HAYA NDIO YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA INJILI,DAR KITUNDA-RELINI



Bwana Yesu asifiwe...
Haleluya...

Kumbe watu wanamuhitaji sana Bwana Yesu katika maisha yao tofauti na vile tunavyofikilia.
Nasema hivi; Wapo watu wengi sana wanaomuhitaji Bwana Yesu.
Kama utakuwa ni mtu wa kanisani tu kila siku huwezi kuyaelewa haya nisemayo, ni mpaka uwe na spirit/roho ya kuhudhuria mikutano ya nje ya injili,jaribu siku moja uhudhurie katika mikutano ya nje,mikutano ya injili na utadhibitisha hili nisemalo kwamba wapo watu wanamuhitaji Bwana Yesu sana kuliko vile unavyofikilia.

Watu wa namna hii hawawezi kuja kanisani wao wenyewe ili waokoke,maana shetani amewafunga kweli kweli.
Bali ili waokoke wanahitajika KUFUATWA MAHALI WALIPO.
Hapo sasa utanielewa.

Sasa, swali la kujiuliza,;
Ni nani awafuate?
Ili aziokoe roho zao?

Jibu lake nikalipata siku ya ya mkutano wa injili wa tar.12/12/13 hadi 14/12/13
Maana kupitia mkutano huo,nikaona watu wengi wakaokoka baada ya kuisikia injili ya kweli,walimpa Bwana Yesu maisha yao,pasipo kuwa na aibu yoyote ile.
Pale sauti iliposikika ya kuwaita wale wanaotaka kuokoka;

"Wale wanaotaka kuokoka,waje huku mbele. Usimuangalie mtu kwamba atakuonaje,Bali muangalie Bwana Yesu ambaye anakuita akutue hiyo mizigo uliyoibeba,
mizigo ya magonjwa,
mizigo ya umaskini...Njoo kwa Yesu nawe uwe huru,huru mbali na dhambi… "



Ulikuwa ni mkutano mzuri ambao ulikonga nyoyo za watu maana injili ya kweli ilisikika masikioni mwa watu.
Mtumishi Mwinjilisti Musa Gwau wa huduma ya living water center-kitunda ,alitumiwa vyema na Bwana kuchapa injili hiyo siku tatu,akishirikiana nami pamoja na watenda kazi.

Pichani ni baadhi tu ya picha zilizonaswa na mpiga picha wetu,picha zinazoonesha baadhi ya matukio kama vile;
01. Mwinjilisti Musa Gwau akihudumu.
02.Mwanamziki wa injili Enock akihudumu(Mzee wa zunguka-zunguka)
*Watenda kazi wakiombea mkutano
*Wana-praising wakisifu.
*Wale waliookoka katika mkutano huo wakiwa kanisani kwa maombezi zaidi.
* Mch.Devota akiwajibika katika kuwafungua wale waliookoka katika mkutano
*Waimbaji wa nyimbo za injili Tanzania wakienda sawa.,kama vile mwimbaji George Haule.
*Watu wakiwa katika mkutano.N.k




Hakika tulimuona Bwana siku hizo tatu.
Sifa na utukufu ni kwa BWANA.

Mtumishi Gasper Madumla.

UBARIKIWE.
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12

Comments