Mkutano wa Injili unaoendelea katika eneo la Vijibweni Soweto kata ya
Kigamboni, Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. Bwana ameendelea
kujidhihilisha kwa namna ya ajabu huku Mtumishi wa Mungu Cosmas Chidumle
akiendelea kuwa chombo kinachotumika kuwaleta watu kwa Bwana Yesu.
Kati ya vivutio katika mkutano huo ni uwepo wa Mtumishi wa Mungu
Betrice William aliyekuwa mshiriki wa Bongo star search akijulikana kwa
wimbo wa KUSAKA MAHELA baada ya kuokoka amejikita katika uinjilisti kwa
njia ya uimbaji sasa anakuambia SIO KAWAIDA WATAHEMEA JUU JUU, Wimbo
ambao ukiimbwa uwanja wote unaitika kwa shangwe kama ilivyo kawaida kwa
Betrice William kulitawala jukwaa.
![]() |
Beatrice William(Beatrice wa BSS) akiimba Watahemea Juu juu
![]() |
NEEMA JECKONIA
Kivutio kingine katika mkutano huo ni Muimbaji anae jua kulitumia vyema
jukwaa kiasi kwamba halimtoshi inabidi ashuke chini ni Mrs Chavala au
Neema Jeckonia ambaye hakufanya makosa alipo karibishwa aimbe wimbo wa
MWENYE UWEZA ulio katika mahadhi ya Segele. Hakika Yesu anasifiwa kwa
namna tofauti.
![]() |
Frola Fabian kama kawaida akimtukuza MUNGU |
Mtumishi Cosmas Chidumle akihubiri
Kama ilivyo katika mkutano mwisho alisimama Gwiji la Mziki(Mwana Mziki
halisi) ambae kwa sasa anamtangaza Yesu kwa Nguvu zake Mwinjilisti
Cosmas Chidumle. Aliwaambia wakazi wa Vijibweni kuwa Kama ni Uhuni yeye
alikuwa Mhuni zaidi, kama ni usharobaro basi alikuwa hivyo ila wa enzi
hizo. Pamoja na maisha ya kujulikana aliyoyaishi kipindi hicho hakuwa na
furaha kwani alikuwa amepungukiwa kitu. Yesu alipoingia katika maisha
yake maisha yake yamekuwa ya tofauti sana. Mwinjilisti huyo aliutumia
dakika kumi kuhubiri kutokana na kuchelewa kufika lakini hio ilikuwa
Ijumaa lakini Jumamos Mungu anaenda kutembea kwa njia ya ajabu ambapo
Mtumishi atasimama mapema na watu kwenda kufunguliwa.
Katika mkutano huo watu walimkubali Bwana Yesu na kuongozwa sala ya toba.
MKUTANO HUU UNALETWA NA KANISA LA P.A.G.
Comments