![]() |
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula wa Maisha ya ushindi ministry |
Vita sio
lelemama.Ni kufa na kupona.Tena
vita vyetu sisi “si juu ya
damu na nyama bali ni
juu ya falme
na mamlaka juu
ya wakuu wa giza
hili, juu ya majeshi
ya pepo wabaya
katika ulimwengu wa roho “{Wafeso
6:12}.Vita kali

Pengine
umekwisha waona hawa waliorudi nyuma wakaanguka.Usidhani kuwa mtu anayekata shaurikumwacha YESU huwa
wanajishtukia wameanguka kushindwa huku ni
sawa na usingizi.ukilala
kitandani unakuwa ukiwaza mambo
mengi au unazungumza na mwenzako. La ajabu ni kwamba
hujui unasinzia saa ngapi na dakika
ngapi na ukaacha kusikia hata kama utalala ukiangalia saa unayezungumza naye
anakuja kugundua kuwa anazungumza peke
yake tu wewe unatambua kuwa ulikuwaumesinzia wakati unapoamka,
ndivyo
ilivyo kwa maisha ya kiroho. Mtu
hawezi kujua lini hasa alipoanguka
Anakwenda taratibu hatua kwa
hatua akisogea nyuma na baadaye
anajikuta ameanguka amekwishatekwa na maadui
Maadui wetu
wana nguvu sana .Maadui hasa ni watatu
-Adui wa
kwanza ni shetani: ni kawaida watu wa
MUNGU kusema shetani ameshindwa Haleluya’’.Ni kweli Lakini hakufa ili kwa vile
ameshindwa na YESU amri jeshi mkuu amekimbia na kuzungukazunguka akikuta mtu
amebaki nyuma na amechoka basi anamteka
tu Yeye shetani kama simba angurumaye huzungukazunguka akitafuta mtu ammeze {1
petro 5:8}
Shetani siyo
mvivu anashughulika usiku na mchana akiwatafuta watu wa MUNGU ili aende
nao jehanamu Tusije tukasahau hili,
Biblia anasema kwamba tukeshe {tukae macho }
ili tumpinge atakapokuja kutushambulia .Tuwe tumevaa silaha zote za MUNGU ili
tupate kujikinga na kuzipinga hila zake {Wafeso 6:11}
-Adui wa pili ni mwili: Biblia inasema “mwili”, ina
maana ya ule utu wa kale, ile hali ya dhambi tuliyonayo kwa asili.mwili
hupambana na roho zetu Tena mwili huu {flesh} ni wa mauti.Paulo anaeleza vizuri
jambo hili katika {Warumi 7:15-24}
Upo
uwezekano wa kuishi kufuatana na mapenzi ya mwili k.m kutamani kuona wivu
kudanganya ili kukwepa hatari kutotii,n.k mwili upo karibu sana nasi tena ni
sehemu yetu.Ni adui wa hatari sana tumchunge
-Adui wa
tatu ni ulimwengu
Ulimwengu ni mambo yote yaliyo kinyume na MUNGU mambo
ya dunia k.m miundo ya jamii,siasa,mazingira,watu n.k
Ulimwengu una
dhiki BWANA hakutoa ahadi kwamba hatutapata dhiki {1thes.3:3,4} Dhiki ni
sehemu ya ukristo wetu Lakini ni vigumu kuvumilia dhiki kama njaa,uchi,ugongwa
na uchungu wa kifo.Hata hivyo ugumu huu siyo
kisingizio cha kushindwa kwetu.
Ulimwengu
hauna dhiki tu.Una raha pia.Raha nayo inaweza kabisa kutufanya tumwache BWANA
kwa mfano Dema, ambaye Paulo alimwita mtendakazi pamoja nami alikaa na
Paulo muda mrefu akihubiri .Lakini Paulo alipo fungwa gerezani
tunashangaa tukiona anamwandikia mpendwa wake timotheo kwa masikitiko akisema
“DEMA aliniacha ,akiupenda ulimwengu huu wa sasa {2timotheo 4:10}
Alikwepa
dhiki akakimbia raha wenzetu wengi wameangushwa na raha hizi kama mali,wapenzi,
vyeo n.k wanasahau kabisa wito waliloitwa na BWANA
Hata hivyo
maadui hawa wasitutishe.tunaye YESU,BWANA wa MAJESHI yule mwanamke aliyeitwa Hana,
alishuhudia akisema “Wala hakuna mwamba kama MUNGU wetu “{1samweli 2:22}
tunaweza kujiunga naye tukiimba
Moyo wangu
wamshangilia BWANA
Pembe yangu imetukuka katika BWANA
Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu
Kwa kuwa
naufurahia wokovo wako {1samweli 2:1}
Tujue tuko.
vitani vita vya kiroho, vya imani. tusiwe kama wajinga tukajisahau
Ndiyo maana
Paulo ,akijaa ROHO MTAKATIFU anatwambia ,”kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za
MUNGU mpate kuweza kushindana siku ya uovu ,mkiisha kuyatimiza yote ,kusimama
“{efeso 6:13}
Katika
sehemu inayifuata, tujaribu kuona silaha hizi za MUNGU zitakazotuwezesha
kumshinda shetani, mwili na ulimwengu,
na kukua kiroho.
MUNGU awabariki sana ndugu wote.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
MUNGU awabariki sana ndugu wote.
Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.
Maisha ya ushindi ministry.

Comments