernest Mangu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mpaka sasa hakuna taarifa za kuibiwa kwa kitu chochote ndani ya kanisa, hali ambayo inalifanya tukio hilo kuwa na maswali mengi likihofiwa kufananishwa na yale ya uchomaji moto Makanisa.
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ernest Mangu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mpaka sasa hakuna taarifa za kuibiwa kwa kitu chochote ndani ya kanisa, hali ambayo inalifanya tukio hilo kuwa na maswali mengi likihofiwa kufananishwa na yale ya uchomaji moto Makanisa.
![]() |
Wananchi wakitafakari tukio hilo nje ya jengo la Kanisa la Gilgal Christian Centre lililopo Pasiansi Ilemela jijini Mwanza. |
![]() |
Ndugu na majirani pamoja na waumini waliomfahamu marehemu Elia Lunyamila aliyeuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa marehemu kuomboleza . |
![]() |
Askofu wa kanisa la Gilgal Christian Centre Eliabu Sentozi. Picha kwahisani ya Gsengo, Chanzo cha habari Mjapinc.blogspot.com |
Comments