MTOTO WA MCHUNGAJI APONYWA KATIKA MKUTANO WA MCH. JOSEPHAT GWAJIMA - MOSHI.





Mchungaji Kapange, wa mjini moshi baada ya kutoka kwenye mkutano wa Mch.Kiongozi josephat Gwajima, na kuona jinsi watu maelfu kwa maelfu wanavyo rudishwa kutoka katika vifungo vya shetani kwa kuitwa njoo na kuitiwa kwa Jina la Yesu, aliona ni vyema akajaribu kuyatumia maarifa na mamlaka hayo nyumbani kwake kwa mwane wa kike aitwaye Herrith
.



Baada ya kumuita kwa muda kidogo tu, mtoto akashtuka kwa nguvu sana, na kuanza kumuhoji baba yake ambaye ndiye mchungaji aliyeyabeba maarifa hayo kutoka mkutanoni, na kumuuliza hapa ni wapi baba?, mbona mimi skua hapa...

ndipo Mchungaji kapange alipo amua kukoleza moto na kumrudisha mtoto wake vizuri na baada ya hapo akamuweka ufahamu wake sawa kwa kumuombea tena kwa Jina la Yesu,na kumuwekea ulinzi wa Damu ya Yesu, ndipo mtoto alipoanza kutoa ushuhuda wake kuwa alikuwa anaishi kuzimu, na dude linaloaminika kuwa ni shetani aitwaye, mkuu wa kafara pia baba yake akamuuliza kwa nini kila siku nilipokuwa nakuuliza kama unashida yoyote hukuwa unasema? , mtoto akajibu kuwa alikuwa amefungwa na haoni na wala hawezi kusema, na alipohojiwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima wakati akitoa ushuhuda wake mbele ya mkutano alidai kuwa alikuwa amechukuliwa na mtu anayeitwa KANUMBA...na uwanja mzima ukalipuka kwa mshangao na haikuweza kujulikana kwa haraka ni kanumba yupi aliyemchukua, ama mwigizaji au ni jina la mchawi wa mtaani kwao.

"Na ndio maana kama kuna wakuchukia Duniani, ambaye anatakiwa abezwe na watu wote ni mchawi anaye "m-host"  shetani - -Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima akiwa katika picha ya pamoja, na baadhi ya waliofika mkutanoni na kupokea miujiza yao na kuwekwa huru kutoka kwenye vifungo mbalimbali vya shetani hasa hasa ilikuwa ni siku ya kuzivunja laana za familia, na kuwaweka huru ambao walikuwa wako msukuleni. Nyuma ya mchungaji kiongozi ni Mchungaji Mwandamizi Mkuu (SRP) Grace Gwajima na aliyevalia kofia ya kiaskari ni Mchungaji Mwandamizi (RP) Maxmillian Machumu.

Comments