MPENDE MUNGU ILI UYAFIKIE MAFANIKIO YA MAISHA YAKO


RUM 8:28

UTANGULIZI
Ahadi hii ni kwa wale tu wampendao Mungu na wajinyenyekeshao kwake kwa njia ya imani katika Kristo (Zab. 37:17).

Mungu anafanya kazi na wale wampendao.

I. SIRI KUBWA YA MAFANIKIO YA MTU NI:
1. Kumpenda Mungu. 
Mungu anafanya kazi na watu manaompenda.
Wale wampendao ndiyo anafanya kazi nao.

Alifanya kazi na Petro ambaye hakusoma akawaacha wasomi makuhani. Miaka 40 kiwete hajawahi kuingia hekaluni akakutana na watu wanaompenda Mungu akapona; angali makuhani wasomi walikuwepo wasiweze kutumiwa kumponya wa huyo kiwete.

2. Ukimpenda- Utajulikana naye (1Kor. 8:3).

Hata kama serikali, balozi n.k. hawakujui lakini wewe unajulikana na Mungu.

Ukijulikana na Mungu matatizo yako yatakuwa bayana, hata kama unapitia mambo magumu, lakini unajulikana mbele zake.

II. UKIMPENDA MUNGU IKO SABABU (2Kor. 3:5-6)

Unatoshelezwa na Mungu.

Hautoshi wewe mwenyewe.

Hautoshi na elimu yako.

Hautoshi na nguvu zako, uwezo wako, Mungu ndiye aingilie kati ndipo utoshelevuwako utatosha.

“TUNATOSHELEZWA NA MUNGU TU”

Adui wakikufuata yeye anajitokeza adui- anakimbia.

“UKIMPENDA MUNGU YEYE ATAKUTOSHELEZA”

Siku zako zitazidishwa (Mit. 9:11).

Hata kama wachawi, wabaya watakutafuta, Baraka zaozitaongezwa; siku zitaongezwa.

Yakatae magonjwa yapeleke kwa wale wanaokuchukia. (Kumb. 7:15)

Utastawi (Zab. 72:7, 92:13b)

Atakuwa na amani (utulivu, uponyaji, uzima, furaha n.k.)

Utazaa matunda (Zab. 92:14)

Utakuwa na ubichi, Bwana atakubariki mpaka uzee wako.

Ibrahimu akiwa na kama miaka 90 ndiyo anazaa, miaka haijalishi mbele za Mungu. Usibabaike kwa miaka mingi kupita.

MUNGU TUNAYEMHUBIRI NI MUHIMU AFANYE MUUJIZA KATIKA UZEE

Tunaye atutimiziaye mambo yetu (MUNGU) “mwite” (Zab. 57:2). Hata kama afya yako imechukuliwa, elimu yako imechukuliwa- Mungu hajabadilika, kama aliokoa, anaokoasasa, kama aliponya ataponya sasa, atabariki.

Utanenepa (Neh. 9:23-25)

Bwana akutishie wenyejiwa nchi hiyo (unakofanya kazi, unakoishi) ndiyo maana wachawi, mapepo tunayatenda kama tupendavyo/ tutakavyo.

Nawe utawatenda wachawina wafuga majini kama utakavyo.

Wakala, wakashiba, wakanenepa. KUNENEPA NI MPANGO WA MUNGU. Bwana akupe kula na kushiba na kunenepa. Funga nzuri ni pale ambapo mtu ana chakula cha kutosha.

Ukimpenda Mungu, atakupa kula na kushiba, kunenepa.




“JIHOJI UNAMPENDA MUNGU?”

Prepared by; Rev. Joseph Marego Mob: +255754334640/ +255712498080

Comments