KWAHERI OPERESHENI TAKASIKA, KARIBU OPERESHENI WEZESHA

Baadhi ya walimu wa semina za operesheni Takasika.


 Kati ya mambo ambayo yamewatoa vijana kutoka hatua moja iliyochoka kwenda hatua nyingine madhuhuri na yenye matumaini kiroho na kimwili, basi ni Operesheni Takasika. Vijana kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam na viunga vyake wamefanikiwa kwa hatua kubwa kupata mabadiliko kwenye maisha yao, na kumpa nafasi Roho Mtakatifu awe kiongozi wa maisha yao.

Gospel Kitaa ambayo imekuwa ikipata simu kadha wa kadha kwa nyakati tofauti kuhusiana na watu wanaohitaji kufika kwenye operesheni hiyo, imeshuhudia maelfu ya vijana waliofika kwa hatihati wakiondoka kwa amani na furaha, mara baada ya kupata mafundusho ya namna ya kuenenda maishani, kwenye kilele cha operesheni hiyo, ambayo imekuwa msaada mkubwa si tu kwa kanisa, bali pia kwa taifa kiujumla, katika kurejesha maadili, na kumrudia Mungu kwa waliogeuka kuwa baridi.
Askofu Sylvester Gamanywa

Mbeba maono wa operesheni hiyo, Rais wa WAPO Mission International, Askofu Sylvester Gamanywa, ambaye anaeleza kuwa ni wakati wa kurithisha maono kwa kizazi kipya, hachoki – na Mungu ambariki, kwani kwa hivi sasa ni mkakati wa kuhakikisha kuwa baada ya kupata muongozo wa Roho Mtakatifu, ifikapo mwaka 2028 vijana wa Kitanzania walioamua kuishi maisha ya uchaji Mungu wawe wamewezeshwa kifedha na wawe pia wamefanikiwa kujitegemea kiuchumi, kupitia Operesheni Wezesha.

Operesheni hii inakuhusu moja kwa moja, Gospel Kitaa itaendelea kukufahamisha kuhusiana na operesheni hii hatua kwa hatua kwa kadri ambavyo taarifa zitakuwa zikipatikana, na kama hukufanikiwa kuwepo siku ya hitimisho ya Takasika, GK itakuletea picha zote, jitayarishe.
 
chanzo:Gospel kitaa blog
 
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12