Kutana na Mtu wa Mungu pale katika Hema ya Kinabi Nyankumbu Mkoani Geita Tanzania,
USHINDI KATIKATI YA VITA
Utangulizi:
Kila mwanadamu
anayeishi hapa Duniani kwanza ifahamike lazima ana Adui anayepambananaye kila
siku Hayo mapambano ndiyo Ninayoyaita Vita lakini Baada ya Mungu kunipa Mafunuo
Haya ndipo nikafahamu pamoja na vita tunayopambana kila siku,Ushindi unaweza
kuoatikania katikati ya Vita, Yesu kristo ni Bwana wa vita, na Vita vyote
vinaanzia Rohoni, Bunduki Haiuwi bali anayeuwa ni Mtu,
Waefeso 6:12,
kushindana kwetu si juu ya Damu na mwili,
Ushindi maana yake ni nini?
Maana ya
Ushindi ni kufanikisha jambo ulilokuwa umekusudia kulifanya likafanikiwa maana
yake umeshinda ugumu au kizuwizi,hadi kufanikiwa, kushinda,kufaulu,kupita, ni
maana zinazoweza kukusaidia
Vita ni
Mapambano ya jambo flani amkubaliani nalo katika pande mbili, maana vita ina
pande Mbili ila siku ya siku lazima Ushuhudiwe ushindi upande Mmoja,
Fahamu kuwa Dui
yako Mkuu Niibilisi wale unaokutana nao katika uwanja wa mapambano ni
wafuasi,watumwa,watenda kazi,maaskari ila jemedari wao yupo nyuma yao,
Nilifundisha
siku mmoja kuwa ibilisi ni yule yule wa kila siku ila anajifunuwa au
kujidhihirisha kwa nanma tofauti tofauti kupitia Matukio Mbali mbali,
kwa Mfano
ukifuatilia Habari ya Ayubu, utagunduwa Matukio yote yaliyokuwa yamempata Ayubu
yaliruhusiwa na ndiyo kona Ibilisi alijifichia kutaka kumtatiza na
kumtenganisha Ayubu na Mungu,
Hatuwa ya kwaza ya Ushindi katikati ya
Vita
·
Usikubali kutenganishwa na Mungu kwa
Namna yeyote ile
·
Usikubali kutoa siri zako kwa Mtu yeyote
·
Usikubali kuruhusu uwoga ukaingia Ndani
ya Moyo wako
·
Ondowa Mitego ya adui kwa umakini
ujasiri huwa unaondoa Mitego iliyotegwa
na Maadui
·
Mtumaini Bwana Mungu wako siku zote nawe
Utakuwa salama,
Mithali 29:25 Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali
amtumainiye Bwana atakuwa salama.
katika vita
inatumika Nguvu ya kila Namna Ilimradi ushindi upatikane sasa watu wengi
wanaenda vitani Bila Nguvu ya kutosha kwakuwa kunakila ainaya mbinu na vifaa
vitakavyotumika na wewe lazima ufahamu kuwa unatakiwa uende na aina gani ya
viifaa,
Mambo ya kuzingatia katika kupata ushindi,
v
Lazima
umfahamu Adui yako vizuri si kwakusontewa kidole,
v
Lazima
ufahamu Kwa uhakika Maskani ya adui yako ni ipi,
v
Lazima
ufahamu Nguvu yake ni kubwa kiasi gani na ni ipi,
v
Lazima
ufahamu Mbinu zake,
Ndugu yangu
usijaribu vita ya kupoteza yaani vita
unayojuwa utashindwa lakini wewe unalazimisha kupambana ,na pia usianzishe vita
unayoona kuwa utashindwa maana itakumaliza,
Msome adui
yako vizuri kabila ya kuingia Uwanjani, jitasmini wewe mwenyewe juu ya
mapambano, kisha hakikisha Una Nguvu ya kutosha kupambana ndipo uanze vita,
Matendo ya Mitume 1:8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha
kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika
Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Mtu yeyote
Jasiri lazima kuna kitu anachokitegemea au kuna Nguvu anayoitegemea yamkini ni
Mali,fedha, Madaraka,yaani Mmlaka,Nguvu za Mungu,Nguvu za Giza,
Matendo ya Mitume 4:13Basi walipoona ujasiri wa Petro na
Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa,
wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.
Usiende vitani Peke yako Nenda na Bwana
wa Vita Yesu Kristo Mwana wa Mungu,
Matendo ya Mitume 5:29B Petro na mitume wakajibu, wakisema,
Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
Ushindi
katikati ya Vita Ni kwamba utaaza kuuona
ushindi kwanzia katikati kwakuwa aliye vitani na wewe ni Mkuu sana Yeye alishinda
vita alishinda mauti,aibu,Mateso, matatizo unayoyapitia siyo kushindwa bali ni
Dalili Ukombozi na ushindi Katikati ya hilo tatizo,
Tatizo ulilo
nalo ni vita Lazima lishugulikiwe likiachwa linasababisha Mauti
Utasa wako ni
Vita Lazima ushugulikiwe
Umaskini wako
Ni vita lazima Ushughulikiwe angalia
Upande wako yupo nani Mshindi au Aliyeshindwa, na Asikilizwe Nani? Ibilisi au Mungu?
Tafakari:
Ukitembea na Mtu aliyeshindwa atakupa
wewe Sababu ya kushiwa na Ghafla ukija shutuka Umishindwa kila jambo, Mbaya
sana,
Tito 2:15Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa
mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.
- 1 Petro 2:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.