MIUJIZA YA AJABU YATOKEA KANISANI KAWE PENTECOSTAL CHURCH(K P C)

Mchungaji Elly Botto akimshukuru MUNGU baada ya watu kutendewa miujiza na BWANA YESU, Kama unahitaji maombezi ni bure kabisa mtafute kwa namba hizi namba 0752965812 au pia unaweza kutafuta kwa namba 0719640642Masaa machache tu yamepita tangu ibada yenye nguvu za MUNGU ilipotokea Kanisa la Kawe Pentecostal Church(K P C) kwa mchungaji Elly Boto ambapo BWANA YESU ametenda miujiza ya ajabu kupitia maombezi yaliyofanya na Mchungaji huyo pamoja na watenda kazi wengine kanisani hapo ambapo waliokua wanateswa na uchawi, majini, mapepo ,mizimu , laana za ukoo walifunguliwa kwa jina kuu la YESU KRISTO waliokua hawawezi kutembea wanatembea sasa tukio la jabu zaidi ambalo Maisha ya ushindi tumeshuhudia ni dada mmoja ambaye alikuwa amechukuliwa ufahamu wake  kichawi na aliyemchukua ufahamu huo ni bibi yake lakini maombezi ya leo yamemfungua. Pata picha za maombezi hayo na miujiza iliyotokea na pia kama unahitaji ushauri na maombezi ya aina yeyote wasiliana na Mchungaji Elly Boto kwa namba 0752965812 au pia unaweza kutafuta kwa namba 0719640642. Pia unaweza kumtafuta mzee wa kanisa kiongozi kwa namba 0657361222. Na maombezi haya ni bure kabisa maana ni agizo la MUNGU alilosema wekeni mikono kwa wagonjwa nao watapata afya. tukio la ibada ya leo ni hili hapa.
Mchungaji Botto akiomba

Dada Ester akifunguliwa kwa jina la YESU KRISTO

Schola akiombewa koo lake ambalo lilikuwa limeziba lakini BWANA YESU akamfungua katika ibada hii

Maumivu ya tumbo yakiondolewa ndani ya mwili wa Prisca

Mama Juniour pokea uzima

huyu naye alifunguliwa

Hakuna cha pepo, jini, kibwengo wala kinyamkera katika jina la YESU KRISTO, Dada huyu alifunguliwa na kunisimlia ushuhuda mzito sana aliofanyiwa na bibi yake, siku nyingine nitakuletea ushuhuda wa dada huyu hapa hapa Maisha ya ushindi blog na page ya facebook.

aliingizwa katika maagano mabaya sana lakini BWANA YESU akamhurumia na kumponya

Veronica akimshukuru MUNGU baada ya kutndewa muujiza wake na BWANA YESU

Hata walishindwa kutembea lakini katika jina la YESU KRISTO uzima wake huja na kuwaweka huru

Kaka huyu akiombea na Mchungaji Botto

Hata kama uliteseka kiasi gani lakini Ukimtegemea BWANA YESU hakika unapona

Mapepo yakisalimu amri kwa BWANA YESU katika maombezi yaliyofanywa na mchungaji Elly Botto na mtumishi Paulo

Comments