![]() |
Baadhi ya wanakijiji ambao walimpa Kristo maisha yao katika huduma ya VHM. |
Huduma ya The Voice of Hope ministry (VHM) yenye makao makuu yake Mwenge jijini Dar es salaam chini ya mkurugenzi wake mchungaji Peter Mitimingi wameendelea kuwasha moto wa injili vijijini na kuleta matumaini kwa watu ambao walikuwa wakiteswa chini ya vifungo vya shetani kwa kipindi kirefu.
Ambapo hivi karibuni walikuwa katika vijiji vya Kilwa mkoani Lindi ambako kama picha zinavyojionyesha watu wengi wakiwemo kutoka dini nyingine wamempa Kristo maisha yao na kufunguliwa kutoka katika matatizo mbalimbali yaliyokuwa yamewafunga.
Huduma hiyo ambayo kwakawaida haifanyi kazi mijini au sehemu zinazofikika kwa urahisi, wamekuwa wakipiga kambi katika vijiji vilivyoshindikana kwa ushirikina na mateso mbalimbali ikiwa pamoja na sehemu ambazo hazijawahi kufikiwa na injili, mpaka sasa wametembelea mikoa ya Kigoma,Mbeya, Tanga ambako walivunja makao makuu ya wachawi, Pwani kama Mkuranga, Kilwa, Msanga na sehemu nyingine nyingi.
Pia huduma hii hurusha vipindi vyake kupitia radio mbalimbali za Kikristo nchini ikiwemo WAPO RADIO 98.1 FM au kwa njia ya mtandao popote ulipo duniani, kila siku za ijumaa na jumapili kuanzia saa 3:30 usiku ambapo unaweza kusikia mambo yanayoendelea vijijini na namna huduma hiyo inavyofanya kazi zake.
![]() |
Neno likasomwa. |
![]() |
Maombi yakafanywa. |
Comments