TUKO HURU KWA SABABU YESU KRISTO AMETUWEKA HURU


ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula




BWANA YESU asifiwe ndugu.


MUNGU amekupa uzima na nafasi ya kujifunza somo hili kwa kusudi lake maana ana mpango mwema sana na wewe.


 karibu.


Tuko huru kwa sababu BWANA YESU ametuweka huru

Unadhani uhuru huo ni upi?

Uhuru ulianza lini?

Uhuru wetu unaanzia Golgotha/ Kalvari pale msalabani ambapo BWANA katika kuukamilisha uhuru wetu na kutupa wokovu alisema IMEKWISHA-Yohana 19:30.

-IMEKWISHA = yaani hatuhitaji  tena kuwafuata waganga wa kienyeji ili kutuponya, hatuwezi tena kuwafuata wasoma nyota, wasoma bao, wasihiri wala hatuhitaji tena kutumia mazindiko ya aina yeyote, hatupaki tena dawa ya kuondoa mikosi  wala hatupulizii tena udi na uvumba  maana BWANA YESU ametuweka huru.


-Tunakuwa huru kwa kumpokea BWANA YESU kuwa BWANA na MWOKOZI wa maisha yetu.


- Tukimpokea BWANA YESU tunakuwa watoto wa MUNGU (Yohana 1:12- 13 ''Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake;
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU.'' )
.


-Tukimpokea BWANA YESU tunakuwa na kibali na haki ya kutokuvamiwa wala kuonewa na wachawi, majini au mapepo.(Isaya 54:17) Hivyo ndugu ni wajibu wako tu leo kumpokea BWANA YESU moyoni mwako na baada ya hapo utakuwa na kibali na haki ya kuharibu kazi zote za shetani.

 omba  tu  leo kwamba wachawi waachie watoto wako kwa jina kuu la YESU KRISTO.


-Tuko huru kwa sababu BWANA YESU ametuweka huru.


-Katika kukamilisha ukombozi pale msaabani

=PAZIA LA HEKALU LILIPASUKA.(Marko 15:38) hiyo inamaanisha mapazia yote waliyokuwekea adui zako  ili usipandishwe cheo kazini tunayapasua leo kwa jina la YESU KRISTO,


Shetani amewafunika ukoo wenu  kwa pazia  ili kwamba kila mtoto anayezaliwa katika ukoo wenu lazima avishwe hirizi shingoni, kiunoni, mikononi, miguuni tena anavishwa haya baada tu ya kuzaliwa. Lakini leo tunaondosha utawala huo wa shetani kwa jina la YESU KRISTO aliyetuweka huru.

Ndugu utakuwa huru kama BWANA YESU KRISTO akikuweka huru.


Shetani amewawekea pazia/ mpaka ukoo wenu hamtakiwi kusoma hadi chuo kikuu nyie ukoo mzima mmeishia darasa la saba tu, leo tunapasua pazia hilo kwa jina la YESU KRISTO anayeweka watu huru mbali na shetani.


-Ndugu ukimpokea BWANA YESU hakika utakuwa huru na yeye anasema katika Yeremia 15:20-21(Nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema BWANA. Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha. ).


Ndugu, shetani haogopi jina lolote ila anaogopa jina la YESU KRISTO pekee, na unajua kwa nini shetani na malaika zake wanaogopa jina moja tu yaani jina la YESU KRISTO? Biblia katika Mathayo 28:18 inajibu swali hilo.''YESU akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. ''


-Tunapozungumzia jina la YESU KRISTO tunazungumzia mamlaka ya maamuzi kwa kila jambo, mamlaka ya YESU KRISTO ni ya mwisho kwa utukufu wa MUNGU BABA.

Ndugu, itumie mamlaka hii shetani na watoto  wake yaani magonjwa, wachawi na majini wataogopa na kukukimbia.

Ndugu yangu,

-BWANA YESU alipokuwa katika kukamilisha wokovu wetu tukio jingine lililotokea ni

 =MAKABURI YA WATAKATIFU YALIFUMKA na watakatifu wakatoka makaburini (Mathayo 27:22).

Kaburi ni kitu chochote kilichokufunga ili shetani akutese, kaburi linaweza kuwa ni ugonjwa, ukimwi,umaskini,kufeli masomo kila siku N.k.

Wewe ni mmoja wa watakatifu hao ambao kaburi lililokufunga lazima liachie kwa jina la YESU KRISTO, Makaburi ya magonjwa lazima yafumke na wewe mtakatifu wa MUNGU utoke salama.


-Makaburi ya madeni lazima yafumke na wewe utoke salama.

Makaburi ya kuteswa na maroho ya ukoo, mizimu na mapepo lazima leo yakuachie wewe uliyeko kwenye makaburi hayo kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.


Utakuwa huru mbali na ukimwi unaokutesa kwa jina la YESU KRISTO, na mimi katika maisha yangu ya wokovu nikiwa Zanzibar tuliwahi kumwombea dada mmoja aliyekuwa na ukimwi ambaye alikuwa ameshapima hospitali tatu yaani Mnazi mmoja, Bububu na Al-rihma ambazo ndizo hospitali kubwa zaidi Zanzibar lakini pote alikutwa na ukimwi, walimleta kanisani tukamwombea baada ya maombezi akaondoka sikumwona tena ila baada ya wiki 2 nikiwa natoka Darajani naenda chukwani niliposhuka tu kituo cha chukwani mwisho nikasikia mtu akiniita kwa nguvu sana akisema ‘’Mchungaji, mchungaji, mchungaji’ nikageuka nikamkuta ni yule dada ambaye wiki mbili nyuma aliletwa kanisani akiwa kakonda na mwili wake kubaki mifupa na hadi ndugu waliokuja nae walikuwa wanamwogopa kwa jinsi alivyokonda lakini kwa maombi BWANA YESU akashuka na kumweka huru. Na alijikuta akinikimbilia kwa furaha huku akiniita mchungaji kumbe wala mimi sio mchungaji ni muumini tu kanisani, na aklikuwa amepima Hospitali 4 tofauti na kukutwa hana tena ukimwi, sifa,heshima, adhama na utukufu ni kwa BWANA YESU anayefungua watu, ndugu mpe maisha yako leo na utakuwa huru tena huru kabisa. Na ninapokueleza juu ya kuwekwa huru nimeona kwa macho yangu matendo hayo makuu ya BWANA YESU akiwaweka watu huru mbali na magonjwa na mapepo na kila aina ya maonezi ya shetani. Ndio maana 1Yohana 3:8 Iinasema kwamba ‘’BWANA YESU ALIDHIHILISHWA ILI AZIVUNJE KAZI ZA SHETANI.’’

Ndugu Biblia inasema ukikubali na kutii utakula mema ya nchi. Na leo mimi nakuambia kwamba ‘’UTAKUWA HURU KAMA BWANA YESU AKIKUWEKA HURU’’


Peter MichaelUtakuwa mbali na uchawi, mbali na mikosi, mbali na balaa, mbali na kifo cha ghafla cha kusababishwa na shetani.

Utakuwa mbali na kifo cha mapema bali JEHOVAH MUNGU atatimiza hesabu ya miaka yako aliyokukusudia.

Mpe YESU maisha yako leo ndugu maana ukiwa ndani ya KRISTO Tazama umekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita na sasa yamekuwa mapya (2 Kor 5:17)


YESU akikuweka huru kakika utaishi MAISHA YA USHINDI.

UTAKUWA HURU LEO KAMA BWANA YESU AKIKUWEKA HURU.

             Ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula.

                        -Maisha ya ushindi Ministry.

Comments