Je, UTAKUWA TAYARI!?



Neno linasema: "KWA SABABU HIYO NINYI NANYI JIWEKENI TAYARI; KWA KUWA KTK SAA MSIYODHANI MWANA WA ADAMU YUAJA" (Math 24:44)
=>Fikiria kama leo Kristo angetokea kwenye mawingu ya mbinguni, ni nani... Angekuwa tayari kumpokea?
=>FIKIRIA KAMA TUNGEHAMISHWA NA KUINGIZWA KWENYE UFALME WA MBINGUNI KAMA TULIVYO. Je, tungekuwa tayari kuungana na watakatifu wa Mungu, kuishi ktk upatanifu na familia ya Kifalme? UMEFANYA MAANDALIZI GANI KWA AJILI YA ILE HUKUMU? Je, umesawazisha mambo yako na Mungu? KUMBUKA KUWA KUKIRI KWAKO HAKUNA THAMANI Bila YA MATENDO YANAYOINGIA KWENYE MAISHA YAKO YA KILA SIKU.
Mungu anajua endapo tunazishika sheria zake ktk ukweli. Anajua kabisa lile tunalo(ifanya, tunaloliwaza na kulisema. Je TUNAJIANDAA KUMPOKEA MFALME? Atakapokuja kwenye mawingu akiwa na nguvu na utukufu mkuu, utaweza kusema, "TAZAMA HUYU NDIYE MUNGU WETU, NDIYE TULIYENGOJA ATUSAIDIE" (Isa. 25:9)? Kwa hao watakaosema, Kristo atawaambia, "PANDENI JUU ZAIDI Mkapokee TAJI YA UZIMA"

Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12 
MUNGU akubariki sana
by Renutus Mzurikwao

Comments