JINSI YA KUONDOA MATATIZO YOTE YA MAISHA

KKUTOKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA-MOSHI   

Na Mchungaji Kiongozi: JOSEPHAT GWAJIMA 
 
 
Matatizo haya yanaweza kuwa ya ndoa,ama ya kifamilia,ama ni matatizo ya kimaisha ama ni ya kibiashara.
Matatizo mengi katika maisha yanaondoka kwa;
  •   Kuombewa

  •   Kusoma neno.

Lakini kuna namna moja ya kumaliza matatizo yote,ambayo hii ndiyo nataka nishirikiane na wewe,na wewe ukiishika utashangaa sana,hebu tuiangalie namna hiyo kwenye maandiko matakatifu.
Kutoka 23:25 
 “Nanyi mtamtumikia Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako”.

Faida za kumtumikia Mungu.
  • Mungu atabarikia chakula chako.
  • Mungu atabariki maji yako. 
  • Mungu anakuondolea ugonjwa kati yako
  • Hapatakuwa na mtu mwenye kuharibu mimba.Maana ya kuharibu mimba ni kwamba kila kitu unachokianza kinaharibika kabla hujakimaliza

  • Hapatakuwa na aliye tasa.
  •  Atawafadhaisha wote watakaokufikiria. Kila mtu atakayefanya vita na wewe atafadhaisha na ataachana na wewe
  • Hesabu ya siku zako ataitimiza
Kutoka 23:26 “Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi    yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza”.

  • Bwana Mungu atatuma utisho wake utangulie mbele yako.

  • Bwana atawafanya hao adui zako wakuoneshe maungo yao.

     Kutoka.23:27 
 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao”.

Utamtumikiaje Bwana Mungu.?
Watu wengine wanafikiri ili kumtumikia Mungu lazima uwe huna au uache kazi yako,Haiko hivyo maana kuna  Watu ambao walimtumikia Bwana huku wakifanya kazi zao kama kawaida, tuwaone wachache kutoka kwenye Biblia;

1.DANIEL.
-Alikuwa makamu wa watu wa Raisi.
Danieli 5:29 “Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake, wakapiga mbiu kutangaza habari zake, ya kwamba yeye ni mtu wa tatu katika ufalme”.
-Mbunge wa jimbo la Babeli.
Danieli.2:48 “Basi mfalme akamtukuza Danieli, akampa zawadi kubwa nyingi sana, akamfanya kuwa mkubwa juu ya uliwali wote wa Babeli, na kuwa liwali mkuu juu ya wote wenye hekima wa Babeli”.
-Waziri mkuu.

Danieli 6:1-3
“1.Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote;
 2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danieli alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.
 3 Basi Danieli huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote”.

2.LUKA,amabaye alikuwa Daktari.

Wakolosai 4:14 “Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu”.

3.MTUME PAULO.
   -Alikuwa mshona mahema
Mdo 18:1-4 “1.Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho.
 2 Akamwona Myahudi mmoja, jina lake Akila, mzalia wa Ponto; naye amekuja kutoka nchi ya Italia siku za karibu, pamoja na Prisila mkewe, kwa sababu Klaudio amewaamuru Wayahudi wote watoke Rumi, naye akafikilia kwao;
 3 na kwa kuwa kazi yao ya ufundi ilikuwa moja, akakaa kwao, wakafanya kazi pamoja, kwa maana walikuwa mafundi wa kushona hema.
 4 Akatoa hoja zake katika sinagogi kila sabato, akajaribu kuwavuta Wayahudi na Wayunani”

4.LIDIA.
-Alikuwa akiuza rangi ya zambarau.
 Mdo.16:13-15 “13.Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.
 14 Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambaye moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo.
 15 Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.”.

5.MAWAKILI WALIOMTUMIKIA BWANA.
Luka 8:1-4 “1.Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,
 2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,
 3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
 4 Mkutano mkuu ulipokutanika, na wale waliotoka kila mji wakimjia, alisema kwa mfano”


Comments